Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ukoma, ni Ugonjwa unaosababishwa na mdudu anayeitwa mycobacterium leprae, mdudu huyu kwa kawaida uathiri sana sehemu za ngozi na sehemu za Neva mbalimbali za mwili
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma.
1. Kwa kawaida hapo mwanzoni kabisa Ugonjwa huu haukuwa na dawa , kwa hiyo watu waliopatwa na Ugonjwa huu walionekana ni watu wenye balaa kwa hiyo hawakuruhusiwa kuishi na watu wengine kwenye jamii, lakini kadiri siku zinavyokwenda kutoka siku moja kwenda nyingine watu wameelewa kuhusu Ugonjwa huu na dawa imepatikana kwa hiyo watu wanapona kwa kufuata mashariti mbalimbali.
2.ugonjwa huu uweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kugusana na mtu mwenye ukoma hasa wakigusana na maji maji ya mtu mwenye ukoma na hasiye na ukoma na pengine kwa njia ya hewa hizi , kwa hiyo watu wanapaswa kuwa makini wakati wanapoishi na watu wa ukoma ili kuweza kuepuka hali ya kusambaa kwa ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
3. Pia mgonjwa anaweza kuwa na Dalili mbalimbali kama vile kuharibika kwa ngozi, kuharibika kwa mfumo wa Neva, pengine mtu anaweza kuwa mgumba kama Ugonjwa umeingia mpaka ndani, pia kunakuwepo na kuharibika kwa mifupa na pengine mtu anaweza kuwa mgumba, kwa hiyo Dalili hizo uweza kuanza taratibu na kuenea taratibu kwenye mwili wa mtu na matibabu yasipotolewa mapema hali ya mtu huwa mbaya zaidi.
4. Kwa hiyo tunajua wazi kuwaa Ugonjwa huu una tiba na dawa zipo kwa hiyo hakuna sababu ya kuwatenga wagonjwa walioathirika na Ugonjwa huu kwa sababu matibabu yakitolewa ipasavyo Mgonjwa anapona Kawaida na kurudia kwenye hali ya kawaida,kwa hiyo watu wenye tabia ya kutenga wagonjwa wenye matatizo haya wanapaswa kupewa elimu ili kuweza kuwajali wagonjwa hawa ili waweze kupata matibabu ipasavyo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 kitabu cha Simulizi π3 ai web app π4 Madrasa kiganjani π5 Bongolite - Game zone - Play free game π6 web hosting
Post zinazofanana:
Sababu za Ugonjwa wa Shinikizo la juu la Damu.
Shinikizo la juu la damu ni hali ya kawaida ambapo nguvu ya muda mrefu ya damu dhidi ya kuta za ateri yako ni kubwa vya kutosha hivi kwamba inaweza kusababisha matatizo ya kiafya, kama vileΓΒ Ugonjwa wa Moyo.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa hepatitis A
Hepatitis A ni ugonjwa wa kuambukiza wa ini unaosababishwa na virusi vya Hepatitis A. Virusi ni mojawapo ya aina kadhaa za virusi vya Hepatitis vinavyosababisha kuvimba na kuathiri uwezo wa ini wako kufanya kazi.
Soma Zaidi...Matatozo katika choo kidogo, maradhi ya figo na dalili zake pia namna ya kujikinga na madhradhi ya figo
MATATIZO YA CHOO KIDOGO NA FIGOFigo ni kiungo muhimu sana katika uchujaji wa mkojo, na afya ya mfumo wa utoaji taka mwili.
Soma Zaidi...Aina za saratani ( cancer)
Posti hii inahusu zaidi Aina za kansa, Kansa ni Aina ya ugonjwa unaosababishwa na kuzaliana kwa seli ambazo sio za kawaida.
Soma Zaidi...Nini chanzo cha malaria
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu chanzo cha ugonjwa wa malaria
Soma Zaidi...Namna ya kumsaidia mtoto mwenye UTI
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.
Soma Zaidi...