Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ukoma, ni Ugonjwa unaosababishwa na mdudu anayeitwa mycobacterium leprae, mdudu huyu kwa kawaida uathiri sana sehemu za ngozi na sehemu za Neva mbalimbali za mwili
Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma.
1. Kwa kawaida hapo mwanzoni kabisa Ugonjwa huu haukuwa na dawa , kwa hiyo watu waliopatwa na Ugonjwa huu walionekana ni watu wenye balaa kwa hiyo hawakuruhusiwa kuishi na watu wengine kwenye jamii, lakini kadiri siku zinavyokwenda kutoka siku moja kwenda nyingine watu wameelewa kuhusu Ugonjwa huu na dawa imepatikana kwa hiyo watu wanapona kwa kufuata mashariti mbalimbali.
2.ugonjwa huu uweza kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kugusana na mtu mwenye ukoma hasa wakigusana na maji maji ya mtu mwenye ukoma na hasiye na ukoma na pengine kwa njia ya hewa hizi , kwa hiyo watu wanapaswa kuwa makini wakati wanapoishi na watu wa ukoma ili kuweza kuepuka hali ya kusambaa kwa ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
3. Pia mgonjwa anaweza kuwa na Dalili mbalimbali kama vile kuharibika kwa ngozi, kuharibika kwa mfumo wa Neva, pengine mtu anaweza kuwa mgumba kama Ugonjwa umeingia mpaka ndani, pia kunakuwepo na kuharibika kwa mifupa na pengine mtu anaweza kuwa mgumba, kwa hiyo Dalili hizo uweza kuanza taratibu na kuenea taratibu kwenye mwili wa mtu na matibabu yasipotolewa mapema hali ya mtu huwa mbaya zaidi.
4. Kwa hiyo tunajua wazi kuwaa Ugonjwa huu una tiba na dawa zipo kwa hiyo hakuna sababu ya kuwatenga wagonjwa walioathirika na Ugonjwa huu kwa sababu matibabu yakitolewa ipasavyo Mgonjwa anapona Kawaida na kurudia kwenye hali ya kawaida,kwa hiyo watu wenye tabia ya kutenga wagonjwa wenye matatizo haya wanapaswa kupewa elimu ili kuweza kuwajali wagonjwa hawa ili waweze kupata matibabu ipasavyo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 web hosting 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Chanzo cha VVU na UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo m ali mbali vinavyohisiwa kuwa chanzo cha UKIMWI
Soma Zaidi...Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu
Hapautajifunza rangi kuu za mkojo na dalili zako kiafya, mkojo mchafu na dalili zake
Soma Zaidi...MATIBABU YA FANGASI
Karibia fangasi wote hawa wanatibika bila ya ugumu wowote maka mgonjwa atakamilisha dozi.
Soma Zaidi...Ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu -multiple sclerosis
Posti hii inazungumzia kuhusiana na dadili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu ambao kitaalamu hujulikana Kama multiple sclerosis.
Soma Zaidi...DALILI ZA UTUMBO KUZIBA
Kuziba kwa utumbo ni kuziba kwa chakula au kimiminika kisipite kwenye utumbo mwembamba au utumbo mpana (colon). Kuziba kwa matumbo kunaweza kusababishwa na mikanda ya nyuzi kwenye fumbatio ambayo huunda baada ya upasuaji, mifuko iliyovimba au iliyoambuk
Soma Zaidi...Fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya fikra potofu kuhusu vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...