Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
Kwa nini Wengi wanaoswali hawafikii Lengo la Swala zao?
Miongoni mwa sababu ya wengi kutofikia malengo ya swala zao ingawa wanaziswali misikitini tena kwa jamaa ni;
Hawajui lengo halisi la swala.
Waislamu wengi huswali kwa lengo la kufutiwa madhambi na kupata thawabu na sio kuepukana na machafu na maovu, ambalo ndio lengo kuu la swala. Kupata thawabu na kufutiwa madhambi ni matunda ya swala.
Rejea Quran (29:45) na (72:23).
Waislamu wengi hawana ujuzi sahihi juu ya swala.
Pamoja na waislamu wengi kutekeleza swala zao kwa jamaa lakini wengi wao hawajui kabisa miiko, sharti na nguzo za swala ila wanafuata mkumbo tu.
Rejea Quran (7:205), (7:55) na (4:142).
Waislamu wengi hawahifadhi swala zao.
Pamoja na kuswali kwao bado wengi hawazingatii na kutekeleza kikamilifu sharti na nguzo za swala zao inavyotakiwa.
Rejea Quran (107:4-5) na (23:1,8).
Wengi hawaswali kwa Unyenyekevu swala zao.
Kukosa unyenyekevu (utulivu wa mwili, fikra na uzingativu) hupelekea mwenye kuswali kutofikia lengo na matunda ya swala.
Rejea Quran (29:45), (23:1-2) na (23:10-11).
Kutosimamisha Swala za jamaa ipasavyo.
Waislamu wengi hawaswali jamaa misikitini au hawazingatia sharti za swala ya jamaa kama kunyoosha safu ipasavyo, kugusanisha mabega, vidole, n.k.
Rejea Quran (23:1-2).
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 3207
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani
👉2 kitabu cha Simulizi
👉3 Kitau cha Fiqh
👉4 Kitabu cha Afya
Maana ya uadilifu na usawa na tofauti zao
Posti hii itakwenda kukufunza utofauti kati ya uadilifu na usawa Soma Zaidi...
Jinsi ya kuoga josho la kiislamu ( janaba, hedhi na nifasi)
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kuoga josho kisheria. Soma Zaidi...
Swala ya ijumaa, nguzo zake na suna zae, namna ya kuswali swala ya ijumaa
Soma Zaidi...
Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...
Zoezi la nne mada ya fiqh.
Maswali mbalimbali kuhusu fiqh. Soma Zaidi...
Sanda ya mwanamke na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
nini maana ya hadathi na ni zipi aina za hadathi na uchafu katika uislamu
Soma Zaidi...
Hukumu na sherei zinazohusu ajira na kazi katika uislamu
Wajibu wa KufanyakaziUislamu siyo tu unawahimiza watu kufanya kazi na kutokuwa wavivu bali kufanya kazi ni Ibada. Soma Zaidi...
Msimamo wa uislamu juu ya utumwa
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Mafungu ya urithi katika uislamu
Hspa utajifunza viwango maalumu vya kutithi mirathi ys kiislamu. Soma Zaidi...
Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini
Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...
Zijuwe Suna zinazofungamana na swaumu na funga ya ramadhani
Soma Zaidi...