Kusimamisha swala za faradh katika nyakati za dharura.


image


Kipengele hichi tutajifunza namna ya kusimamisha swala ukiwa safarini na vitani na nguzo zake.


6.4.Kusimamisha Swala za Faradh katika nyakati za Dharura.

-   Swala imepangiwa muda maalumu, isiswaliwe nje ya muda wake ila kwa udhuru wa kisheria.

-   Hapana ‘kadha’ (kulipa swala) au kuswali swala nje ya wakati wake bila dharura kisheria.

     Rejea Qur’an (4:103), (2:286), (2:185), (5:6).

 

  • Swala ya Mgonjwa
  1. Ameruhusiwa kutayammamu iwapo hawezi kutumia maji.

      Rejea Qur’an (4:43) na (5:6).

 

2. Kama mgonjwa hajimudu kujitwaharisha kwa maji au tayammamu na hana mtu wa kumsaidia, basi atatayammamu kwa ishara na kuswali kwa ishara (kifikra) pia.

      Rejea Qur’an (5:6).

 

3. Mgonjwa anaruhusiwa kuswali akiwa amekaa na kuelekea Qibla kama anaweza, na atarukuu na kusujudu kwa kukaa au kwa ishara jinsi atakavyoweza.

 

4. Iwapo hawezi kukaa basi ataswali akiwa amelala kwa ubavu akiwa ameelekea Qibla kama anaweza, vinginevyo ataelekea popote na kulala chali au kulala vyovyote awezavyo.

 

5. Mgonjwa anaruhusiwa kuchanganya swala na kuzifupisha kama msafiri kulingana na hali ya ugonjwa na mazingira yake.

  • Swala ya Msafiri

-     Muislamu akiwa safarini anawajibika kutekeleza swala kama ifuatavyo;

      Rejea Qur’an (5:6), (4:101) na (2:238-239).

  1. Anaruhusiwa kutayammamu kama maji yatakosekana au hakuna uwezekano wa kuyatumia ndani ya kipando. Kutayammamu kunafaa kwa kutumia ukuta wa chombo cha usafiri pia.

 

2. Anaruhusiwa kupunguza swala zenye rakaa 4 na kuswali rakaa mbili mbili ambazo ni Adhuhuri, Alasir na Ishaa tu.

 

3. Pia msafiri ameruhusiwa kuunganisha swala 2, Adhuhur na Alasir, Magh’rib na Ishaa tu kwa kuziswali muda mmoja, kwa kuzitanguliza muda wa swala ya mwanzo (Jamu’ Taq’diim) au kuzichelewesha na kuziswali muda wa swala inayofuata (Jamu’ Ta’akhiir)

 

4. Pia msafiri anaruhusiwa kuswali huku akiwa anatembea au anaendelea na safari kwenye kipando chake.

 

  • Kusimamisha Swala Vitani

Kusimamisha swala ya faradh katika uwanja wa vita ni kama ifuatavyo;

Rejea Qur’an (4:102-103).

 

-     Askari wagawanyike katika makundi mawili, ambayo yataswalishwa jamaa na imamu mmoja.

 

-     Swala itafupishwa kama ilivyo katika swala ya safari, kwa kuswaliwa rakaa mbili yenye rakaa 4.

 

-     Kundi moja litaanza kuswali na imamu likiwa na silaha zao na jingine likiwa katika ulinzi.

 

-     Imamu ataswali rakaa moja ya mwanzo na kundi la mwanzo, na watakaponyanyuka rakaa ya pili, kila askari atamalizia rakaa ya pili kivyake haraka na baada ya kutoa salaam atarudi kuchukua nafasi ya ulinzi.

 

-     Imamu atabakia amesimama katika rakaa ya pili mpaka kundi la pili litakapounga jamaa nyuma yake ndipo ataendelea kumalizia rakaa yake ya pili.

 

-     Imamu atakapomaliza rakaa ya pili atatoa salaam na kila askari atasimama na kivyake kumalizia rakaa ya pili haraka na kutoa salaam pia.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Funga ya ramadhan na nyinginezo
Nguzo za uislamu (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya kumuamini mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya uislamu.
Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya sura zilizochaguliwa
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Saratul-humaza
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Haki za raia katika dola ya kiislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kuzika-namna ya kuzika hatua kwa hatua
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya zakat
Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya kusimamisha uislamu katika dini
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...