Faida za kula Pilipili

Faida za kula Pilipili

Usiogope kuwashwa, kula pilipili ni nzuri kwa afya yako ia virutubisho vingi sana

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Faida za kula Pilipili

14.Pilipili kali. Watu wengi wamekuwa wakiacha kutumia pilipili etu kwa sababu ya ukali wake. Ila itambulike kuwa ijapokuwa ni kali lakini ila faida nyingi sana kwa afya ya mtu. Pilipili pia ina vitamini c ndani yake kwa kiasi. Vitamini hivi ni muhimu sana katika mfumo mzima wa kinga ya mwili dhidi ya magonjwa na wadudu shambulizi.

Pilipili zote zina vitamin A, C na K lakini pilipili nyekundu zimezidi wenzie. Wataalamu wa afya wanazungumza kuwa antioxidant, vitamin A na C vilivyomo kwenye pilipili husaidia katika kuzuia maradhi ya saratani na baadhi ya maradhi yanayohusiana na kuzeheka, na pia husaidia katka kuboresha mfumo wa kinga. Pia vitamin K husaidia katika kuganda kwa damu, kuimarisha mifupa pia husaidia katika kulinda seli.

Pilipili nyekundu ni chanzo kizuri cha carotenoid ambayo hutambulika kama lycopene, hii ni mujarabu sana katika kuzuia mwili kupata maradhi ya saratani ya kibofu, njia ya uzazi kwa kinamama na saratani ya kongosho.pia kuna carotenoid inayotambulika kama cryptoxanthin hii nayo hujulikana kwa uwezo wake wa kupambana na kuzuia mwili kupata saratani ya mapafu inayohusiana na uvutaji wa sigara.

Wataalamu wa afya wanatueleza kuwa pilipili husaidia katika kurekebisha mapigo ya moyo na kuongeza joto la mwili kwa muda wa dakika 20 baada ya kuila. Hii inaonesha kuwa mwili utakuwa na uwezo wa kuunguza mafuta na cholesteral za ziada kwa muda huo. Pia tafiti nyingine zinaonesha kuwa pilipili husaidia katka kupunguza athari za vidonda vya tumbo kwani husaidia katika kuuwa bakteria ndani ya tumbo.

Ndani ya pilipili kuna antioxidant iitwayo piperine. Wataalamu wa afya wanadai kuwa ulaji wa antioxidant husaidia katika kuimarisha afya ya mtu. Piperine inatambulika kwa kuwa na uwezo mkubwa wa kudhibiti na kulinda uharibifu wa seli. Pia ulaji wa pilipili husaidia katika kuimarisha afya ya ubongo.

Kwa ufupi pilipili husaidia sana kwa afya ya mlaji. Pia pilipili husaidia katika kuulinda mwili dhidi ya maradhi ya kisukari, saratani na maradhi ya moyo. Afya ya ubongo, kuimarisha mapigo ya moyo pamoja na kupunguza mgando wa mafuta kwenye mirija ya damu. Pilipili husaidia katika kuufanya mwili uweze kunyonya virutubisho muhimu kutoka kwenye chakula.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 1717

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Hizi ndio kazi za madini mwilini mwako
Hizi ndio kazi za madini mwilini mwako

Post huu inakwenda kukupa orodha ya madini muhimu kwa ajili ya afya yako.

Soma Zaidi...
Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume
Vyakula vya kuongeza nguvu za kiume

Zijuwe dawa za kuongeza nguvu za kiume, na vyakula salama vya kuongeza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula zaituni
Faida za kiafya za kula zaituni

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula zaituni

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula bamia/okra
Faida za kiafya za kula bamia/okra

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula bamia

Soma Zaidi...
Ni katika kiungo kipi cha mfumo wa mmeng'enyo wa chakula virutubisho hufonzwa?
Ni katika kiungo kipi cha mfumo wa mmeng'enyo wa chakula virutubisho hufonzwa?

Post hii itakupa elimu kuhusu mfumo wa mmrng'enyobwa chakula unavyo fanyankazi

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula passion
Faida za kiafya za kula passion

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula passion

Soma Zaidi...
Faida za chumvi mwilini (madini ya chumvi)
Faida za chumvi mwilini (madini ya chumvi)

Post hii inakwenda kukipa faida za madini ya chumvi mwilini.

Soma Zaidi...
Faida za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe
Faida za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula kunde, maharage, njegere, mbaazi na njugu mawe

Soma Zaidi...
Faida za vitamin C mwilini
Faida za vitamin C mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vitamini C mwilini

Soma Zaidi...