Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maumivu makali , kuna wakati mwingine mgonjwa anapata maumivu makali ya viungo na dawa mbalimbali uweza kutolewa kwa mgonjwa huyo lakini matokeo yake huwa ni kuendelea kwa maumivu kwa hiyo yafuatayo ni matokeo ya maumivu
Matokeo ya maumivu makali.
1. Mgonjwa ubadilika kimtazamo na pengine anaweza kufanana kama amechanganyikiwa.
Hali hii utokea kwa mgonjwa mwenye maumivu makali kwa sababu mgonjwa anafilili kwamba hatapona na hivyo uanza kubadilika na pengine kuwa mkali, juwa na hasira na pengine kufanana kama amechanganyikiwa na kupoteza mwelekeo.
2. Pengine kwa sababu ya maumivu akilala ukosa usingizi na ulala macho kila siku kwa mda mwingine utasikia anaongea mwenyewe usiku au anaita wale ambao hawaumwi na wamelala na aliwalalamikia kuwa wamemwacha na hawamjali kwa hiyo tiba ni lazima ili kumfanya mgonjwa akaweza kupona na kuwa kawaida.
3. Pengine maumivu yakiwa makali sana na wengine ushindwa kabisa kushiriki tendo la ndoa kabisa na hamu kwa wengine uisha kabisa kwa hiyo maumivu yakiwa ya mda mrefu yanaweza kusababisha kuvunjika kwa ndoa kwa hiyo ni vizuri kutibu maumivu mapema .
4. Maumivu pia yanaweza kusababisha kutengana kwa familia kwa sababu kama kutakuwepo na uzembe wa kutoshirikiana katika kuuguza Mgonjwa panaweza kuwepo na kutegeana na pia kama kipato ni kidogo na pia hiyo ni shida kubwa katika kumuuguza mwenye maumivu ya mda mrefu.
5.Kwa hiyo tunapaswa kutibu Magonjwa mapema kabisa ili kuepuka hatari ya kuwepo kwa maumivu ya mda mrefu kwa kufanya hivyo tutaweza kuwasaidia wagonjwa wetu pia na jamii iache tabia mbaya ya kuwanyanyapaa wagonjwa hasa wale walio kwenye maumivu makali.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
 Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo, kitaalamu huitwa Angina ni dalili ya Ugonjwa wa ateri ya Coronary. Ugonjwa huu kawaida hufafanuliwa kama kufinya, shinikizo, uzito, kubana au maumivu kwenye
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatari zilizopo kwa mtu mwenye uzito mkubwa,kwa sababu ya kuwepo kwa uzito mkubwa na pia unene usio wa kawaida usababisha mtu kuwa na matatizo mbalimbali hasa saratani za kila sehemu kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...hatari matokeo ya kunywa kiasi kikubwa cha pombe kwa muda mfupi. Kunywa pombe haraka kupita kiasi kunaweza kuathiri kupumua kwako, mapigo ya moyo, halijoto ya mwili na kunaweza kusababisha Coma na kifo.
Soma Zaidi...Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema.
Soma Zaidi...Kama mtu anatokwa na damu za pua, basi juwa kuwa anahitaji huduma ya kwanza.
Soma Zaidi...