Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.
Mtu aking'antwa na nyuki Kuna dalili ambazo huonekana Kama vile
1.kuvimba .
2.mapigo ya moyo kuenda haraka.
3.maumivu Tena maumivu haya huwa Ni makali Sana endapo umeshambuliwa na nyuki wengi.
4.kupoteza fahamu. Hii hutegemea na ulivyong'atwa
5.kuwa na kizunguzungu.
6.kichwa kuuma.
8.mwili kuwasha hii unaweza isitokee kwa wote kwasababu hutegemeana na mzio (allergy) wa mtu
Huduma ya kwanza kwa aliyeng'ntwa na nyuki.
1.linda usalama wako na usalama wa mgonjwa.hii husaidia ili na wewe unayemtoa usije ukang'atwa kwahiyo kabla ya yote unatakiwa kujiweka Safi.
2.mtoe kwenye Hilo tukio; baada ya hapo unamwondoa mgonjwa kwenye Hilo tukio ili kumsaidia asiendelee kung'antwa na nyuki.
3.mweke sehemu Safi yenye hewe na Kama inawezekana mweke penye baridi .
4.angali Hali ya mgonjwa Kama amepoteza fahamu kiasi kwamba ukimwita Kama anaitika, Kama anasikia maumivu ili ujue mgonjwa Yuko katika Hali gani.
5.angali mgonjwa Kama anapumua na mapigo ya moyo Kama yapo Kama hayapo mwahishe mgonjwa hospitalini.
6.mwondoe ncha za nyuki kwa kutumi kitu chenye ncha Kali Kama vile sindano,Pini n.k na kifaa hiko kiwe Ni kisafi hakijawahi kutumiwa na mtu yoyote ili kumwepusha asipate Magonjwa mengine na pia kumsaidia mgonjwa kuwa katika Hali nzuri.
7.mwekee barafu kwa kukandamiza ili Kupunguza au kuondoa uvimbe na maumivu na usikandamize Sana dakika kumi zinatosha maana ukikandamiza mda mrefu hupelekea kupata oedema.
8.kama unadawa za maumivu mpatie mgonjwa ili Kupunguza maumivu.
9.Angalia mabadiliko ya mgonjwa, ikiwa hayajabadilika mpeleka mgonjwa kituo Cha afya.
Mwisho; Kuna mambo muhimu ya kuangalia wakati mtu ameng'atwa na mdudu . utaangalia Kama hewa ipo, anapumua na mapigo ya moyo.kingine angalia Hali ya mgonjwa Kama anajielewa au hajielewi .
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
maumivu ya kichwa ni moja ya dalili za kiafya ambazo huashiria hali isiyo ya kawaida. hata hivyo maumivu ya kichwa yanaweza kutokea hata kama sio mgonjwa. Hapa nitakuletea sababu zinazopelekea kuumwa na kichwa mara kwa mara.Maumivu
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi umuhimu wa mate mdomoni, mate ni majimaji ambayo hukaa mdomoni na husaidia katika kazi mbalimbali mdomoni.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima,ni sababu ambazo umsaidie mgonjwa ili aweze kupata nafuu mapema na kumsaidia kama tutakavyoona hapo chini
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kumsaidia aliyeumwa na nyoka
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi faida ya chanjo, tunajua wazi kuwa chanjo Ina faida kubwa kwenye mwili wa binadamu na vile vile kwenye jamii kama tutakavyoona hapo chini.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu hasa jinsi uchafu, wadudu na vitu vingine vinavyoweza kuingia machoni.macho ni mojawapo ya milango mitano ya fahamu ambapo kazi yake ni kuona.
Soma Zaidi...Uke ni sehemu ambayo imo ndani ya mwili wa mwanamke, sehemu hii ufanya kazi mbalimbali hasa wakati wa kujamiiana, kubarehe na kujifungua kwa mama.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo, ni njia ya kuwasaidia wagonjwa waliopata madonda ya tumbo
Soma Zaidi...