Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?

Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?

Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.

   Mtu aking'antwa na nyuki Kuna dalili ambazo huonekana Kama vile

1.kuvimba .

2.mapigo ya moyo kuenda haraka.

3.maumivu Tena maumivu haya huwa Ni makali Sana endapo umeshambuliwa na nyuki wengi.

4.kupoteza fahamu. Hii hutegemea na ulivyong'atwa 

5.kuwa na kizunguzungu.

6.kichwa kuuma.

8.mwili kuwasha hii unaweza isitokee kwa wote kwasababu hutegemeana na mzio (allergy) wa mtu

 

Huduma ya kwanza kwa aliyeng'ntwa na nyuki.

1.linda usalama wako na usalama wa mgonjwa.hii husaidia ili na wewe unayemtoa  usije ukang'atwa kwahiyo kabla ya yote unatakiwa kujiweka Safi.

 

2.mtoe kwenye Hilo tukio; baada ya hapo unamwondoa mgonjwa kwenye Hilo tukio ili kumsaidia asiendelee kung'antwa na nyuki.

 

3.mweke sehemu Safi yenye hewe na Kama inawezekana mweke penye baridi .

 

4.angali Hali ya  mgonjwa Kama amepoteza fahamu kiasi kwamba ukimwita Kama anaitika, Kama anasikia maumivu ili ujue mgonjwa Yuko katika Hali gani.

 

5.angali mgonjwa Kama anapumua na mapigo ya moyo Kama yapo Kama hayapo mwahishe mgonjwa hospitalini.

 

 

6.mwondoe ncha za nyuki kwa kutumi kitu chenye ncha Kali Kama vile sindano,Pini n.k na kifaa hiko kiwe Ni kisafi hakijawahi kutumiwa na mtu yoyote ili kumwepusha asipate Magonjwa mengine na pia kumsaidia mgonjwa kuwa katika Hali nzuri.

 

7.mwekee barafu kwa kukandamiza ili Kupunguza au kuondoa uvimbe na maumivu na usikandamize Sana dakika kumi zinatosha maana ukikandamiza mda mrefu hupelekea kupata oedema.

 

8.kama unadawa za maumivu mpatie mgonjwa ili Kupunguza maumivu.

 

9.Angalia mabadiliko ya mgonjwa, ikiwa hayajabadilika mpeleka mgonjwa kituo Cha afya.

 

Mwisho; Kuna mambo muhimu ya kuangalia wakati mtu ameng'atwa na mdudu . utaangalia Kama hewa ipo, anapumua na mapigo ya moyo.kingine angalia Hali ya mgonjwa Kama anajielewa au hajielewi .

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views: 2450

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 web hosting     👉2 ai web app     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Njia za kujikinga na kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kujikinga na kisukari

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu vitamini C na kazi zake

Makala hii itakujulisha kazi kuu za vitamini C mwilini. Hapa pia utatambuwa ni kwa nini tunahitaji vitamini C na wapi tutavipata

Soma Zaidi...
Zijue sababu za kupoteza fahamu.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kupoteza fahamu, ni sababu ambazo umfanya mtu kupoteza fahamu kwa sababu mbalimbali kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Kazi ya protin na vyakula vya protini mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya kazi ya protin na vyakula vya protini mwilini

Soma Zaidi...
Njia za kukabiliana na presha ya kushuka

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kushuka

Soma Zaidi...
Yanayoathiri afya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mambo yanayoathiri afya

Soma Zaidi...