Je, utamsaidia vipi mtu aliyeumwa na nyuki?
Posti hii inazungumzia kuhusiana na kumsaidia mwenye aliyeumwa na nyuki.nyuki na wadudu ambao wakikushambulia Sana na ukikosa msaada unaweza kufa au kuwa katika Hali mbaya.
Mtu aking'antwa na nyuki Kuna dalili ambazo huonekana Kama vile
1.kuvimba .
2.mapigo ya moyo kuenda haraka.
3.maumivu Tena maumivu haya huwa Ni makali Sana endapo umeshambuliwa na nyuki wengi.
4.kupoteza fahamu. Hii hutegemea na ulivyong'atwa
5.kuwa na kizunguzungu.
6.kichwa kuuma.
8.mwili kuwasha hii unaweza isitokee kwa wote kwasababu hutegemeana na mzio (allergy) wa mtu
Huduma ya kwanza kwa aliyeng'ntwa na nyuki.
1.linda usalama wako na usalama wa mgonjwa.hii husaidia ili na wewe unayemtoa usije ukang'atwa kwahiyo kabla ya yote unatakiwa kujiweka Safi.
2.mtoe kwenye Hilo tukio; baada ya hapo unamwondoa mgonjwa kwenye Hilo tukio ili kumsaidia asiendelee kung'antwa na nyuki.
3.mweke sehemu Safi yenye hewe na Kama inawezekana mweke penye baridi .
4.angali Hali ya mgonjwa Kama amepoteza fahamu kiasi kwamba ukimwita Kama anaitika, Kama anasikia maumivu ili ujue mgonjwa Yuko katika Hali gani.
5.angali mgonjwa Kama anapumua na mapigo ya moyo Kama yapo Kama hayapo mwahishe mgonjwa hospitalini.
6.mwondoe ncha za nyuki kwa kutumi kitu chenye ncha Kali Kama vile sindano,Pini n.k na kifaa hiko kiwe Ni kisafi hakijawahi kutumiwa na mtu yoyote ili kumwepusha asipate Magonjwa mengine na pia kumsaidia mgonjwa kuwa katika Hali nzuri.
7.mwekee barafu kwa kukandamiza ili Kupunguza au kuondoa uvimbe na maumivu na usikandamize Sana dakika kumi zinatosha maana ukikandamiza mda mrefu hupelekea kupata oedema.
8.kama unadawa za maumivu mpatie mgonjwa ili Kupunguza maumivu.
9.Angalia mabadiliko ya mgonjwa, ikiwa hayajabadilika mpeleka mgonjwa kituo Cha afya.
Mwisho; Kuna mambo muhimu ya kuangalia wakati mtu ameng'atwa na mdudu . utaangalia Kama hewa ipo, anapumua na mapigo ya moyo.kingine angalia Hali ya mgonjwa Kama anajielewa au hajielewi .
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Chanjo zinazotolewa nchini Tanzania
Posti hii inahusu zaidi chanjo ambazo utolewa nchini Tanzania, ni chanjo ambazo uzuia Magonjwa ambayo yako katika sehemu mbalimbali za nchi.
Soma Zaidi...Namna ya kumhudumia mtu aliyeingongwa na nyoka
Posti hii inahusu njia na namna ya kumhudumia aliyeingiwa na nyoka. Nyoka ni kiumbe ambacho Kina sumu kali na mtu akifinywa na nyoka asipohudumiwa anaweza kupata ulemavu au kupoteza maisha
Soma Zaidi...Mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu.
Posti hii inahusu zaidi mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu, tunajua kubwa kifua kikuu ni Ugonjwa ambao utumia mda mrefu kidogo katika matibabu kwa hiyo mgawanyiko wake uko kwenye sehemu mbili muhimu kama tutajavyoona
Soma Zaidi...Mambo yanayoweza kudhoofisha kinga ya mwili
Kinga ya mwili inapodhoofu mwili unakuwa hatarini kupata maradhi. Je unayajuwa mambo yanayodhoofisha kinga ysbmeili?
Soma Zaidi...Kazi za vitamin B na makundi yake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu kazi za vitamin B na makundi take
Soma Zaidi...Dalili za sumu ya pombe
hatari matokeo ya kunywa kiasi kikubwa cha pombe kwa muda mfupi. Kunywa pombe haraka kupita kiasi kunaweza kuathiri kupumua kwako, mapigo ya moyo, halijoto ya mwili na kunaweza kusababisha Coma na kifo.
Soma Zaidi...