Mambo ambayo hayafunguzi funga


image


Hii ni orodha ya mambo ambayo hayawezi kuharimu funga yako endapo utayafanya.


Yasiyobatilisha funga

Kuna baadhi ya mambo ambayo mtu aliyefunga akiyafanya, anaweza kujiona kuwa amefungua lakini bado hajafungua. Miongoni mwa mambo haya ni:

 


(i)Kula au Kunywa kwa Kusahau

 


Mtu akiwa amesahau kuwa amefunga akala au akanywa kiasi chochote, hata kiasi cha kushiba, bado atakuwa na swaumu kwa ushahidi wa Hadith zifuatazo:
Abu hurairah(r.a) amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Anayefungua Ramadhani kwa kusahau hatalipa wala hatatoa kafara” (Daral Qutni, Bayhaqi na Hakim).
Abu Hurairah ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Yeyote yule atakayesahau akala au akanywa wakati amefunga, na amalizie funga yake kwa sababu Allah (s.w) amemlisha na kumnywesha ”. (Bukhari na Muslim).

 


Hali kadhalika, kama mtu atalishwa au kunyweshwa au kufuturishwa kwa namna yoyote ile kwa kutezwa nguvu, saumu yake haitabatilika:
Ibn Abbas (r.a) ameeleza kwamba Mtume (s.a.w) amesema: “Mwenyezi Mungu ameuondolea umati wangu (Jukumu la) kukosea, kusahau na waliotezwa nguvu.” (Ibn Majah, Ta bran na Hakim).

 


(ii)Kuoga wakati umefunga

 


Kuoga kwa kujimwagia maji au kujitumbukiza majini hakuharibu funga kwa maana imepokelewa kwamba Mtume (s.a.w) alikuwa akijimwagia maji kichwani kwa sababu ya kiu au joto, hali amefunga:

 


Mmoja wa Maswahaba ameeleza: Hakika nimemuona Mtume (s.a.w) akiwa Arji (bonde moja kati ya Makka na Madina) akijimwagilia maji kichwani mwake akiwa amefunga kwa sababu ya kiu au joto. (Malik, Abu Daud).

 

(iii)Kutokwa na Manii
Mtu akitokwa na manii kwa kuota au kwa namna ambayo hakukusudia, atakuwa hajafungua.

 


(iv)Kuamka na Janaba

 


Kuamka na janaba hakufunguzi kwani Mtume (s.a.w) wakati mwingine alikuwa anaamka na janaba na huku amefunga.
Aysha (r.a) ameeleza kuwa alfajiri iliingia wakati Mtume (s.a.w) yuko katika janaba. Kisha alioga na kuendelea na swaumu. (Bukhari na Muslim).
Hali kadhalika mwenye hedhi au nifasi, ambaye damu yake ilikoma kabla ya alfajiri, akiamka atafunga hata kama atakuwa hajaoga.
(v)Kubusiana na kukumbatiana Mume na Mke

 


Mtu kumbusu na kumkumbatia mkewe au mumewe wakati amefunga haiharibu funga iwapo kuna haja ya kufanya hivyo alimradi tu waweze kujizuia wasiendelee zaidi ya hapo. Hivi ndivyo tunavyojifunza katika Hadithi ifuatayo:
Aysha (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah alikuwa akimbusu na kumkumbatia wakati amefunga na alikuwa mw enye kumiliki matashi yake kuliko yeyote miongoni mw enu (Bukhari na Muslim).

 


Amehadithia baba wa Hisham kuwa: Aysha (r.a) amesema: “Mtume wa Allah alikuwa akiwabusu baadhi ya wake zake akiwa amefunga: na kisha akacheka. (Bukhari).
Miongoni mwa Masahaba walioruhusu hili la mtu kumbusu na kukumbatia mkewe wakati amefunga ni Sayyidna Umar (r.a), Ibn Abbas (r.a.), Abu-Hurairah (r.a) na Bibi Aysha (r.a). Kwa maoni ya Imam Abu Hanifa na Shafii, kumbusu na kumkumbatia wakati mtu amefunga ni makruhu iwapo kutaamsha matamanio. Vinginevyo si makruhu, lakini ni bora kuacha iwapo hapana haja ya lazima kufanya hivyo.

 


(vi)Kupiga Mswaki

 


Si vibaya kupiga mswaki wakati mtu amefunga kwani Mtume (s.a.w) alikuwa akipiga mswaki wakati amefunga kama tunavyofahamishwa katika Hadith zifuatazo:
Amr bin Rabiyah (r.a) ameeleza: Nilimuona mtume (s.a.w) Mara nyingi nisizoweza kuhesabu akipiga msw aki akiwa amefunga.(Tirmidh na Abu Da ud).

 

Amesimulia Abu Hurairah(r.a) kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Si kwa kuw a ninahofia kuw a litakuw a jam bo zito kw a umm ati w angu, ningekuw a nimeshawaamrisha kutumia mswaki (kupiga mswaki) kila wakitawadha. (Bukh ari).

 


Hadith hii haikubagua mtu aliyefunga na asiyefunga. Bali tunapata fundisho kuwa kupiga mswaki ni kitendo kilichosisitizwa sana.
Bibi Aysha (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Mswaki hutakasa mdomo na ni njia ya kutakia Radhi za Allah (s.w). ” (Bukhari).

 


(vii)Kusukutua na kupandisha Maji Puani

 


Wakati mtu anatawadha anaruhusiwa kusukutua na kupandisha maji puani lakini asifanye sana mpaka maji yakaingia ndani kwani hilo amelikataza Mtume (s.a.w) katika Hadith iliyopokelewa na Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na Nasai.

 


(viii)Kupaka Wanja na Dawa ya Machoni

 


Kupaka wanja kunaruhusiwa kwa mtu aliyefunga Mtume (s.a.w) ameruhusu hilo katika Hadith ifuatayo:
Anas(r.a) ameeleza kuwa mtu mmoja amekuja kwa Mtume (s.a.w) na akasema: “Ninaumwa macho. Ninaweza kupaka wanja wakati nimefunga? `Ndio’ Alijibu Mtume (s.a.w).”

 


Pia dawa ya macho iwe ya mafuta au ya maji inaruhusiwa kutumiwa wakati mtu amefunga kwa sababu hapana tundu la kuungana moja kwa moja na koo kama yalivyo matundu ya pua na masikio.

 


(ix)Kumeza usichoweza kujizuia nacho
Ukimeza vitu usivyoweza kujizuia kama vile mate, kohozi, vumbi la njiani, vumbi la unga, kumeza mdudu aliyeingia kwa ghafla hadi kooni, n.k. utakuwa hujafungua.

 


(x)Kujipaka mafuta au manukato
Kujipaka mafuta au manukato mwilini au nguoni, kunusa manukato, kujifukiza udi na ubani, n.k. hakuharibu funga.

 


(xi)Kuumika au kutoa Damu
Kuumika hakufunguzi kwani Mtume (s.a.w) amefanya hivyo wakati akiwa amefunga kama tunavyofahamishwa katika Hadith ifuatayo:
Amehadithia Ibn Abbas (r.a) kwamba Mtume (s.a.w) aliumikwa akiwa katika “Ihram” na pia akiwa amefunga. (Bukhari).

 

Hata hivyo, kama kuumika huko kutamfanya mtu awe dhaifu, basi itakuwa ni makruhu. Hali kadhalika mtu anaruhusiwa kutoa damu kwa ajili ya kuwasaidia wagonjwa (blood transfusion), akiwa amefunga.

 


(xii) Kupiga Sindano
Kupiga sindano ya dawa, iwe ya mshipa au chini ya ngozi, haifunguzi.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Lengo la kusimamisha swala kwa mwanadamu
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la kusimamisha swala. Soma Zaidi...

image Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja
Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja. Soma Zaidi...

image Faida na umuhimu wa nfoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...

image Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume. Soma Zaidi...

image Maandalizi kwa ajili ya kifo
Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo. Soma Zaidi...

image Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake. Soma Zaidi...

image Taratibu za kutaliki katika uislamu.
Hapa utajifunza taratibu zinazofuatwa wakati wa kukusudia kumuacha mke. Pia utajifunza sababu za kiwepo kwa eda baada ya kuachwa mwanamke. Soma Zaidi...

image Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda
Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuswali swala ya kuoatwa kwa juwa ama swala ya kuoatwa kwa mwezi.
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya kupatwa yaani kupatwa kwa juwa na kupatwa kwa mwezi swalat kusuf na swalat khusuf Soma Zaidi...

image Ni nini maana ya Talaka katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha. Soma Zaidi...