Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake

Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali.

7.Swalatudh-Dhuhaa

Swala ya Dhuhaa ni sunnah inayoswaliwa kati ya kipindi cha baada ya jua kupanda juu kiasi cha mita tatu hivi na kabla ya jua kufikia katikati. Lakini ni bora kuswali katikati ya kipindi hicho.

 


Swala hii inaswaliwa kwa rakaa mbili mbili hadi zitimie nane, lakini kwa uchache unaweza kuswali rakaa mbili tu na pia unaweza kuswali zaidi ya rakaa nane.


Umuhimu wa swala ya Dhuhaa uko wazi. Kipindi kati ya swala ya Alfajir na Dhuhuri ni kirefu sana kiasi kwamba mja anaweza kusahau kumkumbuka na kumtaja Allah (s.w). Kama tunavyofahamu kumkumbuka Allah (s.w) kila wakati ndio ngao pekee ya kumzuia mja na mambo maovu na machafu. Hivyo Swalatudh-Dhuhaa kwa mtu mwenye wasaa katika kipindi hicho cha harakati nyingi za kutafuta riziki, itampa msukumo mpya wa kumkumbuka na kumuabudu Allah ipasavyo.

 


Kutokana na hadith iliyopokelewa na Abu Daud na Ahmad, Buraidah (r.a) amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Katika mwili wa binaadam kuna viungo (joints) 360 na binaadam ni lazima akitolee sadaka kila kiungo kimoja”. Watu wakauliza:“Nani awezaye kufanya hivyo ewe Mjumbe wa Allah?”Mtume akawajibu: “Mtu anaweza kufanya hivyo kwa kuondosha kitu chenye madhara njiani. Na iwapo hatoweza, kufanya hivyo basi rakaa mbili za Dhuhaa zitamtosheleza ”.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3839

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

msimamo wa uislamu juu ya kupanga uzazi na uzazi wa mpango

Msimamo wa Uislamu juu ya kudhibiti uzaziKama tulivyoona, msukumo wa kampeni ya kudhibiti kizazi, umetokana na mfumo mbaya wa kijamii na kiuchumi ulioundwa na wanadamu kutokana na matashi yao ya ubinafsi.

Soma Zaidi...
NI LIPI HASA LENGO LA KUFARADHISHWA SWALA ZA FARADHI NA KUWEPO KWA SWALA ZA SUNNAH (SUNA)

Lengo la Kusimamisha SwalaBila shaka swala imepewa umuhimu mkubwa kiasi cha kufanywa nguzo kubwa ya Uislamu kutokana na lengo lake.

Soma Zaidi...
Dhana ya mirathi na kurithi katika zama za ujahiliya

Mirathi katika jamii za kijahiliKatika jamii nyingi za kijahili kama vile jamii ya Waarabu kabla ya Mtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu

Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu.

Soma Zaidi...
Swala ya idil fitir na idil haji nanjinsi ya kuziswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya idil haji na swala ya idil fitir

Soma Zaidi...
Taratibi za malezi ya watoto wadogo baada ya talaka katika uislamu

Endapo mke na mume wameachana na hali ya kuwa mke ana watoto wachanga. Je uislamu unasemaje kuhusu taratibu za malezi?

Soma Zaidi...