Ni viumbe watiifu wasiomuasi Allah(SW)
Malaika ni viumbe watiifu kwa Allah(SW). Wakipewa amri ya kumuadhibu mtu muovu, hawagomi wala kumuonea huruma mtu huyo.Enyi mlioamini! Ziokoeni nafsi zenu na nafsi za watu wenu na moto ambao kuni zake ni watu na mawe. Juu yake kuna Malaika w akali wenye nguvu.Haw amuasi Allah(SW) katika yale anayowaamuru, na wanatekeleza vile walivyoamrishwa.(66:6)
Wana elimu ya kutosha kutekeleza majukumu yao
Malaika wana elimu inayowawezesha kutekeleza majukumu yao bila ya kubabaisha. Elimu waliyopewa malaika ni sehemu ndogo sana katika ujuzi wa Allah(SW). Na wenyewe walikiri mbele ya Allah(SW)Wakasema: Utukufu ni wako! Hatuna elimu ila ile uliyotufundisha, bila shaka wewe ndiye mjuzi na mwenye hekima(2:32)
Malaika hawana jinsia ya kike wala ya kiume. Qurβan inawakosoa watu wanaodhani kuwa malaika ni wanawake. In a h oji:
Na wamewafanya malaika ambao ni waja wa Mwingi wa Rehma kuwa ni wanawake. Je wameshuhudia kuumbwa kwao(43:19).
Ni viumbe wenye mbawa
βSifa zote njema ni za Allah, Muumba wa mbingu na ardhi. Aliyewafanya malaika kuwa wajumbe wenye mbawa mbili-mbili, na tatu tatu, na nne nne. Huzid is ha katika kuumba apendavyo. Bila shaka Allah ni mwenye uweza juu ya kila kituβ. (35:1)
Huweza kujimithilisha umbile la mwanadamu
Malaika huweza kujimithilisha kuwa kama wanadamu. Hufanya hivyo pale wanapotumwa na Allah(SW)kuleta ujumbe kwa watu maalumu. Kwa mfano, Bibi Maryam, mama yake nabii Isa(a.s), alijiwa na malaika katika umbo mithili ya mwanaume.Na mtaje katika kitabu, Maryam, alipojitenga na watu wake katika upande wa mashariki.
Tukampelekea Muhuisha sharia Yetu(Jibril) akajimithilisha kwake kwa sura ya binaadamu aliye kamilifu. (19:16-1 7)
Lengo la kuumbwa malaika
Lengo la kuumbwa malaika ni kumtumikia Allah(SW). Katika kutekeleza lengo la kuumbwa kwao, malaika hawana hiyari katika kutekeleza amri za Allah(SW), hufanya mambo yote vile anavyotaka Allah(SW).
..Hawamuasi Allah(SW) katika yale anayowaamuru, na w anatekeleza vile w alivyoamrishw a.(66:6)
Umeionaje Makala hii.. ?
Ushahidi wa kuthibitisha kutendeka kwa kosa la uzinifu unapatikana kwa namna tatu zifuatzo: (i)Kushuhudia tendo hilo likifanyika kwa wakati mmoja watu wanne Mukalafu (Walio baleghe na wenye akili timamu), wakiwa ni Waislamu waadilifu.
Soma Zaidi...Ukizingatia maana halisi ya dini, kuwa dini ni utaratibu wa maisha, utadhihirikiwa kuwa umbile la mwanaadamu ni la kidini.
Soma Zaidi...Maana ya dini kwa mujibu wa makafiri ina utofauti mkubwa na vile ambavyo uislamu unaamini kuhusu dini.
Soma Zaidi...Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)
Soma Zaidi...Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s.
Soma Zaidi...Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.
Soma Zaidi...