MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu.
MAGONJWA YA INI NA DALILIZAKE, NA KUKABILIANA NAYO
Ini ni katika viungo vikuu katika mwili wa binadamu. Ni katika viungo vichache ambavyo vikikatwa vinaweza kujirudisha, yaani kukuwa. Ini ni katika viungo vinavyo shambuliwa na vimelea vya maradhi mbalimbali pamoja na sumu za vyakula. Ini mwilini husaidia katika mmengenyo wa chakula, na kuondoa sumu za vyakula mwilini. Endapo ini litadhurika kwa namna yeyote ile afya ya mtu katu haitakuwa salama, na athari zake endapo zitachelewa kupatiwa matibabu hupelekea kifo.
Katika makala hii tutakwenda kuyaona baadhi ya maradhi ya ini, dalili zake na njia za kukabiliana nayo. Kuwa nasi kwenye makala hii, na wasambazie wengine uwapendao, kulinda afya zao. Makala kama hizi na nyinginezo utazipata kwenye tovuti yetu www.bongoclass.com
Maradhi yanayoshambulia figo yapo mengi sana, na yapo ambayo hurithiwa na mengine hayarithiwi. Na yapo ambayo huambukizwa na mengine hayaambuizi. Ifuatayo ni orodha ya maradhi ya ini:-
SABABU ZA KUTOKEA KWA MARADHI YA INI:
Ili tuone sababu hizo kwanaz atuone aina za maradhi ya ini. Na himo kwenye aina hizo ndipo utakapojua ni sababu ipi imesababisha maradhi hayao:-
A. Maradhi ya ini yanayosababishwa na maambukizi
Maradhi ya ini yanayosababishwa na maambukizi yanajulikana kama homa ya heatitis. Homa hii husababishwa na virusi wanaotambulika kama hepatisis viruses. Miongoni mwa virusi hao ni:-
1.hepatitis A
2.Hepatitis B
3.Hepatitis C
B. Maradhi ya ini yanayosababishwa na mashambulizi ya mfumo wa kinga mwilini, kushambulia seli za ini. Kitaalamu hutambulika kama immune system Abnomality au Autoimune. Maradhi ya ini yanayosababishwa kwa njia hii ni:-
1.Autoimmune hepatitis
2.Primary biliary cirhosis
3.Primary sclerosing cholangitis
C. Maradhi ya ini yanayosababishwa kwa kurithi
Unaweza kurithi maradhi ya ini kutoka kwa wazazi wako ,ima mmoja wapo ama kwa wote. Maradhi ya ini yanayosababishwa na kurithi ni:-
1.Homochromatosis
2.Hyperoxaluria na oxalosis
3.Wilson’s diseases
D. Maradhi ya ini yanayosababishwa na saratani (cancer)
1.saratani ya ini
2.Saratani ya nyongo
3.Kuvimba vya ini
DALILI ZA MARADHI YA INI
Katika maradhi yote tulioyataja hapo juu, ynashirikiana kwa pamoja katika dalili zifuatazo:
1.macho na ngozi kuwa na rangi ya njano.
2.Maumivu yasiyo ya kawaida yanayoendana na kuvimba mwili
3.Kuvumba kwenye miguu na vifundo vya miguu (ankles)
4.Kuuma kwa ngozi
5.Mkojo kuwa na rangi nyeusi ama giza
6.Kupata choo chenye rangi kupauka, ama kuwa na damu
7.Uchovu mkali sana na usio wa kawaida
8.Kichefuchefu na kutapika
9.Kukosa hamu ya kula
10.Ngozi kuchubuka kwa urahisi.
MAMBO YANAYOHATARISHA AFYA YA INI NA KULETA MARADHI YA INI
1.unywaji wa pombe kupitiliza
2.Kujidunga sindano kwa kushirikiana
3.Uwekaji wa tatuu
4.Kuongezewa damu
5.Muingiliano wa majimajin ya mwili na damu
6.Kupanya ngono zembe
7.Kisukari
8.Kuzidi kwa uzito
VIPI UTAWEZA KUZUIA MARADHI YA INI
1.Punguza unywaji wa pombe
2.Jiepushe na tabia hatarishi kama kujidunga masindano, kushirikiana vitu vya ncha kali, ngono zembe n.k
3.Pata chanjo ya baadhi ya maradhi ya ini kama hepatitis
4.Ilinde ngozi yako
5.Hakikisha huna uzito wa kuzidi
6.Fanya mazoezi
7.Unapopuliza dawa za wadudu vaa kitambaa puani (mask)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuwaka moto mara kwa mara mdomoni bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea ya mdomo wako wot
Soma Zaidi...Madhara ya ugonjwa wa akili yanaweza kuwa ya muda au ya kudumu. Unaweza pia kuwa na zaidi ya ugonjwa mmoja wa afya ya akili kwa wakati mmoja. Kwa mfano, unaweza kuwa na ulegevu na ugonjwa wa matumizi ya madawa ya kulevya.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Soma Zaidi...Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU/ UKIMWI
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia ambazo zinaweza kutumika Ili kuweza kupunguza kuwepo kwa magonjwa ya zinaa
Soma Zaidi...Manung'uniko ya moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako.
Soma Zaidi...Watu wengi wamekuwa na mawazo kuwa ili nipate ukimwi ninatakiwa nishiriki ngono zembe na aliyeathirika mara ngapi? Majibu ya swali hili ni mafupi tu, ni kuwa unaweza kuathirika kwa ngono zembe ya siku moja tu ndani ya dakika chache. Lakini jambo la kuzing
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Donda Koo ni ugonjwa unaosababishwa na vimelea viitwavyo kwa kitaalamu corynebacterium diphtheria, ugonjwa huu ushambulia Koo na unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa, mate na
Soma Zaidi...Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuungua kinywani kwa mara kwa mara (kwa muda mrefu) bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea
Soma Zaidi...