image

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.w)unaolandana na Elimu sahihi.

(ii) Tujiepushe na tabia ya kiiblis ya kumtukuza au kumdharau mtu kutokana na nasaba, rangi, sura, hali yake kiuchumi, n.k.

(iii) Tujiepushe na tabia ya Kiiblis ya kuwa na chuki binafsi dhidi ya watu wasio na hatia yeyote.

(iv) Tujiepushe na tabia ya Kiiblis ya kibri na majivuno.

(v) Tuwe na msimamo katika kutekeleza amri za Allah(s.w) na Mtume wake na tusiwe tayari kuyumbishwa na hadaa za shaitwani.

(vi) Tunapofikwa na tashwishi za kishetani tujikinge kwa Allah(s.w).



“Na kama shetani akikushawishi kwa tashwishi (zake), wewe jikinge kwa Mwenyezi Mungu (kwa kusema: A’uudhubillah Minash-shaytwanir-Rajiim). Yeye ni mwenye kusikia mwenye kujua.” (41:36)

Au ujikinge kwa kusema:




Sema: najikinga kwa Bwana mlezi wa watu. Mfalme wa watu. Muabudiwa wa watu. Na shari ya mwenye kutia wasiwasi mwenye kurejea nyuma. Atiaye wasiwasi nyoyoni mwa watu. Ambaye ni katika majini na watu. (114:1-6)

Au kuleta Dua ifuatayo:




“...... Mola wangu! Najikinga kwako uniepushe na wasiwasi wa mashetani. Na najikinga kwako, Mola wangu, ili wasinihudhurie”. (23:97-98)


(vii) Muda wote Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari kwani kiasili (tangu mwanzo wake) Uislamu ni dini yenye maadui miongoni mwa mashetani wa kijini na watu.



................

“Na namna hii tumemfanyia kila Nabii maadui, (nao ni) mashetani katika watu na majini. Baadhi yao wanawafunulia wenziwao maneno ya kupamba pamba ili kuwadanganya…..........” (6:112)


(viii)Mwanaadamu tangu mwanzo wa kuumbwa kwake amekusudiwa kuwa Khalifa katika ardhi na nyenzo kuu ya kumuwezesha kuwa Khalifa ni elimu ya mazingira na ya mwongozo.

(ix) Tujiepushe na kuwahusudu watu juu ya meema walizotunukiwa na Allah(s.w) bali tumuelekeeAllah(s.w) kwa unyenyekevu na
k umuomba atuneemeshe kama wale aliowaneemesha.

Wala msitamani vile ambvyo MwenyeziMungu amewafadhilisha badhi yenu (kwa vitu hivyo) kuliko wengine. wanaume wanayo sehemu (kamili) ya vile walivyovichuma; na wanawake nao wanayo sehemu(kamili) ya vile walivyovichuma na mwombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake. Hakika Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu.(4:32)

(x) Allah(s.w) huwaongoza na kupokea maombi ya wale wajitakasao:
........

“...... Hakika Mwenyezi Mungu huwapenda wanaotubu na kuwapenda wanaojitakasa” (2:222)

(xi) Muislamu muumini anatakiwa ajihidi kuondosha ubaya au alipize ubaya aliofanyiwa kwa wema,yaani kumsamehe aliyemkosea kumpa aliyemnyima na kumchangamkia aliye mkasirikia. Tunahimizwa katika Qur’an:



“Mambo mazuri na mabaya hayawi sawa. Ondosha (ubaya uliofanyiwa kwa wema), tahamaki yule ambaye baina yako na baina yake kuna uadui atakuwa kama ni jamaa (yako) mwenye kukufia uchungu. Lakini (jambo hili) hawatapewa ila wale wanaosubiri wala hawatapewa ila wenye hadhi kubwa (mbele ya Mwenyezi Mungu)”(41:34-35)

(xii) Tunapoteleza na kumkosea Allah(s.w),tumuelekee kwa unyenyekevu kwa kuleta toba ya kweli kama alivyofanya Adam(a.s) na mkewe.

(xiii) Kumkosea Allah(s.w) kwa kibri kama alivyofanya Iblis ni jambo baya mno la hatari kwani humpelekea mtu kupigwa muhuri moyoni mwake kiasi cha kumfanya asione haja yoyote ya kuleta toba. Tunakumbushwa hili katika Qur’an.



“Hakika wale waliokufuru (kwa ukaidi tu na inadi) ni sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye hawataamini. Kama kwamba Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya ya nyoyo zao na juu ya masikio yao; na juu ya macho yao pana kifuniko; basi watakuwa na adhabu kubwa.”(2:6-7)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 710


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

HISTORIA YA NABII ISMAIL
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)
(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s. Soma Zaidi...

Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ayyuub(a.s)
Kutokana na kisha hiki cha Nabii Ayyuub(a. Soma Zaidi...

Adam na Hawah Kushushwa Ardhini
Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake. Soma Zaidi...

Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...

Historia ya Dhulqarnain
Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”. Soma Zaidi...

Historia ya Dhana ya Kudhibiti Uzazi
Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Lut (a.s)
(i) Tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuondoa maovu katika jamii kwa mikono yetu na ikiwa hatuwezi tuyakemee kama alivyofanya Nabii Lut(a. Soma Zaidi...

Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake
Nabii Lut(a. Soma Zaidi...