Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah

Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

-  Mtume (s.a.w) alitumia kila aina ya fursa iliyopatikana katika kuufikisha 

    ujumbe Uislamu kwa watu wengine.

 

-  Mtume (s.a.w) alifikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu na makabila mbali 

    mbali kwa siri na dhahiri kutokana na uadui wa Maquraish dhidi yake.

 

-  Mtume (s.a.w) alitumia mikataba kwa kuandaa ummah wa kiislamu kutoka 

   sehemu mbali mbali hasa mji wa Madinah (Yathrib) kama ifuatavyo;

   -  Hii ilikuwa ni baina ya Mtume (s.a.w) na watu wanaotoka nje ya mji wa   

      Makkah hasa waliokuja kuhiji msimu wa Hija.

 

   -  Mtume (s.a.w) alikutana na kikosi cha kwanza kabisa cha watu sita (6) 

      kutoka Madinah (Yathrib) wa kabila la Khazraj, baada ya kuwafikishia 

      ujumbe wa Uislamu, walisilimu na wakaahidi kuufikisha kwao Madina.

 

  -  Mwaka uliofuata, 621 A.D, kikundi kingine cha waislamu 12 (2 Aus na 

     10 Khazraj) walikutana na Mtume (s.a.w) kwa siri eneo la ‘Jaratul 

     ‘Aqabah’ na kuweka mkataba wa kwanza wa ‘Aqaba na kukubaliana 

      yafuatatayo;

  1. Hawataabudu chochote isipokuwa Allah (s.w) pekee.
  2. Hawataiba wala hawatapokonya misafara ya biashara njiani.
  3. Hawatazini.
  4. Hawatawaua watoto wao tena.
  5. Hawatasema uongo wala hawatawasingizia wengine uovu.
  6. Hawatamuasi Mtume kwa kila atakalowaamrisha na watakuwa waaminifu kwake kwa hali yeyote iwayo.

 

                -  Mtume (s.a.w) aliwapa mwalimu wa kuwafundisha Uislamu, ‘Mus’ab bin 

                             Umair.

                -  Mwaka uliofuata, 622 A.D.walimjia Mtume (s.a.w) waislamu 75   

    (wanawake 2) wakiongozwa na mwalimu wao, ‘Mus’ab na kufunga   

    Mkataba wa pili wa ‘Aqabah sehemu ile ile kwa kukubaliana kuwa;

 

               

                -  Mtume (s.a.w) aliwachagulia viongozi 12 (9 Khazraj na 3 Aus) na watu 

                             watakaokuwa chini ya kila kiongozi, na wanaume wote walimpa Mtume 

                            (s.a.w) mkono wa bai’at kwa maana ya utii wao kwake.

 

                -  Baada ya kikundi hicho kurejea na kufika Madinah salama, ndipo Mtume 

                            (s.a.w) aliwatangazia waislamu wote wa Makkah kuhamia Madinah.

 

                -   Na takriban baada ya miezi miwili hivi, Waislamu wote wenye uwezo wa   

                            kuhama walishahamia Yathrib (Madinah) kwenda kujiimarisha zaidi.

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1270

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Ni jitihada gan alizo zifanya sayyidna othman katika kuihifadh qur an ?
Ni jitihada gan alizo zifanya sayyidna othman katika kuihifadh qur an ?

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Jitihada alizozifanya Khalifa wa Tatu katika kuilinda Quran

Soma Zaidi...
tarekh 09
tarekh 09

KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana.

Soma Zaidi...
Mtume amezaliwa mwaka gani?
Mtume amezaliwa mwaka gani?

Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake.

Soma Zaidi...