Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah


image


Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)


  • Mtume (s.a.w) alivyoandaa Ummah wa Kiislamu Makkah.

-  Mtume (s.a.w) alitumia kila aina ya fursa iliyopatikana katika kuufikisha 

    ujumbe Uislamu kwa watu wengine.

 

-  Mtume (s.a.w) alifikisha ujumbe wa Uislamu kwa watu na makabila mbali 

    mbali kwa siri na dhahiri kutokana na uadui wa Maquraish dhidi yake.

 

-  Mtume (s.a.w) alitumia mikataba kwa kuandaa ummah wa kiislamu kutoka 

   sehemu mbali mbali hasa mji wa Madinah (Yathrib) kama ifuatavyo;

  •   Mikataba ya ‘Aqabah.

   -  Hii ilikuwa ni baina ya Mtume (s.a.w) na watu wanaotoka nje ya mji wa   

      Makkah hasa waliokuja kuhiji msimu wa Hija.

 

   -  Mtume (s.a.w) alikutana na kikosi cha kwanza kabisa cha watu sita (6) 

      kutoka Madinah (Yathrib) wa kabila la Khazraj, baada ya kuwafikishia 

      ujumbe wa Uislamu, walisilimu na wakaahidi kuufikisha kwao Madina.

 

  -  Mwaka uliofuata, 621 A.D, kikundi kingine cha waislamu 12 (2 Aus na 

     10 Khazraj) walikutana na Mtume (s.a.w) kwa siri eneo la ‘Jaratul 

     ‘Aqabah’ na kuweka mkataba wa kwanza wa ‘Aqaba na kukubaliana 

      yafuatatayo;

  1. Hawataabudu chochote isipokuwa Allah (s.w) pekee.
  2. Hawataiba wala hawatapokonya misafara ya biashara njiani.
  3. Hawatazini.
  4. Hawatawaua watoto wao tena.
  5. Hawatasema uongo wala hawatawasingizia wengine uovu.
  6. Hawatamuasi Mtume kwa kila atakalowaamrisha na watakuwa waaminifu kwake kwa hali yeyote iwayo.

 

                -  Mtume (s.a.w) aliwapa mwalimu wa kuwafundisha Uislamu, ‘Mus’ab bin 

                             Umair.

                -  Mwaka uliofuata, 622 A.D.walimjia Mtume (s.a.w) waislamu 75   

    (wanawake 2) wakiongozwa na mwalimu wao, ‘Mus’ab na kufunga   

    Mkataba wa pili wa ‘Aqabah sehemu ile ile kwa kukubaliana kuwa;

 

  • Mtume na Waislamu wote wa Makka wahamie Madinah (Yathrib) na wao watawapokea na kuwahifadhi dhidi ya maadui wao.

               

                -  Mtume (s.a.w) aliwachagulia viongozi 12 (9 Khazraj na 3 Aus) na watu 

                             watakaokuwa chini ya kila kiongozi, na wanaume wote walimpa Mtume 

                            (s.a.w) mkono wa bai’at kwa maana ya utii wao kwake.

 

                -  Baada ya kikundi hicho kurejea na kufika Madinah salama, ndipo Mtume 

                            (s.a.w) aliwatangazia waislamu wote wa Makkah kuhamia Madinah.

 

                -   Na takriban baada ya miezi miwili hivi, Waislamu wote wenye uwezo wa   

                            kuhama walishahamia Yathrib (Madinah) kwenda kujiimarisha zaidi.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Maswali juu ya Nguzo za uislamu
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kusimamisha swala za faradh katika nyakati za dharura.
Kipengele hichi tutajifunza namna ya kusimamisha swala ukiwa safarini na vitani na nguzo zake. Soma Zaidi...

image Mikataba ya aqabah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala. Soma Zaidi...

image Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya zakat
Nguzo za uislamu,kutoa zakat na sadaqat (EDK form 2; dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Faida za funga
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kuamini vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)
Nguzo za Imani (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kutoa zakat
Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu
Nguzo za uislamu,umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...