Hili ni somo la nne katika mafunzo ya html basic level. Hapa tutakwenda kuona jinsi ya kuzifanyia kazi tag ambazo umejifunza katika somo lililotangulia.
HTML SOMO LA NNE
Karibu tena lwenye mafunzo haya ya HTML lugha ya kompyuta inayotumika katika kutengenezea website, blog na web application. Html hutumika na mchanganyiko wa lugha nyingine za kompyuta kutengeneza software na system. Hata hivyo unaweza kutumia html peke yake kutengeneza website (tovuti) na ikawa live watu wakaweza kuitembelea.
Je na kama na wewe ni mmoja kati ya wenye ndoto za kuweza kufanya haya, karibu tena kwenye somo hili. Katika somo la kwanza hadi la tatu tuliona namna ambavyo HTML inavyofanya kazi, pia tuliona mpangilio wa faili lake na tukaona tag na element. Katika somo la tatu tulijifunza code 25 muhimu zinazotumuka katika uandidhi. Unaweza kupata somo la kwanza la pili na tatu kwenye linki hizo hapo chini:-
Katika somo hili la nne tutaona jinsi ambavyo tag 25 tulizozitaja kwenye somo la tatu zinavyoweza ktumika na kuandikia makala katika ukurasa wa mtandao. Kama utakuwa unatumia kompyuta funguwa note pad kisha fatilia somo hili, tumia notepad kuandikia code kama somo litakavyoonyesha. Kwa wale wanaotumia simu kama mimi, utaratibu umetangulia katika somo la kwanza, unatakiwa utumie App inayojulikana kama TrebEdit ipo playstore, linki utaipata kwenye somo la kwanza.
FILE EXTENTION KATIKA FAILI LA HTML
Tunapozungumzia file extension huwenda likaonekana kama neno gumu, ila kwa ufupi nitolee mifano. Unapotaka kusevu faili katika microsoft office unaweza kusave as document (.doc), extensive document (.docx) portable document file (.pdf). pia katika media kuna (.mp3, .mp4) kwenye web site kuna (.com, .net, .io, .co, .ac). hivyo extension ndio ambayo huiambia kompyuta aina ya faili. Sasa unapoandika faili lako la code za HTML, wakati wa ku save lazima uweke (.html) mfano katika somo la kwanza tulitumia faili tuliloliita “index.html” usisahau kuweka doti.
Sasa funguwa App yako ya Treb editi kisha menu, kisha workplace, kisha click project yako kama tulivyofanya kwenye somo la kwanza na pili. Kisha new file, weka jina mfano “tag.html” kisha save. Click hilo faili, kisha bofya HTML snippet chini, hapo ukurasa mpya wa code utatokea. Kwa watumiaji wa kompyuta kweka code hizi kwenye notepad yako:
<!DOCTYPE html> <html lang="en"> <head> <meta charset="utf-8"> <title>Tag Muhimu</title> </head> <body> </body> </html>
Kisa saveas all files kija weka tag.html
Sasa hadi kufikia hapa tupo tayari kuanza somo. Somo
Katika tag zote 25 tulizoziona katika somo la tatu, baadhi yake tutakuja kuziona tena kwenye masomo yajayo kutokana yanahitaji ufafanuzi zaidi. Kwa mgano tag hii <img na <a> hizi tutakuja kuziona zaidi katika somo lijalo. Sasa kama ulishafunguwa TrebEdit yako ama notepad, sasa kopi code hizo hapo chini kisha paste kwenye faili lako ulilolisave kwa jina la tag.html. Kisha previes, kwa kubofya kitufe cha kuplay au click file kwenye komputer litafunguka kama website.
Code zenyewe ni hizi:-
<!DOCTYPE html> <html lang="en"> <head> <meta charset="utf-8"> <title>Tag Muhimu</title> </head> <body> <h1>Heading 1</h1> <h2>heading 2</h2> <h3>heading 3</h3> <h4>heading 4</h4> <h5>heading 5</h5> <h6>heading6</h6> <p>hii ni paragraph</p> <b>bold</b> <u>underlined</u> <hr> msitari<hr> <i>italic</i> <br> 6<sup>2</sup><br> H<sub>2</sub>O <br> <code>code type</code> <br> <tt>type writer</tt> <br> <small>small text</small><br> <em>emphasizing</em> <br> <strong>strong text</strong> <br> <mark>marked text</mark> <br> <s>striked text</s> <br> <q>quoted text</q> <br> line<br>break<br>break<br> wacha nafasi nafasi <br> <a href="https://bongoclass.com">link</a><br> <button>Tabani</button><br> <pre> maandishi yatakuwa kama unavyoyaonahapa kwenye cde mfano: kama unapoandika mashairi unataka iwe kama ilivyo bila kuharibu mpangilio wa vina </pre> <br> <form> <label>Jina kamili</label> <input type="text" placeholder="enter your name"> </form> <br> <img src="" alt="picture"> <br> <div>this is block text</div> <span>this is inline block text</span> </body> </html>
Katika posti ijayo tutakuja kuona namna ya kuweka staili kwenye faili la html, kama kuweka rangi, kupangilia text, kuweka link na kupangilia muonekano wa text. Endelea kufanyia mazoezi tag hizo hapo juu, ili iwe rahisi kuendelea na somo lijalo. Usisite kuuliza swali ambapo hapaposawa.
Mafunzo haya yamekujia kwa hisani ya:
Bongoclass.com
Web: www.bongoclass.com
Email: mafunzo@bongoclass.com
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
hili ni somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2 html full course for beginners. Katika somo hili tutaangalia utangulizi juu ya HTML na pia utajifunza faida za HTML.
Soma Zaidi...Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho.
Soma Zaidi...hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php.
Soma Zaidi...Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database
Soma Zaidi...Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1.
Soma Zaidi...Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.
Soma Zaidi...huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.
Soma Zaidi...Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development
Soma Zaidi...Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)
Soma Zaidi...