hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.
SOMO LA TATU
NAMNA YA KUWEKA VARIABLE
Variable ni moja katika kitu mihimu kwenye faili la php. Huwezi kuunganisha tovuti yako kwenye database, huwezi kuzifikia data kwenye database bila kutumia variable. Huwezi kuweka function bilakutumia variable. Kwa ufupi php inazungumza kwa kutumia variable.
Variable ni nini?
Ni ngumu kutoa maana ya hili neno likafahamika bila maswali, ila niseme tu kwa ufupi variable unaweza kuwema ni chombo cha kuhifadhia data kwenye program. Unaweza kuzikusanya data nyingi zinazofanana kwa kutumia variable moja.
Kwa mfano unaweza kusema neno gari likawa na mgawanyiko kama toyota, benzi, basi na pikap. Sasa badala ya kuyaida majina yao unaweza tu kuweka variable ya gari hala fu compyuta ikadisplay magariyote. Badala ya kuanza tena kutaja, majina ya magari unaweka variable gari yanakuja yote.
Cheki mfano huu:
<?php
$gari = array("basi", "benzi", "toyota","tractor", "isuzu");
echo "tunauza magari aina ya ". $gari[2].",". $gari[1].".";?>
Kwa kutumia variable gari naweza kutaja vina la gari lolote kati ya hayo bila ya kuandika jina lake halisi. Hii inasaidia kusave time.
Kanuni za kuweka variable
Mafano 1
<?php
$chakula = "ugali wa sembe iliyonyeupe na samaki wa bwawani pamoja na kachumbari yenye ndimu nyingi";
echo " napenda kula $chakula";
?>
Kw akutumia mfano huu, baada ya kuyaudia maneno yaliyopo kwenye variable ambayo ni “ugali wa sembe iliyonyeupe na samaki wa bwawani pamoja na kachumbari yenye ndimu nyingi” sasa badala ya kuyaridia rudia nitatumia neno chakula kisha maneno hayo yatatolea. Haijalshi nimeyarudia mara ngapi.
Mfano 2
<?php
$a = "kaka";
$b = "mama";
$c = "baba";
$d = "shamba";
echo "$a, $b, na $c wamekenda $d kulima mihogo";
?>
Hapa utaona sentensi hii inasomeka kaka, dada na baba wamekwenda shamba kulima mihogo. Kwa kutumia variable hakuna haja ya kuandika tena kaka, dada na baba.
Unaweza kutumia variable kwenye elementi za HTML na kuleta matokeo kulingana na element ya HTML iliyotumika na style ambazo zimetumika. Angalia mfano namba 3 hapo chini:-
Mfano 3
<?php
$a = "kaka";
$b = "mama";
echo "
<h1><b>hiini hadithi ya $a na $b </b><h1>";
?>
Katika sentenzi hii hii hadithi ya kaka na baba, tag ya HTML <h1> na <b> zitatumika kuifanya sentensi iwe heading 1 na kuwa bolded.
Unaweza pia kutumia variable kufanyia hesabu, angalia mfano wa nne hapo chini
Mfano 4
<?php
$e = "5";
$f = "7";
$g = "5";
echo $e + $f;
echo "<br>";
echo $f * $g;
?>
Hapa utapata jibu la hesabu ya kwanza
5 + 7 ambalo ni 12
Na hesabu ya pili ambayo ni
7 * 5 ambalo ni 35
Kwa ufupi hivi ndivyo variable zinavyoweza kuhifadhi taarifa katika gaili la php. Ttajifunzamengi zaidi kuhusu variable katika masomo yanayokuja.
LINE BREAK KWENYE PHP
Katika html tulijifunza kuwa tag ya <br> ndio hutumika kukata msitari. Katika php endapo utaitumia tag hii inaweza kukupa error. Hivyo ili uweze kuitumia unatakiwa uiweke ndani ya echo ama print. Angalia mfano namba tano hapo chini
Mfano 5
<?php
echo "hi my budy are you drinking?";
echo "<br><br>";
echo "welcome at bongoclass";
?>
Hapo kama <br> itakuwa nje ya echo faili halitaweza kufunguka. Katika masomo yanayofata tujifunzapia namna ya kuongeza space zaidi ya moja kwenye php.
Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.
Soma Zaidi...Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL na hili ni somo la pili. Hapa tutakwenda kuona kwa ufupi ni nini DATABASE
Soma Zaidi...hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza.
Soma Zaidi...hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php.
Soma Zaidi...Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.
Soma Zaidi...huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database.
Soma Zaidi...haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.
Soma Zaidi...Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database
Soma Zaidi...