Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)

hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.

SOMO LA TATU

NAMNA YA KUWEKA VARIABLE

Variable ni moja katika kitu mihimu kwenye faili la php. Huwezi kuunganisha tovuti yako kwenye database, huwezi kuzifikia data kwenye database bila kutumia variable. Huwezi kuweka function bilakutumia variable. Kwa ufupi php inazungumza kwa kutumia variable.

 

Variable ni nini?

Ni ngumu kutoa maana ya hili neno likafahamika bila maswali, ila niseme tu kwa ufupi variable unaweza kuwema ni chombo cha kuhifadhia data kwenye program. Unaweza kuzikusanya data nyingi zinazofanana kwa kutumia variable moja.

 

Kwa mfano unaweza kusema neno gari likawa na mgawanyiko kama toyota, benzi, basi na pikap. Sasa badala ya kuyaida majina yao unaweza tu kuweka variable ya gari hala fu compyuta ikadisplay magariyote. Badala ya kuanza tena kutaja, majina ya magari unaweka variable gari yanakuja yote.

 

Cheki mfano huu:

<?php

$gari = array("basi", "benzi", "toyota","tractor", "isuzu");

echo "tunauza magari aina ya ". $gari[2].",". $gari[1].".";?>

Kwa kutumia variable gari naweza kutaja vina la gari lolote kati ya hayo bila ya kuandika jina lake halisi. Hii inasaidia kusave time.

 

Kanuni za kuweka variable

  1. Kwanz aunatakiwa uanze na alama ya dola ambayo ni $
  2. Kisha utaandika jina la variable usianze na namba
  3. Kisha ruka nafasi kisha weka alama ya =
  4. Kisha weka alama za kunukuu “   ”
  5. Ndani ya alama za kunukuu andiak thamani ya variable yako, yaani unataka variable hiyo iwakilishe nini?
  6. Weka alama ya semi colon ambayo  ni ;
  7. Baada ya hapo ni kuitumia variable yako.

 

Mafano 1

<?php

$chakula = "ugali wa sembe iliyonyeupe na samaki wa bwawani pamoja na kachumbari yenye ndimu nyingi";

echo " napenda kula $chakula";

?>

 

Kw akutumia mfano huu, baada ya kuyaudia maneno yaliyopo kwenye variable ambayo ni “ugali wa sembe iliyonyeupe na samaki wa bwawani pamoja na kachumbari yenye ndimu nyingi” sasa badala ya kuyaridia rudia nitatumia neno chakula kisha maneno hayo yatatolea. Haijalshi nimeyarudia mara ngapi.

 

Mfano 2

<?php

$a = "kaka";

$b = "mama";

$c = "baba";

$d = "shamba";

echo "$a, $b, na $c wamekenda $d kulima mihogo";

?>

Hapa utaona sentensi hii inasomeka kaka, dada na baba wamekwenda shamba kulima mihogo. Kwa kutumia variable hakuna haja ya kuandika tena kaka, dada na baba.

 

Unaweza kutumia variable kwenye elementi za HTML na kuleta matokeo kulingana na element ya HTML iliyotumika na style ambazo zimetumika. Angalia mfano namba 3 hapo chini:-

Mfano 3

<?php

$a = "kaka";

$b = "mama";

echo "

<h1><b>hiini hadithi ya $a na $b </b><h1>";

?>

 

Katika sentenzi hii hii hadithi ya kaka na baba, tag ya HTML <h1> na <b> zitatumika kuifanya sentensi iwe heading 1 na kuwa bolded.

 

Unaweza pia kutumia variable kufanyia hesabu, angalia mfano wa nne hapo chini

Mfano 4

<?php

$e = "5";

$f = "7";

$g = "5";

 

echo $e + $f;

echo "<br>";

echo $f * $g;

 

?>

Hapa utapata jibu la hesabu ya kwanza

5  + 7 ambalo ni 12

Na hesabu ya pili ambayo ni

7 * 5 ambalo ni 35

 

Kwa ufupi hivi ndivyo variable zinavyoweza kuhifadhi taarifa katika gaili la php. Ttajifunzamengi zaidi kuhusu variable katika masomo yanayokuja.

 

 

LINE BREAK KWENYE PHP

Katika html tulijifunza kuwa tag ya <br> ndio hutumika kukata msitari. Katika php endapo utaitumia tag hii inaweza kukupa error. Hivyo ili uweze kuitumia unatakiwa uiweke ndani ya echo ama print. Angalia mfano namba tano hapo chini

 

Mfano 5

<?php

echo "hi my budy are you drinking?";

echo "<br><br>";

echo "welcome at bongoclass";

?>

 

Hapo kama <br> itakuwa nje ya echo faili halitaweza kufunguka. Katika masomo yanayofata tujifunzapia namna ya kuongeza space zaidi ya moja kwenye php.

 

Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email:mafunzo@bongoclass.com

Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1138

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

PHP level 1 somo la kumi (10)

Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la nne (4)

somo hili la 4 katika mafunzo ya PHP level 1 utajifunza aina za data mabazo php inakwenda kuzitumia.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment

Soma Zaidi...
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)

Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tisa (9).

Somo la nane mafunzo ya php, katika somo hili utajifunza kuhusu array na jinsi ya kutengeneza array.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 6 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 6)

Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 8 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Katika somo hili la 8 mafunzo ya html level 8 utajifunza jinsi ya kuhost project ya html na kuwa live, watu wakaipitia na kusoma maudhui yake.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi na mbili (12) final

Mafunzo ya php level 1 somo ka 12 mwisho wa mafunzo. Hapa utaona project ambazo unaweza kufanya kutokana na mafunzo haya.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL database somo la 9

haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE.

Soma Zaidi...