Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7

Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7

Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7.

SOMO LA SABA

Katika somo lililotangaulia tumejifunza namna ya kutengeneza table. Sasa katika somo hili tutajifunza jinsi ya kuedit jina la table, kufuta. Tutafanya haya kwa kutumia MySQL na kwa kutumia SQL command. Kabla hujaanza somo hili tengeneza table nyingine kisha iite text. Table hiyo ndio tunakwenda kuifanyia mazoezi ya kuiedit jina na kuifuta. Fuata maelekezo ya somo lililotangulia kutengeneza table.

 

Jinsi ya kubadili jina la table kwenye MySQL

Tunabadili jina kwa sababu maalumy, huwenda jina la mwanzo ni gumu sana ama haliendani na data ambazo zipo kwenye database. Ama linafanana na table nyingine ambayo unataka kuitengeneza. Ili kufanya hivi yaani kubadili jina fuata hatuwa zifuatazo:-

Tengeneza Table kwa kutumia command hii

CREATE TABLE IF NOT EXISTS test (

    id INT,

    name VARCHAR (255),

    aka VARCHAR (255)

    )

    

  1. Bofya hiyo table itafunguka utaona hizo column ambazo umetengeneza.
  2. Ingia kwenye operations
  3. Kwenda chini hadi ukute palipoandika table options
  4. Chini utaona palipoandikwa Rename table to na mbele yake kuna kabox.
  5. Kwenye kabox hako weka jina unalotaka lisomeke kwenye table yako mfano tutumie jaribio, hivyo futa jina la mwanzo kisha weka jaribio hapo
  6. Bofya GO
  7. Mpaka kufika hapo jina la table yako litakuwa limebadilika kuwa jaribio

 

 

1. Kubadili jina la table kwa kutumia SQL command

Sasa kama huhitaji kutumia MySQL interface kufanya hivyo unaweza kutumia SQL fuata hatuwa zifuatazo:-

 

        1. Funguwa uwanja wa SQL

  1. Kubadili jina tunatumia RENAME TABLE  au ALTER TABLE kisha inafatiwa na jina la mwanzo ambalo ni jaribio kisha unaandika to kisha unaweka jina jipya mfano test. Statement hii itakuwa hivi
  2. RENAME TABLE jaribio to test;
  3. Pia unaweza kutumia hii kubadili jina ALTER TABLE test RENAME to jaribio
  4. Baada ya hapo bofya GO
  5. Kufikia hapo utakuwa umebadili jina la table yako.

 

2. Kubadili jina la column

Chukulia unataka kubadili jina la column lmfano katika katika table hiyo tuliotoka kuirename ina column tatui mabzo ni id, name na aka. Sasa tunataka kubadili name tuweke firstname badala ya kuwa nme. Kufanya hivi kwa kutumia MySQL fuata hatuw zifuatazo:-

 

  1. Bofya hiyo table
  2. Bofya palipoandika structure
  3. Utaona column zote tatu zipo hapo
  4. Kwa upande wa kulia kwa kila column kuna palipoandikwa change. Bofya hapo
  5. Kutakuja ukurasa wenye vijibox vingi
  6. Tafuta kibox kilichoanikwa name
  7. Futa name kisha andika jina unalotaka kubadili mfano firstname kumbuka hakuna kuruka nafasi katika kuandika majina.
  8. Bofya neno save lipo upande wa kulia
  9. Mpaka kufika hapo utakuwa umeweza kubadili jina la column.

 

3. Kubadili jina la column kwa kutumia SQL

Tofauti na kupitia hatuwa hizo nyingi kwa kutumia SQL unaweza kubadili kwa haraka zaidi. Kufanya hivo fata hatuwa zifuatazo:-

  1. Ingia kwenye uwanja wa SQL
  2. Kubadili jina tunatumia ALTER TABLE kisha inafata jina la table unalotaka kubadili kisha unaandika neno CHANGE kisha unafata column unayotaka kubadili  halafu unafata kuweka jina ambalo unataka iwe, kisha utamaliza na kuandika type yake ya data kisha utaweka na character length yake iwe ndani ya mabao. Mfano wa statement hi kama hii
  3. Katika table yako ya jaribio kuna column inaitwa aka sasa tunakwenda kuibadilisha kuwa nickname.
  4. ALTER TABLE jaribio CHANGE aka nickname VARCHAR(255);

 

 

4. Kuongeza column kwenye table

Sasa kuna jambo hili. Baada ya kutengeneza table kumbe ukahitaji kuongeza column. Let say kwa mfano katika table yetu ya jaribio kuna column tunataka kuiongeza kwa ajili ya kkuweka namba za simu. Na tunataka kuiita phone. Kufanya hivi fata hatuwa zifuatazo kwa kutumia MySQL:-

  1. Bofya hiyo table yako.
  2. Bofya structure
  3. Shuka chini tafuta palipoandikwa Add utaona kulia kuna kabox ndani kuna namba moja. Hapo utaamuwa je unataka kuongeza column ngapi kama ni mbili utaweka mbili. Ok kwa saa wacha hiyo moja
  4. Kisha bofya GO
  5. Ukurasa mpya utafunguka na hapo utatakiwa kujaza taarifa kama ulivyojifunza kwenye somo la sita.
  6. Kwenye jina utaweka phone, kwenye type utaweka INT kwani type ya data hapa ni namba, kwenye length weka 15
  7. Bofya save
  8. Mpaka kufika hapo table yako ya jaribio itakuwa na column nne ambapo hii ya phone imeongezeka.

 

 

5. Kuongeza column kwa kutumia SQL

Sasa tunakwenda kuongeza column nyingine ambayo tutaiita jinsia. Tutakwenda kutumia SQL kufanya haya. Hivyo baada ya hapa table yetu itakuwa na column 5. fata hatuwa zifuatazo:-

  1. Funguwa uwanja wa SQL
  2. Kuongeza column tunatumia ALTER TABLE kisha jina la table kisha ADD kisha column unayotaka kuongeza kisha type of data ilifuataiwa na character length kwenye mabano. Kisha utatakiwa kusema kuwa column hiyo itakuwa baada ya column ipi. Hapa utatumia after. Kwa mfano katika mfano wetu itakuwa after nickname Kisha alama ya ; hivyo statement hii itaonekana hivi
  3. ALTER TABLE jaribio ADD jinsia INT(15) AFTER nickname;
  4. Bofya GO
  5. Mpaka kufuka hapa utakuwa umeongeza column nyingine ya tano.

 

 

6. Kufuta column kwa kutumia MySQL

Sasa unataka kufuta moja ya colun baada ya kuona haina kazi. Kufanya hivi ni rahisi sana . fanya hivi:-

  1. Bofya table
  2. Bofya structure
  3. Utaona column zote
  4. Kulia mwa kila column kuna neno limeandikwa Drop
  5. Bofya hilo neno kulia mwa column unayotaka kuifuta kwa mfano bofya hapo kwenye nickname
  6. Kabox ka alert katakuja kuuliza kuwa je unataka kufuta kweli. Wewe piga Ok
  7. Mpaka kufikia hapo utakuwa umefuta column hiyo.

 

 

7. Kufuta column kwa kutumia SQL

Kufuta column kw akutumia SQL. Kufanya hivi kwa command za SQL fuata hatuwa hizi:-

  1. Ingia kwenye uwanja wa SQL
  2. Kufanya hivi tutatumia ALTER TABLE kija litafuata jina la table ambalo ni jaribio. Sasa tunakwenda kufuta column ya phone. Hivyo baada ya kuandika jina la table andika neno DROP likifuatiwa na column ambayo unataka kuifuta ambayo ni phone kisha maliza na alama ya ; hivyo itasomeka hivi
  3. ALTER TABLE jaribio DROP phone;
  4. Bofya GO
  5. Utatakiwa kuthibitisha weka OK
  6. Mpaka kufika hapo utakuwa umeifuta colunm ya phone.

 

 

Tukutane somo la nane tutakapojifunz ajinasi ya kuweka data kwenye database. Hakikisha kablya ya kuingia somo la nane somo la sita umelielewa vyema vinginevyo utasumbuka.

 

 

Mafunzo haya yamekujia kwa ihsani ya Bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com

 

Bongoclass
Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1291

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 5 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment

Soma Zaidi...
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)

Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 1 (HTML basic level FOR BEGINNERS)

Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tano (5)
PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

Soma Zaidi...
Php level 1 somo la saba (7)
Php level 1 somo la saba (7)

Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.

Soma Zaidi...
Utangulizi wa Android App Development
Utangulizi wa Android App Development

Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la nane (8)
PHP level 1 somo la nane (8)

Hapa utajifunza utofauti kati ya php constant na variable. Na hili ni somo la nane katika mfululizo wa masomo haya ya php level 1.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 5  (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 5)
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 5 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 5)

Karibu tena katika mafunzo haya ya html level 2 na hili ni somo la 5. Katika somo hili utajifunza zaidi kuhusu kuweka style kwenye html file.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la kumi (10)
PHP level 1 somo la kumi (10)

Somo la 10 mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza kuhusu condition statement.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)
Mafunzo ya php level 1 somo la kwanza (1)

Karibu kwenye mafunzo ya PHP level 1 na hili ni somo la kwanza. Hapa utajifunza maana ya php, inavyofanya kazi pamoja na historia yake kwa ufupi

Soma Zaidi...