Mafunzo ya hadithi zilizochaguliwa
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
7.2. Mafunzo ya Hadith Zilizochaguliwa.
- Hadith ya Kwanza; Kuamrisha mema na Kukataza Maovu.
Kutoka kwa Abi Saidil-Khudhur (r.a) amesema: Nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi Mungu anasema;
“Mwenye kuuona uovu miongoni mwenu na auondoshe kwa mkono wake, ikiwa hawezi (na aondoshe) kwa ulimi wake iwapo hawezi (na aondoshe) kwa moyo wake (achukie) na hiyo ndiyo imani dhaifu.”
(Ameipokea Muslim).
Hatua za kuondosha uovu:
- Hatua ya kwanza na bora ni kuondosha kwa mikono.
- Hatua ya pili kwa ubora ni kuondosha kwa kusema.
- Na hatua ya mwisho na dhaifu ni kuchukia moyoni.
Mafunzo ya Hadith kwa Ufupi:
- Ni wajibu kuondosha maovu kwa kisaidizi chochote kile kiwacho kulingana na mazingira.
- Jukumu la kuamrisha mema na kukataza maovu linaanzia kwa mtu mmoja mmoja na ummah kwa ujumla
- Kutochukia uovu na kuridhika nao ni dalili ya kukosa imani moyoni.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
dua ya kuomba jambo ufanikiwe
hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe
Soma Zaidi...AL-ARBAUWN AN-NAWAWIYYAH HADITHI YA 4: Uumbwaji wa mwanadamu
HAdithi hii itakufundisha namna ambavyo mwanadamu anapitia hatuwa mbalumbali tumboni mwa mama yake
Soma Zaidi...JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe.
Soma Zaidi...