Mafunzo ya hadithi zilizochaguliwa
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
7.2. Mafunzo ya Hadith Zilizochaguliwa.
- Hadith ya Kwanza; Kuamrisha mema na Kukataza Maovu.
Kutoka kwa Abi Saidil-Khudhur (r.a) amesema: Nimemsikia mjumbe wa Mwenyezi Mungu anasema;
“Mwenye kuuona uovu miongoni mwenu na auondoshe kwa mkono wake, ikiwa hawezi (na aondoshe) kwa ulimi wake iwapo hawezi (na aondoshe) kwa moyo wake (achukie) na hiyo ndiyo imani dhaifu.”
(Ameipokea Muslim).
Hatua za kuondosha uovu:
- Hatua ya kwanza na bora ni kuondosha kwa mikono.
- Hatua ya pili kwa ubora ni kuondosha kwa kusema.
- Na hatua ya mwisho na dhaifu ni kuchukia moyoni.
Mafunzo ya Hadith kwa Ufupi:
- Ni wajibu kuondosha maovu kwa kisaidizi chochote kile kiwacho kulingana na mazingira.
- Jukumu la kuamrisha mema na kukataza maovu linaanzia kwa mtu mmoja mmoja na ummah kwa ujumla
- Kutochukia uovu na kuridhika nao ni dalili ya kukosa imani moyoni.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π3 Kitabu cha Afya π4 Madrasa kiganjani π5 web hosting π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba
Nini kilichangia ongezeko la uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba.
Soma Zaidi...MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.
Soma Zaidi...DUA 113 - 126
DUA ZA WAKATI WA SHIDA Dua ya wakati wa taabu βLAA ILAAHA ILLA-LLAHUL-βADHIMUL-HALIIMU.
Soma Zaidi...Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 2: Ujio wa Jibril kwa Mtume (s.a.w)
Hii ni hadithi ya pili katika kitabu cha Arbain Nawawiy
Soma Zaidi...