Ria ni kinyume cha Ikhlas.
Ria ni kinyume cha Ikhlas. Kufanya ria ni kufanya jambo jema ili watu wakuone, wakusifu, wakupe shukurani, n.k. Mtu anayefanya ria hafanyi wema kwa kutarajia malipo kutoka kwa Allah (s.w) bali hufanya kwa kutarajia malipo ya hapa duniani tu, iwe ni mali au sifa au shukurani.
Mwenye kufanya ria hata akijiita Muislamu hana malipo yoyote mbele ya Alllah(s.w) katika siku ya Hukumu isipokuwa adhabu kali Motoni kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:-
“Wanaotaka maisha ya dunia na mapambo yake, tutawapa huku duniani (ujira wa) vitendo vyao kamili, humu wao hawatapunjwa. Hao ndio ambao hawatakuwa na kitu katika akhera ila moto na wataruka patupu waliyoyafanya katika dunia hii na yatakuwa bure waliyokuwa wakiyatenda.” (11:15-16)
Katika aya nyingine Allah (s.w) anatukamia:
“Basi adhabu (kali) itawathubutikia wanaoswali; ambao wanapuuza swala zao. Ambao hufanya riyaa ”. (107:4)
Katika Hadith tunafahamishwa kuwa Mtume (s.a.w) amesema:
“Katika siku ya hukumu, vitendo vyote vilivyofanywa hapa duniani vitahudhurishwa mbele ya Allah (s.w). Vitendo vilivyofanywa kwa ajili ya Allah (s.w) vitatengw a. Na vitendo vingine vilivyofanyw a kw a nia nyingine mbali mbali vitatupw a motoni”. (Baihaqi).
Umeionaje Makala hii.. ?
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani.
Soma Zaidi...Download kitabu hiki na upate kusoma zaidi ya dua 120, pamoja na darsa mbalimbali za dini ya kiislamu.
Soma Zaidi...Wapo watu kadhaa ambao waliomba dua hazirudi. Hapa nitakueleza wawili ambao ni mzazi na msafiri.
Soma Zaidi...HAdithi hii itakufundisha namna ambavyo mwanadamu anapitia hatuwa mbalumbali tumboni mwa mama yake
Soma Zaidi...As salaam alaykum warahmatullah wabarakatuh, nauliza inajuzu wanawake kuzuru makaburi?
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukugundisha dua ambazo itazitumia katika swala yako.
Soma Zaidi...