Ria ni kinyume cha Ikhlas.
Ria ni kinyume cha Ikhlas. Kufanya ria ni kufanya jambo jema ili watu wakuone, wakusifu, wakupe shukurani, n.k. Mtu anayefanya ria hafanyi wema kwa kutarajia malipo kutoka kwa Allah (s.w) bali hufanya kwa kutarajia malipo ya hapa duniani tu, iwe ni mali au sifa au shukurani.
Mwenye kufanya ria hata akijiita Muislamu hana malipo yoyote mbele ya Alllah(s.w) katika siku ya Hukumu isipokuwa adhabu kali Motoni kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:-
“Wanaotaka maisha ya dunia na mapambo yake, tutawapa huku duniani (ujira wa) vitendo vyao kamili, humu wao hawatapunjwa. Hao ndio ambao hawatakuwa na kitu katika akhera ila moto na wataruka patupu waliyoyafanya katika dunia hii na yatakuwa bure waliyokuwa wakiyatenda.” (11:15-16)
Katika aya nyingine Allah (s.w) anatukamia:
“Basi adhabu (kali) itawathubutikia wanaoswali; ambao wanapuuza swala zao. Ambao hufanya riyaa ”. (107:4)
Katika Hadith tunafahamishwa kuwa Mtume (s.a.w) amesema:
“Katika siku ya hukumu, vitendo vyote vilivyofanywa hapa duniani vitahudhurishwa mbele ya Allah (s.w). Vitendo vilivyofanywa kwa ajili ya Allah (s.w) vitatengw a. Na vitendo vingine vilivyofanyw a kw a nia nyingine mbali mbali vitatupw a motoni”. (Baihaqi).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika uislamu inaonkana katika maeneo yafuatayo: Kwanza, Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya hadithi al Quds na Hadith an-Nabawiy
Soma Zaidi...Posti hii inakwenda kukupa orodha ya dua 10 ambazo unaweza kuziomba kila siku.
Soma Zaidi...DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 1.
Soma Zaidi...Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha umuhimu wa nasaha katika dini
Soma Zaidi...Hizi ni Dua ambazo unatakiwa uziombe wakati wa shida na taabu
Soma Zaidi...