Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Hadith ya Tatu: Ukarimu na Kusaidiana.
Kutoka kwa Abi Saidil-Khudhur (r.a) kasema: ilitokezea tumo safarini pamoja na Mtume (s.a.w); akaja mtu mmoja juu ya kipando chake, akawa anaangaza kulia na kushoto, Mtume (s.a.w) akasema;
“Mwenye kipando cha ziada na ampe msaada asiye na kipando, na mwenye chakula kilichozidi (matumizi yake) na ampe msaada mwenye kukihitaji (asiyenacho)”
Akataja aina mbali mbali za mali mpaka tukaona (tukajua) kwamba hatuna haki ya kuweka ziada (baada ya matumizi yetu).
(Ameipokea Muslim)
Mafunzo ya Hadith kwa Ufupi:
- Ni wajibu wa kila muislamu aliyenacho kumtilia hima kila anayehitaji msaada wa kibinaadamu.
- Ugawaji mbaya wa rasilimali na utajiri ndio sababu ya kuwepo matabaka ndani ya jamii.
- Uislamu umekataza kuhodhi bidhaa muhimu kwani kinyume cha sheria.
- Uislamu umetilia mkazo maisha bora kwa kila raia na kukataza kufanya israfu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Share follows: 0 |
Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
👉1 ai web app 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
dua ya kuomba jambo ufanikiwe
hii ni damna ya kuomba dua ukubaliwe, dua ya kuomba jambo ufanikiwe
Soma Zaidi...Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 3: Nguzo za uislamu
Katika hadithi hii utakwenda kujifunza nguzo za uislamu
Soma Zaidi...