Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana
Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)
- Hadith ya Tatu: Ukarimu na Kusaidiana.
Kutoka kwa Abi Saidil-Khudhur (r.a) kasema: ilitokezea tumo safarini pamoja na Mtume (s.a.w); akaja mtu mmoja juu ya kipando chake, akawa anaangaza kulia na kushoto, Mtume (s.a.w) akasema;
“Mwenye kipando cha ziada na ampe msaada asiye na kipando, na mwenye chakula kilichozidi (matumizi yake) na ampe msaada mwenye kukihitaji (asiyenacho)”
Akataja aina mbali mbali za mali mpaka tukaona (tukajua) kwamba hatuna haki ya kuweka ziada (baada ya matumizi yetu).
(Ameipokea Muslim)
Mafunzo ya Hadith kwa Ufupi:
- Ni wajibu wa kila muislamu aliyenacho kumtilia hima kila anayehitaji msaada wa kibinaadamu.
- Ugawaji mbaya wa rasilimali na utajiri ndio sababu ya kuwepo matabaka ndani ya jamii.
- Uislamu umekataza kuhodhi bidhaa muhimu kwani kinyume cha sheria.
- Uislamu umetilia mkazo maisha bora kwa kila raia na kukataza kufanya israfu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitabu cha Afya π2 Kitau cha Fiqh π3 Simulizi za Hadithi Audio π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 Madrasa kiganjani π6 web hosting
Post zinazofanana:
DUA na Adhkar kutoka kwenye quran
hii ni orodha ya dua mbalimbali kutoka kwenye quran. Unaweza kuzitumia dua hizi kujipendekeza kwa Allah na kupata msamaha, neema na mengineyo.
Soma Zaidi...Wajbu wa wazazi kwa watoto wao
Wajibu wa Wazazi kwa Watoto Wazazi wanawajibu kwa watoto wao.
Soma Zaidi...Vyanzo vitano vya elimu zote duniani: Chanzo cha Elimu ni Allah (s.w)
Kama tunavyojifunza katika surat βAlaq (96:4-5), chanzo cha elimu au mkufunzi wa binadamu ni Allah (s.
Soma Zaidi...