Menu



Hadithi ya tatu:ukarimu na kusaidiana

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

 

Kutoka kwa Abi Saidil-Khudhur (r.a) kasema: ilitokezea tumo safarini pamoja na Mtume (s.a.w); akaja mtu mmoja juu ya kipando chake, akawa anaangaza kulia na kushoto, Mtume (s.a.w) akasema;

 

“Mwenye kipando cha ziada na ampe msaada asiye na kipando, na mwenye chakula kilichozidi (matumizi yake) na ampe msaada mwenye kukihitaji (asiyenacho)”

 

Akataja aina mbali mbali za mali mpaka tukaona (tukajua) kwamba hatuna haki ya kuweka ziada (baada ya matumizi yetu).

(Ameipokea Muslim)




 

Mafunzo ya Hadith kwa Ufupi:

  1. Ni wajibu wa kila muislamu aliyenacho kumtilia hima kila anayehitaji msaada wa kibinaadamu.
  2. Ugawaji mbaya wa rasilimali na utajiri ndio sababu ya kuwepo matabaka ndani ya jamii.
  3. Uislamu umekataza kuhodhi bidhaa muhimu kwani kinyume cha sheria. 
  4. Uislamu umetilia mkazo maisha bora kwa kila raia na kukataza kufanya israfu.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Views 1470

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA

NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA.

Soma Zaidi...
DUA ZA KUONDOA WASIWASI

DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.

Soma Zaidi...
Masharti ya kukubaliwa kwa dua

Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua.

Soma Zaidi...
Adhkari unazoweza kuomba kila siku

Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu

Soma Zaidi...