JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe.
Ili kuomba dua itakayokubaliwa unatakiwa uzingatie adabu za dua, nyakati za kuomba dua pia ujuwe hali zinazozunguruka dua yako. Hapa nitakueleza baadhi ya taratibu za kuomba dua itakayokubaliwa
Zingatia adabu na taratibu za dua kama ifuatavyo:-
1. Omba dua ukiwa twahara
2. Elekea kibla
3. kuwa twahara katika mavazi na mwili
4. Anza na kumsifu Allah (Tahmid, kwa kusema Alhamduliilahi rabbil-'alamiina)
5. Mswalie mtume (Swala ya mtume)
6. waombee dua waislamu wote
7.Taka istighfar kwa kusema Astaghfirullah (mara kadhaa)
8. sasa omba dua yako
Zingatia nyakati za kuomba dua. Nyakati zifatazo dua hukubaliwa rahisi:-
1. siku ya ujumaa
2. usiku wa manane
3. Baada ya Swala
4. Baada ya adhana
5. Wakati ukiwa umefunga
6. Wakati unapofanya jambo jema la kumfurahisha Allah
Pia omba Dua yako katika hali hizi:-
1. ukiwa umefunga
2. baada ya kusoma quran
3. Toa sadaka kisha muombe Allah dua yako
4. Mfanyie wema mtu aliye mbali akikuombea dua yake itakubaliwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
ADHKAR NA DUA
ADHKARI MBALIMBALI NA DUA Hapa tutajifunza dua mbalimbali ambazo ni adhkari.
Soma Zaidi...SHUGHULI ZA KILA SIKU
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Uandishi wa Hadithi wakati wa Matabiina
Historia ya uandishi wa hadithibwakati wa Matabiina, yaani wafuasi wa maswahaba
Soma Zaidi...Dua ya wakati wa kuvaa nguo
Mtume Muhammad (s.a.w) ametufundisha maneno ya kuyasema (Dua) wakati unavaa nguo.
Soma Zaidi...