Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.
Yafuatayo Ni maandalizi ya Mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia;
1.kuwepo na usafiri ; mama anapo hudhurua clinic hufundishwa dalili za Hatari hivyo ujauzito sio kitu Cha kushtukiza hvyo unatakiwa kujipanga ili kutafuta usafiri mapema .
2.mtu atakayebaki nyumba; husaidia kulinda nyumba na familia iliyobaki pia na kuangalia usalama wa hapo nyumbani.
3.mtu wa kumsindikiza; mama anapoenda kujifungua awe na msaidizi kwa ajili ya kuenda kumsaidia na msindikizaji huyu awe anajiweza ili aweze kumsaidia mama pale atakapohitajika msaada wake.
4. Vifaa vya kujifungulia; Kawaida mama akiwa anahudhuria cliniki hupewa mwongozo wa kila kitu hivyo anatakiwa awe na vifaa kwa ajili ya kujifungulia ,na vifaa hivyo Ni Kama vile
1. karatasi aina ya nailoni kwaajili ya kutandikia kitanda anachojifungulia mama ili kuepusha kuchafua mazingira.
2. mipira ya Kuvaa mikononi (gloves) hizi hutumika wahudumu wanapokua wanamuhudumia mama akiwa anajifungua.
3. Kiwembe Cha Upasuaji hutumika kukatia kitovu kilichounganisha Mtoto na kondo la nyuma ili kutenganisha pia kukatia nyuzi wakati mama anaposhonwa Kama akiwa amechanika.
4. kibanio Cha kitovu (clamp) hutumika kubania kitovu kikitenganishwa ili kisitoe Damu.
-5. vitenge au khanga ; ambazo hutumika kumfunikia mtoto,kutandikia kwenye nailoni,mama kujifungua na nguo hizi zisiwe mpya ziwe Ni khanga zilizotumika.
6. malapa ambayo atavaa mam anapotaka kwenda kuoga,kufanya mazoezi maana hawezi kutembea bila kitu mguuni.
7. beseni (dishi) au ndoo ndogo hutumika kuwekea ndoo chafu pia kiafa hiki hutumika mama kunisaidia wakati anakaribia kujifungua maana hauruhusiwi kwenda chooni.
8. sabuni na mafuta ya mama
9. Pamba kubwa na nyuzi za upasuaji
10. pedi kubwa za mama ambapo akijifungua anaweza kuitumia Ila so lazima maana mama anaweza kuitumia khanga.
11. vifaa vya Mtoto Kama vile soksi, bebshoo,pampasi,kofia,mafuta ya Nazi ili vimpatie Mtoto joto pia na leso laini kwaajili ya kumfutia Mtoto.
5.fedha; mama na familia kiujumla wanatakiwa kujipanga kwa matumizi ya hela pale zitakapohitajika wawe nazo.
Mwisho; mama mjamzito anapohudhuria kliniki hupewa mwongozo wote na swala la ujauzito sio la kushtukiza Ni kitu ambacho kipo wazi hivi mama au familia unatakiwa kujipanga na maandalizi.
Mwisho; mama mjamzito anapojigundua tu kuwa ana mimba anatakiwa awahi cliniki kwaajili ya kupewa eleimu juu ya kujikinga,Mambo Hatari kujua na vifaa na Mambo mengine mengi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sifa ambazo mtoto mchanga anapaswa kuwa Nazo,ni sifa ambazo lazima zionekane kwa mtoto mchanga pale anapozaliwa na zikikosa ni lazima kuja kuwa mtoto ana matatizo mbalimbali kwa hiyo zifuatazo ni sifa za mtoto mchanga kama ifuatavy
Soma Zaidi...Jifunze muda ambao mjamzito hatatkiwa kishiriki tendo la ndoa. je kuna madhara kwa mjamzito kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa, ni njia zitoleeazo na wakunga Ili kumtunza mtoto mchanga aliyezaliwa.
Soma Zaidi...Hii ni orodha ya dawa ambazo hutumiwa sana na watu kutoka maduka ya dawa lakini sio salama kwa wajawazito.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kujaa tmgesi tumbon
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea ugonjwa wa kisukari wakati mama akiwa mjamzito.na yafuatayo ni Mambo hatari yanayotokea wakati Mama akiwa na ujauzito.
Soma Zaidi...Dalili za kuharibika kwa ujauzito na dalili za kuharibika kwa ujauzo
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi vyakula mbalimbali vya kuongeza tendo la ndoa, kwa kawaida kuna vyakula mbalimbali ambavyo watu ukitumia ili kuweza kuongeza tendo la ndoa vyakula hivyo ni kama tutakavyoona hapo baadaye
Soma Zaidi...