Maandalizi ya mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia.

Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.

   Yafuatayo Ni maandalizi ya Mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia;

1.kuwepo na usafiri ; mama anapo hudhurua clinic hufundishwa dalili za Hatari hivyo ujauzito sio kitu Cha kushtukiza hvyo unatakiwa kujipanga ili kutafuta usafiri mapema .

 

2.mtu atakayebaki nyumba; husaidia kulinda nyumba na familia iliyobaki pia na kuangalia usalama wa hapo nyumbani.

 

3.mtu wa kumsindikiza; mama anapoenda kujifungua awe na msaidizi kwa ajili ya kuenda kumsaidia na msindikizaji huyu awe anajiweza ili aweze kumsaidia mama pale atakapohitajika msaada wake.

 

4. Vifaa vya kujifungulia; Kawaida mama akiwa anahudhuria cliniki hupewa mwongozo wa kila kitu hivyo anatakiwa awe na vifaa kwa ajili ya kujifungulia ,na vifaa hivyo Ni Kama vile

   1. karatasi aina ya nailoni kwaajili ya kutandikia kitanda anachojifungulia mama ili kuepusha kuchafua mazingira.

  2. mipira ya Kuvaa mikononi (gloves) hizi hutumika wahudumu wanapokua wanamuhudumia mama akiwa anajifungua.

  3. Kiwembe Cha Upasuaji hutumika kukatia kitovu kilichounganisha Mtoto na kondo la nyuma ili kutenganisha pia kukatia nyuzi wakati mama anaposhonwa Kama akiwa amechanika.

  4. kibanio Cha kitovu (clamp) hutumika kubania kitovu kikitenganishwa ili  kisitoe Damu.

  -5. vitenge au khanga ; ambazo hutumika kumfunikia mtoto,kutandikia kwenye nailoni,mama kujifungua na nguo hizi zisiwe mpya ziwe Ni khanga zilizotumika.

  6. malapa ambayo atavaa mam anapotaka kwenda kuoga,kufanya mazoezi maana hawezi kutembea bila kitu mguuni.

  7. beseni (dishi) au ndoo ndogo hutumika kuwekea ndoo chafu pia kiafa hiki hutumika mama kunisaidia wakati anakaribia kujifungua maana hauruhusiwi kwenda chooni.

  8. sabuni na mafuta ya mama

  9. Pamba kubwa na nyuzi za upasuaji

  10. pedi kubwa za mama ambapo akijifungua anaweza kuitumia Ila so lazima maana mama anaweza kuitumia khanga.

  11. vifaa vya Mtoto Kama vile soksi, bebshoo,pampasi,kofia,mafuta ya Nazi ili vimpatie Mtoto joto pia na leso laini kwaajili ya kumfutia Mtoto.

 

5.fedha; mama na familia kiujumla wanatakiwa kujipanga kwa matumizi ya hela pale zitakapohitajika wawe nazo.

 

    Mwisho; mama mjamzito anapohudhuria kliniki hupewa mwongozo wote na swala la ujauzito sio la kushtukiza Ni kitu ambacho kipo wazi hivi mama au familia unatakiwa kujipanga na maandalizi.

 

Mwisho; mama mjamzito anapojigundua tu kuwa ana mimba anatakiwa awahi cliniki kwaajili ya kupewa eleimu juu ya kujikinga,Mambo Hatari kujua na vifaa na Mambo mengine mengi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 13745

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Dalili za upungufu wa homoni ya projestron

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.

Soma Zaidi...
Dalili za PID

Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana

Soma Zaidi...
ZIJUWE DALILI KUU 5 ZA MIMBA CHANGA

Dalili za mimba, na m,imba changa

Soma Zaidi...
Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...
Je kukosa hedhi kwa mwanmke anayenyonyesha ni dalili ya mimba

Kipimo cha mimba cha mkojo hakiwezi kyonyesha mimva changa sana. Hivyo kama ni mimba baada ya wikibpima tena itaweza kuonekana. Dalili hizobulizotaja pekee haziashirii mimba tu huwenda ni homoni zimebadilika kidogo, ama una uti.

Soma Zaidi...
mkewang alikuwa anasumbuliwa na tumbo kama siku tatu lika tuliya saivi analalamika kiuno na mgongo vina muuma nini tatizo tockt

Maumivu ya tumbo nakiuno kwa mwanamke yanahitaji uangalizi wakina. Kwani kuna sababu nyingi ambazo zinawezakuwa ni chanzo.

Soma Zaidi...
Madhara ya kupungua kwa homoni ya projestron

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa homoni ya projestron ikipungua mwilini na pia kuweza kutambua dalili za kupungua kwa homoni hii ya progesterone.

Soma Zaidi...
Magonjwa madogo madogo kwa Mama wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa madogo madogo kwa akina Mama wajawazito, ni magonjwa ambayo hayawezi kupelekea kupoteza maisha kwa Mama mjamzito, magonjwa haya upotea ikiwa Mama atajifungua.

Soma Zaidi...
Nini husababisha upungufu wa nguvu za kiume

Post hii itakujulidha mambo ambayo hupunguza nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Sababu za Mayai kushindwa kuzalishwa kwa mwanamke

Posti hii inahusu zaidi sababu za kushindwa kuzalishwa mayai kwa mwanamke, ni tatizo ambalo utokea kwa mwanamke ambapo mwanamke anashindwa kuzalisha mayai.

Soma Zaidi...