picha

Mabadiliko kwenye tumbo la uzazi wa Mama anapobeba Mimba.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye tumbo la uzazi la Mama pindi anapobeba mimba, ni mabadiliko yanayotokea kwa mwanamke anapobeba mimba kama ifuatavyo.

Mabadiliko kwenye Tumbo la Mama anapobeba mimba.

1.Mama anapobeba tu mimba tumbo la uzazi  linakomaa na kuwa na mazingira ya kumpatia mtoto chakula  na mazingira kwa ajili ya kukua kwa mtoto, hii utokea pale ambapo mimba ukomaliza kutungwa tu tumbo la uzazi uandaliwa kwa ajili ya kutunza mimba iliyotungwa na namna ya kulisha mimba iliyotungwa kwa miezi Tisa mpaka pale mtoto anapozaliwa.

 

2.Baada ya  Mimba iliyotungwa kutoka kwenye milija ambapo mimba utungiwa kwa kitaalamu huitwa follapian tube mimba ushuka mpaka kwenye tumbo la uzazi hapo placenta utengenezwa na kumalizika kwa mda wa wiki Kumi, na kazi za hiyo placenta ni kusafilisha hewa Safi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, kusafirisha chakula kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, hewa chafu kutoka kwa mtoto kwenda kwa Mama na pia kuzuia sumu kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.

 

3.Sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa myometrium kwa kusaidia a na homoni ambayo huitwa ostrogen usaidia kukomaa kwa misuli ambayo IPO ndani ya tumbo, hiyo misuli ukua na kukomaa kwa ajili ya kutunza mtoto.

 

4. Kiwango Cha uzito wa tumbo la uzazi uongezeka kutoka kwenye hali ya kawaida ambayo ni 60gm kama mwanamke Hana mimba mpaka 1000gm ikiwa mwanamke ana mimba, kwa hiyo hiki ni kiwango kikubwa kutoka 60gm mpaka 1000gm kwa hiyo sehemu ya tumbo la uzazi inabidi kuandaliwa vizuri Ili kuweza kumtunza vyema mtoto.

 

5. Size ya mlango wa kizazi nayo ubadilika kutoka kwenye hali ya kawaida ambayo ni 7.5 mara 5 mara 2.5 mpaka 30 mara 22.5 mara 20 in cm. Tunaona size kabla mama hajabeba mimba ni tofauti kabisa na baada ya kubeba mimba kwa hiyo Mama anapaswa kuangaliwa kwa namna ya pekee kwa sababu ya Mzigo Mzito aliubeba.

 

6. Na pia kwenye mlango wa uzazi mishipa ya damu unaongezeka Ili iweze kusambaza damu vizuri kwa Mama na mtoto  na pia kuweza kufanya kazi ya placenta vizuri Ili damu kwa mtoto na Mama iweze kutosha kwa kiwango kinachohitajika kwa hiyo Mama akiwa na Mimba mishipa ya damu uongezeka kwa namba na idadi Ili kusambaa kwa damu ya kutosha kwa Mama na Mtoto.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2228

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 ai web app     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...
Damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu damu, uteute na maji yanayotoka ukeni kipindi cha ujauzito

Soma Zaidi...
Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.

Soma Zaidi...
Madhara ya fangasi ukeni

Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke.

Soma Zaidi...
mimi mara ya mwisho kubleed ilikuwa tareh 3/9 nilisex tarehe 4 je ni kwel nna mimba maana hadi sasa sijableed au ni kawaida tu

Je unaijuwa siku yako hatari ya kupata mimba. Na itakuwaje kama tayari umebeba mimba changa. Nakala hii inakwenda kukushauri machache kuhusu maswali haya.

Soma Zaidi...
Aina za uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za uvimbe kwenye kizazi, uvimbe unatokea kwenye kizazi ila utofautiana kulingana na sehemu ambazo uvimbe huo umepata.

Soma Zaidi...