Mabadiliko kwenye tumbo la uzazi wa Mama anapobeba Mimba.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye tumbo la uzazi la Mama pindi anapobeba mimba, ni mabadiliko yanayotokea kwa mwanamke anapobeba mimba kama ifuatavyo.
Mabadiliko kwenye Tumbo la Mama anapobeba mimba.
1.Mama anapobeba tu mimba tumbo la uzazi linakomaa na kuwa na mazingira ya kumpatia mtoto chakula na mazingira kwa ajili ya kukua kwa mtoto, hii utokea pale ambapo mimba ukomaliza kutungwa tu tumbo la uzazi uandaliwa kwa ajili ya kutunza mimba iliyotungwa na namna ya kulisha mimba iliyotungwa kwa miezi Tisa mpaka pale mtoto anapozaliwa.
2.Baada ya Mimba iliyotungwa kutoka kwenye milija ambapo mimba utungiwa kwa kitaalamu huitwa follapian tube mimba ushuka mpaka kwenye tumbo la uzazi hapo placenta utengenezwa na kumalizika kwa mda wa wiki Kumi, na kazi za hiyo placenta ni kusafilisha hewa Safi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, kusafirisha chakula kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, hewa chafu kutoka kwa mtoto kwenda kwa Mama na pia kuzuia sumu kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.
3.Sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa myometrium kwa kusaidia a na homoni ambayo huitwa ostrogen usaidia kukomaa kwa misuli ambayo IPO ndani ya tumbo, hiyo misuli ukua na kukomaa kwa ajili ya kutunza mtoto.
4. Kiwango Cha uzito wa tumbo la uzazi uongezeka kutoka kwenye hali ya kawaida ambayo ni 60gm kama mwanamke Hana mimba mpaka 1000gm ikiwa mwanamke ana mimba, kwa hiyo hiki ni kiwango kikubwa kutoka 60gm mpaka 1000gm kwa hiyo sehemu ya tumbo la uzazi inabidi kuandaliwa vizuri Ili kuweza kumtunza vyema mtoto.
5. Size ya mlango wa kizazi nayo ubadilika kutoka kwenye hali ya kawaida ambayo ni 7.5 mara 5 mara 2.5 mpaka 30 mara 22.5 mara 20 in cm. Tunaona size kabla mama hajabeba mimba ni tofauti kabisa na baada ya kubeba mimba kwa hiyo Mama anapaswa kuangaliwa kwa namna ya pekee kwa sababu ya Mzigo Mzito aliubeba.
6. Na pia kwenye mlango wa uzazi mishipa ya damu unaongezeka Ili iweze kusambaza damu vizuri kwa Mama na mtoto na pia kuweza kufanya kazi ya placenta vizuri Ili damu kwa mtoto na Mama iweze kutosha kwa kiwango kinachohitajika kwa hiyo Mama akiwa na Mimba mishipa ya damu uongezeka kwa namba na idadi Ili kusambaa kwa damu ya kutosha kwa Mama na Mtoto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 ai web app 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko ya mzunguko wa damu kwa wajawazito, tunajua wazi kuwa wajawazito pindi ujauzito ukiingia tu, kila kitu kwenye mwili ubadilika vile vile na mzunguko wa damu ubadilika.
Soma Zaidi...Mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama.
Soma Zaidi...Fahamu dalili za hatari kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa mama mjamzito, kwa sababu kuna baadhi ya Dalili zikitokea kwa mama mjamzito ni vizuri kabisa kuwahi hospitali mara moja.
Soma Zaidi...Dalili za mama mjamzito akikaribia kujifungua
Post hii inazungumzia mama wajawazito Mara tu mama anapohisi kuwa yeye ni mjamzito anashauriwa kuanza clinic.na clinic hizi zinasaidia kuwapatia wakina mama elimu,namna ya kumkinga Mtoto asipatwe na maradhi Kama UKIMWI. Pia mama anapoanza clinic
Soma Zaidi...DALILI ZA UJAUZITO KICHEFU CHEFU, KUTAPIKA, HEDHI, DAMU UKENI, KUJOJOAKOJOA N.K (mimba changa, mimba ya wiki moja, mimba ya mwezi mmoja )
DALILI KUU ZA MIMBA (UJAUZITO) Watu wengi sana wamekuwa wakilalamika kuwa mimba zao zinatoka, ama kupotea bila ya kujulikana tatizo wala bila ya kuugua.
Soma Zaidi...Hiv n kweli majivu hutoa mimb ya siku moja hadi wiki moja
Inashangaza sana, wakati wengine wanahangaika kutafutavijauzito kwa gharama yoyote ile, kuna wengine wanataka kutoa ujauzito kwa gharama yeyote ile. Unadhani njia za kienyeji sa kutoa mimba ni salama?
Soma Zaidi...