Mabadiliko kwenye tumbo la uzazi wa Mama anapobeba Mimba.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye tumbo la uzazi la Mama pindi anapobeba mimba, ni mabadiliko yanayotokea kwa mwanamke anapobeba mimba kama ifuatavyo.
Mabadiliko kwenye Tumbo la Mama anapobeba mimba.
1.Mama anapobeba tu mimba tumbo la uzazi linakomaa na kuwa na mazingira ya kumpatia mtoto chakula na mazingira kwa ajili ya kukua kwa mtoto, hii utokea pale ambapo mimba ukomaliza kutungwa tu tumbo la uzazi uandaliwa kwa ajili ya kutunza mimba iliyotungwa na namna ya kulisha mimba iliyotungwa kwa miezi Tisa mpaka pale mtoto anapozaliwa.
2.Baada ya Mimba iliyotungwa kutoka kwenye milija ambapo mimba utungiwa kwa kitaalamu huitwa follapian tube mimba ushuka mpaka kwenye tumbo la uzazi hapo placenta utengenezwa na kumalizika kwa mda wa wiki Kumi, na kazi za hiyo placenta ni kusafilisha hewa Safi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, kusafirisha chakula kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto, hewa chafu kutoka kwa mtoto kwenda kwa Mama na pia kuzuia sumu kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.
3.Sehemu ya ndani ya tumbo la uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa myometrium kwa kusaidia a na homoni ambayo huitwa ostrogen usaidia kukomaa kwa misuli ambayo IPO ndani ya tumbo, hiyo misuli ukua na kukomaa kwa ajili ya kutunza mtoto.
4. Kiwango Cha uzito wa tumbo la uzazi uongezeka kutoka kwenye hali ya kawaida ambayo ni 60gm kama mwanamke Hana mimba mpaka 1000gm ikiwa mwanamke ana mimba, kwa hiyo hiki ni kiwango kikubwa kutoka 60gm mpaka 1000gm kwa hiyo sehemu ya tumbo la uzazi inabidi kuandaliwa vizuri Ili kuweza kumtunza vyema mtoto.
5. Size ya mlango wa kizazi nayo ubadilika kutoka kwenye hali ya kawaida ambayo ni 7.5 mara 5 mara 2.5 mpaka 30 mara 22.5 mara 20 in cm. Tunaona size kabla mama hajabeba mimba ni tofauti kabisa na baada ya kubeba mimba kwa hiyo Mama anapaswa kuangaliwa kwa namna ya pekee kwa sababu ya Mzigo Mzito aliubeba.
6. Na pia kwenye mlango wa uzazi mishipa ya damu unaongezeka Ili iweze kusambaza damu vizuri kwa Mama na mtoto na pia kuweza kufanya kazi ya placenta vizuri Ili damu kwa mtoto na Mama iweze kutosha kwa kiwango kinachohitajika kwa hiyo Mama akiwa na Mimba mishipa ya damu uongezeka kwa namba na idadi Ili kusambaa kwa damu ya kutosha kwa Mama na Mtoto.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Habari Mimi ni mjamzito was miezi Tisa sasa nimeanza kutokwa na maji kidogo kidogo ukeni bila uchungu na no mimba yangu ya kwanza he Kuna shida?
Ujauzito husababisha mabadiliko mengi mwilini, ikiwepo ongezeko la Majimaji ukeni ifikapo tarehe za kukaribia kujifunguwa. Majimaji haya ni muhimu kwa afya ya mtoto aliye tumboni.
Soma Zaidi...Dalili za Maambukizi na Uvimbe katika mirija ya uzazi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na maambukizi na uvimbe katika mirija ya uzazi. Mara nyingi hutumiwa sawa na ugonjwa wa uvimbe kwenye fupa nyonga (PID), ingawa PID haina ufafanuzi sahihi na inaweza kurejelea magonjwa kadhaa ya njia ya juu ya uzazi
Soma Zaidi...Vyakula vinavyosaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone
Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo usaidia katika uzalishaji wa homoni ya testosterone.
Soma Zaidi...Fahamu siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba.
Posti hii inahusu zaidi siku za kubeba mimba na zisizo za kubeba mimba , tunapaswa kujua hivi Ili kuweza kupanga uzazi na kuepuka njia ambazo ni hatarishi kwa afya zetu.
Soma Zaidi...VYAKULA VYA KUONGEZA HAMU YA TENDO LA NDOA NA NGUVU ZA KIUME
Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.
Soma Zaidi...Je dalili ya kuuma tumbo huanza baada ya wiki ngapi Toka mwanamke apate ujauzito?
Maumivu ya tumbo ni moja katika dalili za ujauzito. Maumivu wanawake wengi hushindwa kujuwa kuwa ni ujauzito ama laa. Na hii ni kwa sababu kwa wanawake wengi maumivu ya tumbo ama changu ni jalivya kawaida kwao.
Soma Zaidi...