Maana ya kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

 

4.2. Maana ya Kusimamisha Swala.

Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo, sharti zote za swala na kuwa na unyenyekevu (khushui) ndani ya swala. 

 

Nafasi na Umuhimu wa Kusimamisha Swala katika Uislamu.

Swala imesisitizwa na ina umuhimu katika Uislamu kwa sababu zifuatazo;

 

Kusimamisha Swala ni Amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Mwenyezi Mungu (s.w) ameamrisha waumini (waislamu) wote wasimamishe swala zote za faradh na sunnah ipasavyo.

Rejea Quran (29:45), (4:103) na (14:31).

 

Kusimamisha swala ni nguzo ya Pili ya Uislamu.

Baada ya shahada mbili, nguzo ya pili na ya msingi mno katika Uislamu ni kusimamisha swala.

 

Swala humtakasa muislamu na mambo machafu na maovu.

Bila shaka swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mja na mambo machafu na maovu.

Rejea Quran (29:45).

 

Swala ni amali ya mwanzo kabisa kuhesabiwa siku ya Qiyama.

Swala ya muumini ikitengemaa vizuri ndio sababu ya kufaulu kwake Duniani na Akhera pia.

Rejea Quran (23:1-2,9), (87:14-15) na (22:34-35).

 

Kutosimamisha swala ni sababu ya mtu kuingizwa motoni.

Hii ni baada ya muislamu Kupuuza swala kwa kutozingatia sharti na nguzo zake kikamilifu na kukosa unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.

Rejea Quran (74:42-47), (68:42-43) na (107:4-5).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3095

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 web hosting    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.

Soma Zaidi...
Mambo yanayobatilisha funga au yanayoharibu swaumu.

Hapa utajifunza mambo ambayo akiyafanya mtu aliyefunga, basi funga yake itaharibika.

Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na namna ya kuzitekeleza

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Namna ya kutawadha yaani kuchukuwa udhu

Kuchukuwavudhu ni ibada, lakini pia ni matendo ya kuufanya mwilivuwe safi. Katika post nitakwenda kukifundisha namna ya kutia udhu katika uislamu.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya uchumi katika uislamu

Katikabuislamu dhana ya uchumi imetofautiana na dhana ya kidunia hivi leo ambapo kamari na riba ni moja ya vitu muhimu katika uchumi.

Soma Zaidi...
Swala ya witiri na faida zake, na jinsi ya kuiswali

Hapa utajifunza jinsi ya kuswali swala ya witiri na faida zake kwa mwenye kuiswali.

Soma Zaidi...