Maana ya kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

 

4.2. Maana ya Kusimamisha Swala.

Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo, sharti zote za swala na kuwa na unyenyekevu (khushui) ndani ya swala. 

 

Nafasi na Umuhimu wa Kusimamisha Swala katika Uislamu.

Swala imesisitizwa na ina umuhimu katika Uislamu kwa sababu zifuatazo;

 

Kusimamisha Swala ni Amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).

Mwenyezi Mungu (s.w) ameamrisha waumini (waislamu) wote wasimamishe swala zote za faradh na sunnah ipasavyo.

Rejea Quran (29:45), (4:103) na (14:31).

 

Kusimamisha swala ni nguzo ya Pili ya Uislamu.

Baada ya shahada mbili, nguzo ya pili na ya msingi mno katika Uislamu ni kusimamisha swala.

 

Swala humtakasa muislamu na mambo machafu na maovu.

Bila shaka swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mja na mambo machafu na maovu.

Rejea Quran (29:45).

 

Swala ni amali ya mwanzo kabisa kuhesabiwa siku ya Qiyama.

Swala ya muumini ikitengemaa vizuri ndio sababu ya kufaulu kwake Duniani na Akhera pia.

Rejea Quran (23:1-2,9), (87:14-15) na (22:34-35).

 

Kutosimamisha swala ni sababu ya mtu kuingizwa motoni.

Hii ni baada ya muislamu Kupuuza swala kwa kutozingatia sharti na nguzo zake kikamilifu na kukosa unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.

Rejea Quran (74:42-47), (68:42-43) na (107:4-5).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3024

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?

Soma Zaidi...
Maana ya talaka na kuacha ama kuachwa

Maana ya TalakaTalaka ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa waliofunga mume na mke wakati wa kufunga ndoa mbele ya mashahidi wawili.

Soma Zaidi...
Haki za kiuchumi za mwanamke katika uislamu

Haki za UchumiKuwa imara kiuchumi ni sababu mojawapo kubwa ya kumpa mtu hadhi katika jamii.

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.

Soma Zaidi...
Twahara na umuhimu wake katika uislamu

Katika post hii utajifunza maana ya twahara kiligha na kishria. Pia utajifunza umuhimu wake

Soma Zaidi...
Haki ya kumiliki mali na mipaka yake katika uislamu

Je unaijuwa mipaka yako katika kumiliki mali. Ama unajuwa haki zako katika mali inayomiliki. Endelea na somo

Soma Zaidi...
Hawa ndio wanaoruhusiwa kurithi

Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu.

Soma Zaidi...