picha

Ndoto ya Nabii Yusufu(a.s) Yatimia

Yusufu(a.

Ndoto ya Nabii Yusufu(a.s) Yatimia

Ndoto ya Nabii Yusufu(a.s) Yatimia


Yusufu(a.s.) aliwasamehe na kuwaagiza waende wakamlete baba yao mzee Yaaqub(a.s.) na wao waje wote na familia zao.




Akasema: “Hakuna lawama juu yenu leo; Mwenyezi Mungu atakusameheni, naye ni Mwenye rehema zaidi kuliko wanaorehemu. (12:92)



Nendeni na kanzu yangu hii na muiweke mbele ya uso wa baba yangu: naye atafunuka macho aone. Na nijieni pamoja na watu wenu wote(12:93)

Waliporudi nyumbani walichukuzana wote, familia nzima akiwemo baba yao, mzee Ya’aquub(a.s),wakahamia Misri.

Na walipoingia kwa Yusufu aliwakumbatia wazazi wake na akasema; “Ingieni Misri, Inshaa-Allah mumo katika amani. (12:99)



Aliwainua wazazi wake na kuwaweka katika kiti cha Ufalme. Na wote wakaporomoka kumsujudia. Na Yusufu akasema: “Ewe babangu! Hii ndiyo hakika ya ndoto yangu ya zamani. Hakika Mola wangu ameithibitisha. Na amenifanyia hisani akanitoa gerezani na akakuleteni ninyi kutoka jangwani; baada ya Shetani kuchochea baina yangu na ndugu zangu. Hakika Mola wangu ni mwenye kulifikia alitakalo. Bila shaka Yeye ni Mjuzi na Mwenye hekima.(12:100)



Shukurani za Nabii Yusufu(a.s) kwa Allah(s.w)


Yusufu(a.s)alimshukuru Mola wake kwa kuleta dua ifuaatayo:

“Ee Mola wangu! Hakika umenipa Ufalme na umenifundisha tafsiri ya mambo. Ewe Muumba wa mbingu na ardhi! Wewe ndiye Mlinzi wangu katika dunia na Akhera. Nifishe hali ya kuwa ni Muislamu na unichanganyishe na watendao mema (12:101)



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 2133

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 ai web app     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Bongolite - Game zone - Play free game     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Lengo la kushushwa vitabu vya mwenyezi Mungu (s.w)

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tawhiid

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Al-Munaafiqun

Wanapokujia wanafiki, husema: "Tunashuhudia ya kuwa kwa yakini wewe ni Mtume wa Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Mafundisho yao kutoathiriwa na mazingira ya jamii zao

Takriban Mitume wote walitokea katika jamii zilizozama katika ujahili, lakini kamwe ujumbe wao haukuathiriwa na mitazamo ya ujahili kwa ujumla, walahawakuingizautamaduni wa kijahili katika dini ya Allah (s.

Soma Zaidi...
zijue Nguzo za uislamu, imani, ihsani pamoja na dalili za qiyama

عَنْ عُمَرَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَيْضًا قَالَ: " بَيْنَمَا نَحْنُ جُلُوسٌ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ذَاتَ يَوْمٍ، إذْ ?...

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kukaribia zinaa

Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa.

Soma Zaidi...