picha

Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu

Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu)

 

Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu ni:

1. Il-hamu.


-    Ni mtiririko wa habari (ujumbe) unaomjia mwanaadamu bila kufundishwa na mtu yeyote au kuona mfano wake katika mazingira yeyote.

2. Kuongea na Mwenyezi Mungu (s.w) nyuma ya pazia.


-    Ni njia mwanaadamu huongeleshwa na Mwenyezi Mungu (s.w) moja kwa moja kwa sauti ya kawaida bila kumuona.

-    Nabii Musa (a.s) ni miongoni mwa Mitume waliosemeshwa na Allah (s.w) nyuma ya pazia.

    Rejea Qur’an (28:30), (7:143) na (19:23-26).

3. Kutumwa Malaika na kufikisha ujumbe kama alivyotumwa.


-    Ni njia anayoitumia Allah (s.w) kumuelimisha mwanaadamu kwa kupeleka ujumbe kupitia mitume na watu wengine wema.

    Rejea Qur’an (53:1-12), (15:51-66), (19:16-19), (2:102) na (3:41).

4. Ndoto za kweli (ndoto za mitume).


-    Ni kupata ujumbe kupitia ndoto za kweli hasa kwa mitume ambayo huwa ni maagizo ya Allah (s.w) kwa Mitume.

-   Mfano ndoto ya Nabii Ibrahim (a.s) juu ya kumchinja mwanae Nabii Ismail (a.s).

    Rejea Qur’an (37:102), (12:4-5), (12:100) na (48:27).

5. Njia ya Maandishi (mbao zilizoandikwa).


-    Ni njia ya mawasiliano ya Allah (s.w) na waja wake kupitia maandishi yaliyoandikwa tayari.

-    Nabii Musa aliletewa ujumbe kwa maandishi kutoka kwa Allah (s.w).

    Rejea Qur’an (7:145) na (7:154).

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Views 4885

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰2 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰3 web hosting     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰5 ai web app     πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Lengo la kuletwa mitume

Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:β€œKwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere..

Soma Zaidi...
Ni Ipi Elimu yenye manufaa

Elimu inaweza kugawanyika katika makundibmrngine mawili ambayo ni elimu yenye manufaa na elimubisiyi na manufaa

Soma Zaidi...
Elimu Yenye Manufaa

Kwenye kipengele hiki tutajifunza elimu yenye manufaa kwenye jamii na pia tutajifunza sifa za elimu yenye manufaa.

Soma Zaidi...