Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
Namna lengo la zakat linavyofikiwa.
Zakat na sadaka zinalengo la kutakasa mali na nafsi ya mtoaji na mpokeaji kama ifuatavyo;
Zakat na sadaka inavyotakasa mali ya mtoaji.
Zakat hutolewa 2.5% ya mali na kuwapa wanaostahiki, hivyo kuitakasa mali ya mtoaji kutokana na chumo la haramu na haki za watu.
Zakat na sadaka zinavyotakasa nafsi ya mtoaji.
Utoaji mali kwa wanaostahiki huitakasa nafsi ya mtoaji kutokana na ubakhili, kuabudu mali, kibri, n.k katika kumiliki mali na kuwa na upole, huruma, n.k.
Rejea Quran (61:10-12) na (9:102-103).
Zakat na sadaka inavyotakasa nafsi ya mpokeaji.
Utoaji wa zaka na sadaka kwa wanaostahiki huondoa chuki, husuda, uadui, unyonge kwa wasionacho na kuleta udugu, upendo, shukurani na ushirikiano.
Rejea Quran (9:60).
Zakat na sadakat huitakasa jamii ya waislamu.
Utoaji wa zakat na sadaka hujenga jamii yenye udugu wa kweli, kujenga uchumi wa halali na kuondoa chuki na uadui baina ya masikini na matajiri.
Rejea Quran (61:4).
Umeionaje Makala hii.. ?
(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya Twahara Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu
Soma Zaidi...Endapo mtu atamuacha mke wake kabla hata ya kukutana kimwili, basi talaka hii itahukumiwa kwa namna hii.
Soma Zaidi...Post hii itakufundisha mambo ambayo yatasababisha swqla yako isikubaliwe.
Soma Zaidi...Sharti za SwalaSharti za Swala Sharti za swala ni yale mambo ya lazima anayotakiwa Muislamu ayachunge na kuyatekeleza kabla hajaanza kuswali.
Soma Zaidi...