Swala ya jamaa.

Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa.

6.5 Kusimamisha Swala ya Jamaa

Swala ya jamaa inaanzia na watu wawili (imamu mwenyewe na maamuma moja).

  1. Kusimamisha swala ya jamaa ni amri kama aya ya Qur’an (4:102) inavyobainisha.
  2. Kusimamisha swala katika jamaa ina ubora kwa daraja 27 kuliko ya mtu peke yake.
  3. Kusimamisha swala ya jamaa hupelekea ukamilifu na ubora wa swala kwa kuepukana na vishawishi vingi ndani ya swala.
  4. Kusimamisha swala ya jamaa ina jenga umma wa waislamu na kuwa wa moja na kushikamana ipasavyo.

Zifuatazo ni miongoni mwa sababu za kutoswali jamaa msikitini kisheria;

  1. Machafuko ya hali ya hewa kama vile; mvua, baridi au jua kali sana, n.k.
  2. Wakati ukiwa na njaa na chakula kimetengwa mezani.
  3. Kushikwa (kuwa) na haja ndogo au kubwa.
  4. Kuwa mgonjwa au muuguzi.
  5. Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani kama vile; wanyama wakali, n.k.

-     Swala ya Jamaa huanza kwa watu wawili, imamu na maamuma moja.

      Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 136-141.

 

-     Imamu ni kiongozi, hivyo mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anafaa kuoza swala;

  1. Mwenye kuweza kuisoma Qur’an vizuri na kuielewa vizuri.
  2. Anayefahamu na kuelewa vizuri Hadith na Sunnah za Mtume (s.a.w).
  3. Mwenye tabia njema na siha (afya) nzuri.
  4. Mwenye umri mkubwa.

 

-   Swala ya Ijumaa ni faradh inayosimamishwa siku ya Ijumaa badala ya swala ya adhuhuri.

 

-   Si lazima kutimia idadi fulani ya waumini ili kuswihi swala ya Ijumaa, uthibitisho wa hadith ya Mtume (s.a.w) ni kuwa watu wawili, imamu na maamuma wanatosheleza kuswaliwa Ijumaa.

 

  1. Swala ya Ijumaa ni faradh (amri) ya Allah (s.w) kwa waislamu wote wanaume na wanawake wasio na udhuru wa kisheria.

Rejea Qur’an (62:9-10)

 

2.Kutoswali swala ya Ijumaa bila udhuru kisheria ni miongoni mwa sababu za kupata madhambi na kustahiki adhabu za Allah (s.w).

 

 

-     Wanaolazimika kuswali swala ya Ijumaa ni Waislamu wote wenye sifa zifuatazo;

  1. Wenye afya nzuri (wasio wagonjwa, vikongwe, vilema wasiojiweza, n.k.)
  2. Waungwana (wasio watumwa)
  3. Waliobaleghe (sio watoto)
  4. Wakazi wa mji (wasio wasafiri)
  5. Wasio katika kizuizi kama vile; mvua, n.k.

-     Swala ya Ijumaa ni faradh kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke aliye baleghe asiye na udhuru, isipokuwa wafuatao;

  1. Wanawake
  2. Watoto wadogo
  3. Vikongwe na Vilema
  4. Wagonjwa na wenye kuuguza wagonjwa
  5. Wasafiri
  6. Kuzuizi (machafuko) ya hali ya hewa kama vile; mvua, joto kali sana, n.k.
  7. Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani.

 

-     Lengo ni kuwausia, kuwatanabaisha na kuwakumbusha waislamu juu ya wajibu wao kwa Allah (s.w).

 

-     Khatibu ni sharti awe na udhu na akhutubu akiwa amesimama na kuwaelekea watu anaowakhutubia.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1869

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Je ni kwa nini lengo la finga halifikiwi kwa wafungaji

Lengo la funga ni kuwa mchamungu sasa ni kwa nini wafungaji hawalifikii lengo hili na kuwa wachamungu.

Soma Zaidi...
Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini maana ya twahara katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya twahara katika uislamu. Pia utakwenda kujifunza hukumu za twahara, aina za twahara na mambo mengineyo

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia na kupunguza zinaa katika jamii

(ii) Hatua za Kuzuia Uzinzi JamiiUislamu pamoja na kutoa mafunzo ya maadii yanayomuwezesha mtu binafsi ajiepushe kwa hiari yake na kitendo kibaya cha zinaa, umechukua hatua mbali mbali ambazo huifanya zinaa isiwe kitendo chepesi katika jamii.

Soma Zaidi...
Saumu (funga)

Nguzo za uislamu (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kusimamisha swala.

Kwenye kipengele hiki tutajifunza maana ya swala ni nin?. Na masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Aina za hijjah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...