Swala ya jamaa.
Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa.
6.5 Kusimamisha Swala ya Jamaa
Swala ya jamaa inaanzia na watu wawili (imamu mwenyewe na maamuma moja).
- Umuhimu wa Swala za Jamaa
- Kusimamisha swala ya jamaa ni amri kama aya ya Qur’an (4:102) inavyobainisha.
- Kusimamisha swala katika jamaa ina ubora kwa daraja 27 kuliko ya mtu peke yake.
- Kusimamisha swala ya jamaa hupelekea ukamilifu na ubora wa swala kwa kuepukana na vishawishi vingi ndani ya swala.
- Kusimamisha swala ya jamaa ina jenga umma wa waislamu na kuwa wa moja na kushikamana ipasavyo.
- Udhuru wa Kutoswali Jamaa Msikitini
Zifuatazo ni miongoni mwa sababu za kutoswali jamaa msikitini kisheria;
- Machafuko ya hali ya hewa kama vile; mvua, baridi au jua kali sana, n.k.
- Wakati ukiwa na njaa na chakula kimetengwa mezani.
- Kushikwa (kuwa) na haja ndogo au kubwa.
- Kuwa mgonjwa au muuguzi.
- Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani kama vile; wanyama wakali, n.k.
- Namna ya Kuswali katika Jamaa
- Swala ya Jamaa huanza kwa watu wawili, imamu na maamuma moja.
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 136-141.
- Sifa za Imamu
- Imamu ni kiongozi, hivyo mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anafaa kuoza swala;
- Mwenye kuweza kuisoma Qur’an vizuri na kuielewa vizuri.
- Anayefahamu na kuelewa vizuri Hadith na Sunnah za Mtume (s.a.w).
- Mwenye tabia njema na siha (afya) nzuri.
- Mwenye umri mkubwa.
- ​​​​​​​Swala ya Ijumaa
- Swala ya Ijumaa ni faradh inayosimamishwa siku ya Ijumaa badala ya swala ya adhuhuri.
- Si lazima kutimia idadi fulani ya waumini ili kuswihi swala ya Ijumaa, uthibitisho wa hadith ya Mtume (s.a.w) ni kuwa watu wawili, imamu na maamuma wanatosheleza kuswaliwa Ijumaa.
- Umuhimu wa Swala ya Ijumaa
- Swala ya Ijumaa ni faradh (amri) ya Allah (s.w) kwa waislamu wote wanaume na wanawake wasio na udhuru wa kisheria.
Rejea Qur’an (62:9-10)
2.Kutoswali swala ya Ijumaa bila udhuru kisheria ni miongoni mwa sababu za kupata madhambi na kustahiki adhabu za Allah (s.w).
- Wanaolazimika kuswali Swala ya Ijumaa
- Wanaolazimika kuswali swala ya Ijumaa ni Waislamu wote wenye sifa zifuatazo;
- Wenye afya nzuri (wasio wagonjwa, vikongwe, vilema wasiojiweza, n.k.)
- Waungwana (wasio watumwa)
- Waliobaleghe (sio watoto)
- Wakazi wa mji (wasio wasafiri)
- Wasio katika kizuizi kama vile; mvua, n.k.
- Wasiolazimika kuswali Swala ya Ijumaa
- Swala ya Ijumaa ni faradh kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke aliye baleghe asiye na udhuru, isipokuwa wafuatao;
- Wanawake
- Watoto wadogo
- Vikongwe na Vilema
- Wagonjwa na wenye kuuguza wagonjwa
- Wasafiri
- Kuzuizi (machafuko) ya hali ya hewa kama vile; mvua, joto kali sana, n.k.
- Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani.
- Khutuba ya Ijumaa
- Lengo ni kuwausia, kuwatanabaisha na kuwakumbusha waislamu juu ya wajibu wao kwa Allah (s.w).
- Khatibu ni sharti awe na udhu na akhutubu akiwa amesimama na kuwaelekea watu anaowakhutubia.
- Nguzo za Khutuba ya Ijumaa
- Kumshukuru Allah (s.w) kwa kusema, “Al-hamdulillaah”
- Kumtakia rehema na amani (kumswalia) Mtume (s.a.w).
- Kuwausia waislamu kumcha Allah (s.w) au mawaidha juu ya Uislamu.
- Kusoma Qur’an angalau aya moja.
- Kuwaombea waislamu dua.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Vipi funga yaani swaumu itapelekea uchamungu na kutekeleza lengo
Funga inavyomuandaa mtu kuwa mcha-Mungu.
Soma Zaidi...Nguzo za swaumu (kufinga)
Hapa utajifunza nguzo kuu za swaumu. Kama hazitatimia nguzo hizi basi swaumu itakuwa ni batili.
Soma Zaidi...Tarstibu za kulipa swaumu ya Ramadhani
Hapa utajifunza namna ambayo utatakiwa kulipa funga ya Ramadhani kwa siku ambazo hukufunga
Soma Zaidi...Namna ya kuosha maiti hatua kwa hatua
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...