Swala ya jamaa.

Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa.

6.5 Kusimamisha Swala ya Jamaa

Swala ya jamaa inaanzia na watu wawili (imamu mwenyewe na maamuma moja).

  1. Kusimamisha swala ya jamaa ni amri kama aya ya Qur’an (4:102) inavyobainisha.
  2. Kusimamisha swala katika jamaa ina ubora kwa daraja 27 kuliko ya mtu peke yake.
  3. Kusimamisha swala ya jamaa hupelekea ukamilifu na ubora wa swala kwa kuepukana na vishawishi vingi ndani ya swala.
  4. Kusimamisha swala ya jamaa ina jenga umma wa waislamu na kuwa wa moja na kushikamana ipasavyo.

Zifuatazo ni miongoni mwa sababu za kutoswali jamaa msikitini kisheria;

  1. Machafuko ya hali ya hewa kama vile; mvua, baridi au jua kali sana, n.k.
  2. Wakati ukiwa na njaa na chakula kimetengwa mezani.
  3. Kushikwa (kuwa) na haja ndogo au kubwa.
  4. Kuwa mgonjwa au muuguzi.
  5. Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani kama vile; wanyama wakali, n.k.

-     Swala ya Jamaa huanza kwa watu wawili, imamu na maamuma moja.

      Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 136-141.

 

-     Imamu ni kiongozi, hivyo mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anafaa kuoza swala;

  1. Mwenye kuweza kuisoma Qur’an vizuri na kuielewa vizuri.
  2. Anayefahamu na kuelewa vizuri Hadith na Sunnah za Mtume (s.a.w).
  3. Mwenye tabia njema na siha (afya) nzuri.
  4. Mwenye umri mkubwa.

 

-   Swala ya Ijumaa ni faradh inayosimamishwa siku ya Ijumaa badala ya swala ya adhuhuri.

 

-   Si lazima kutimia idadi fulani ya waumini ili kuswihi swala ya Ijumaa, uthibitisho wa hadith ya Mtume (s.a.w) ni kuwa watu wawili, imamu na maamuma wanatosheleza kuswaliwa Ijumaa.

 

  1. Swala ya Ijumaa ni faradh (amri) ya Allah (s.w) kwa waislamu wote wanaume na wanawake wasio na udhuru wa kisheria.

Rejea Qur’an (62:9-10)

 

2.Kutoswali swala ya Ijumaa bila udhuru kisheria ni miongoni mwa sababu za kupata madhambi na kustahiki adhabu za Allah (s.w).

 

 

-     Wanaolazimika kuswali swala ya Ijumaa ni Waislamu wote wenye sifa zifuatazo;

  1. Wenye afya nzuri (wasio wagonjwa, vikongwe, vilema wasiojiweza, n.k.)
  2. Waungwana (wasio watumwa)
  3. Waliobaleghe (sio watoto)
  4. Wakazi wa mji (wasio wasafiri)
  5. Wasio katika kizuizi kama vile; mvua, n.k.

-     Swala ya Ijumaa ni faradh kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke aliye baleghe asiye na udhuru, isipokuwa wafuatao;

  1. Wanawake
  2. Watoto wadogo
  3. Vikongwe na Vilema
  4. Wagonjwa na wenye kuuguza wagonjwa
  5. Wasafiri
  6. Kuzuizi (machafuko) ya hali ya hewa kama vile; mvua, joto kali sana, n.k.
  7. Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani.

 

-     Lengo ni kuwausia, kuwatanabaisha na kuwakumbusha waislamu juu ya wajibu wao kwa Allah (s.w).

 

-     Khatibu ni sharti awe na udhu na akhutubu akiwa amesimama na kuwaelekea watu anaowakhutubia.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2230

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 web hosting    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maana ya sadaqat

Nguzo za imani, maana ya sadaqat (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda

Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Haki za binadamu kwa ujumla (basic human rights)

Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni upi umuhimu wa kufunga katika uislamu

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kufunga kiroho, kiafya na kijamii.

Soma Zaidi...
Mambo yanayotenguwa udhu

Post hiibinakwenda kukufundisha mambo ambayo yanaharibu udhu.

Soma Zaidi...
MALI ZISIZORUHUSIWA KUTOLEWA ZAKA

*Suala la kumilikiwa binaadam (utumwa), japokuwa linaendelea kutajwa kwenye Sharia (katika vitabu), ni suala ambalo haliko.

Soma Zaidi...
namna ya kuswali 6

Lugha ya Swala Lugha ya swala,kuanzia kwenye Takbira ya kuhirimia Swala mpaka kumalizia swala kwa Salaam, ni Kiarabu.

Soma Zaidi...
Mafungu ya urithi katika uislamu

Hspa utajifunza viwango maalumu vya kutithi mirathi ys kiislamu.

Soma Zaidi...