Swala ya jamaa.
Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa.
6.5 Kusimamisha Swala ya Jamaa
Swala ya jamaa inaanzia na watu wawili (imamu mwenyewe na maamuma moja).
- Umuhimu wa Swala za Jamaa
- Kusimamisha swala ya jamaa ni amri kama aya ya Qur’an (4:102) inavyobainisha.
- Kusimamisha swala katika jamaa ina ubora kwa daraja 27 kuliko ya mtu peke yake.
- Kusimamisha swala ya jamaa hupelekea ukamilifu na ubora wa swala kwa kuepukana na vishawishi vingi ndani ya swala.
- Kusimamisha swala ya jamaa ina jenga umma wa waislamu na kuwa wa moja na kushikamana ipasavyo.
- Udhuru wa Kutoswali Jamaa Msikitini
Zifuatazo ni miongoni mwa sababu za kutoswali jamaa msikitini kisheria;
- Machafuko ya hali ya hewa kama vile; mvua, baridi au jua kali sana, n.k.
- Wakati ukiwa na njaa na chakula kimetengwa mezani.
- Kushikwa (kuwa) na haja ndogo au kubwa.
- Kuwa mgonjwa au muuguzi.
- Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani kama vile; wanyama wakali, n.k.
- Namna ya Kuswali katika Jamaa
- Swala ya Jamaa huanza kwa watu wawili, imamu na maamuma moja.
Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 136-141.
- Sifa za Imamu
- Imamu ni kiongozi, hivyo mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anafaa kuoza swala;
- Mwenye kuweza kuisoma Qur’an vizuri na kuielewa vizuri.
- Anayefahamu na kuelewa vizuri Hadith na Sunnah za Mtume (s.a.w).
- Mwenye tabia njema na siha (afya) nzuri.
- Mwenye umri mkubwa.
- ​​​​​​​Swala ya Ijumaa
- Swala ya Ijumaa ni faradh inayosimamishwa siku ya Ijumaa badala ya swala ya adhuhuri.
- Si lazima kutimia idadi fulani ya waumini ili kuswihi swala ya Ijumaa, uthibitisho wa hadith ya Mtume (s.a.w) ni kuwa watu wawili, imamu na maamuma wanatosheleza kuswaliwa Ijumaa.
- Umuhimu wa Swala ya Ijumaa
- Swala ya Ijumaa ni faradh (amri) ya Allah (s.w) kwa waislamu wote wanaume na wanawake wasio na udhuru wa kisheria.
Rejea Qur’an (62:9-10)
2.Kutoswali swala ya Ijumaa bila udhuru kisheria ni miongoni mwa sababu za kupata madhambi na kustahiki adhabu za Allah (s.w).
- Wanaolazimika kuswali Swala ya Ijumaa
- Wanaolazimika kuswali swala ya Ijumaa ni Waislamu wote wenye sifa zifuatazo;
- Wenye afya nzuri (wasio wagonjwa, vikongwe, vilema wasiojiweza, n.k.)
- Waungwana (wasio watumwa)
- Waliobaleghe (sio watoto)
- Wakazi wa mji (wasio wasafiri)
- Wasio katika kizuizi kama vile; mvua, n.k.
- Wasiolazimika kuswali Swala ya Ijumaa
- Swala ya Ijumaa ni faradh kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke aliye baleghe asiye na udhuru, isipokuwa wafuatao;
- Wanawake
- Watoto wadogo
- Vikongwe na Vilema
- Wagonjwa na wenye kuuguza wagonjwa
- Wasafiri
- Kuzuizi (machafuko) ya hali ya hewa kama vile; mvua, joto kali sana, n.k.
- Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani.
- Khutuba ya Ijumaa
- Lengo ni kuwausia, kuwatanabaisha na kuwakumbusha waislamu juu ya wajibu wao kwa Allah (s.w).
- Khatibu ni sharti awe na udhu na akhutubu akiwa amesimama na kuwaelekea watu anaowakhutubia.
- Nguzo za Khutuba ya Ijumaa
- Kumshukuru Allah (s.w) kwa kusema, “Al-hamdulillaah”
- Kumtakia rehema na amani (kumswalia) Mtume (s.a.w).
- Kuwausia waislamu kumcha Allah (s.w) au mawaidha juu ya Uislamu.
- Kusoma Qur’an angalau aya moja.
- Kuwaombea waislamu dua.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 web hosting 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Jinsi ya kutawadha kama aalivyotawadha Mtume Muhammad (s.a.w)
Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutawadha kama vile ambavyo alitawadha Mtume
Soma Zaidi...