Swala ya jamaa.

Kipengele hiki tutajifunza kusimamisha swala ya jamaa,swala za ijumaa.

6.5 Kusimamisha Swala ya Jamaa

Swala ya jamaa inaanzia na watu wawili (imamu mwenyewe na maamuma moja).

  1. Kusimamisha swala ya jamaa ni amri kama aya ya Qur’an (4:102) inavyobainisha.
  2. Kusimamisha swala katika jamaa ina ubora kwa daraja 27 kuliko ya mtu peke yake.
  3. Kusimamisha swala ya jamaa hupelekea ukamilifu na ubora wa swala kwa kuepukana na vishawishi vingi ndani ya swala.
  4. Kusimamisha swala ya jamaa ina jenga umma wa waislamu na kuwa wa moja na kushikamana ipasavyo.

Zifuatazo ni miongoni mwa sababu za kutoswali jamaa msikitini kisheria;

  1. Machafuko ya hali ya hewa kama vile; mvua, baridi au jua kali sana, n.k.
  2. Wakati ukiwa na njaa na chakula kimetengwa mezani.
  3. Kushikwa (kuwa) na haja ndogo au kubwa.
  4. Kuwa mgonjwa au muuguzi.
  5. Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani kama vile; wanyama wakali, n.k.

-     Swala ya Jamaa huanza kwa watu wawili, imamu na maamuma moja.

      Rejea EDK Kitabu cha 1, Sekondari, Uk. 136-141.

 

-     Imamu ni kiongozi, hivyo mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anafaa kuoza swala;

  1. Mwenye kuweza kuisoma Qur’an vizuri na kuielewa vizuri.
  2. Anayefahamu na kuelewa vizuri Hadith na Sunnah za Mtume (s.a.w).
  3. Mwenye tabia njema na siha (afya) nzuri.
  4. Mwenye umri mkubwa.

 

-   Swala ya Ijumaa ni faradh inayosimamishwa siku ya Ijumaa badala ya swala ya adhuhuri.

 

-   Si lazima kutimia idadi fulani ya waumini ili kuswihi swala ya Ijumaa, uthibitisho wa hadith ya Mtume (s.a.w) ni kuwa watu wawili, imamu na maamuma wanatosheleza kuswaliwa Ijumaa.

 

  1. Swala ya Ijumaa ni faradh (amri) ya Allah (s.w) kwa waislamu wote wanaume na wanawake wasio na udhuru wa kisheria.

Rejea Qur’an (62:9-10)

 

2.Kutoswali swala ya Ijumaa bila udhuru kisheria ni miongoni mwa sababu za kupata madhambi na kustahiki adhabu za Allah (s.w).

 

 

-     Wanaolazimika kuswali swala ya Ijumaa ni Waislamu wote wenye sifa zifuatazo;

  1. Wenye afya nzuri (wasio wagonjwa, vikongwe, vilema wasiojiweza, n.k.)
  2. Waungwana (wasio watumwa)
  3. Waliobaleghe (sio watoto)
  4. Wakazi wa mji (wasio wasafiri)
  5. Wasio katika kizuizi kama vile; mvua, n.k.

-     Swala ya Ijumaa ni faradh kwa kila muislamu mwanamume na mwanamke aliye baleghe asiye na udhuru, isipokuwa wafuatao;

  1. Wanawake
  2. Watoto wadogo
  3. Vikongwe na Vilema
  4. Wagonjwa na wenye kuuguza wagonjwa
  5. Wasafiri
  6. Kuzuizi (machafuko) ya hali ya hewa kama vile; mvua, joto kali sana, n.k.
  7. Kuwa na hofu ya kudhuriwa njiani.

 

-     Lengo ni kuwausia, kuwatanabaisha na kuwakumbusha waislamu juu ya wajibu wao kwa Allah (s.w).

 

-     Khatibu ni sharti awe na udhu na akhutubu akiwa amesimama na kuwaelekea watu anaowakhutubia.

 

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1706

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Ubainifu kati ya halali na Haramu na kujiepusha na mambo yanayo tatiza

عَنْ أَبِي عَبْدِ اللَّهِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، قَالَ: سَمِعْت رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَقُ?...

Soma Zaidi...
Nguzo za kufunga ramadhani

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuswali swala vitani

Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani.

Soma Zaidi...
Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu

Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu.

Soma Zaidi...
Aina mbili za talaka zisizo na rejea katika uislamu

Huwezi kuruhusiwa kumrejea mke endapo utamuacha kwa talaka hizi mbili.

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa

Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.

Soma Zaidi...