Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu
- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu
- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.k.
- Benki hurahisisha kutoa huduma ya malipo kwa watu au wafanyakazi kupitia cheque, cash au hundi, n.k.
- Benki hurahisisha mtu kupata huduma ya malipo ya kifedha katika masafa ya mbali popote ulimwenguni kupitia matawi yake.
- Benki huepusha watu kuibiwa au kutembea na fedha nyingi au vitu vya thamani kubwa mkononi.
- Benki pia zinatoa mikopo mikubwa ili kuendeleza uchumi kwa watu na nchi kwa ujumla kama sekta za viwanda, kilimo, n.k.
Benki za Kiislamu
Ni miongoni mwa taasisi za kifedha zinazotoa huduma katika msingi isiyokuwa na riba kupitia miradi au biashara zifuatazo;
i. Mudharabah
- Ni makubaliano kati ya watu wawili au zaidi ambapo mmoja hutoa mtaji na mwingine hushiriki kikamilifu kuendesha biashara au mradi.
ii. Musharakah
- Ni ushiriki kikamilifu wa watu wawili au zaidi katika kutoa mtaji na kuendesha biashara au mradi.
iii. Ijara – Uara wa Iktna
- Ni utaratibu wa kutumia fedha au mtaji kukodisha majumba, magari, mashamba, n.k. kwa ajili ya uzalishaji mali.
iv. Murabah
- Ni njia ya kununua bidhaa kwa wingi ili kuwauzia wafanyabiashara kwa
oda ya bei walioafikiana.
v. Muqaradhah
- Ni mtindo ambao mtu au benki hununua hisa “share” au “bonds” katika
kampuni za uzalishaji kwa makubaliano ya kugawana faida au hasara.
Faida ya benki za Kiislamu
- Kuokoa uchumi wa jamii kutokana na riba na madhara yake.
- Hutoa mgawo na ushirika sawa katika kusimamia na kuendesha miradi na rasilimali kati ya maskini na wamiliki (matajiri).
- Huinua uchumi wa jamii kutokana na tahadhari na umakini mkubwa unaochukuliwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 web hosting 👉3 ai web app 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Jinsi Uislamu Ulivyokomesha Biashara ya Utumwa wakati na baada ya Mtume Muhammad (s.a.w)
- Uislamu ulieneza nadharia kuwa wanaadamu wote ni sawa na wote ni watumwa mbele ya Mwenyezi Mungu (s.
Soma Zaidi...Kwa nini imefaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani
Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani.
Soma Zaidi...Hatua za kinga za ugumba na Utasa.
Ugumba ni “ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasa kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba.
Soma Zaidi...Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Assalamu Alaykum Warahmatu-llah Wabarakaatuh Naomba kuuliza: Je kama maiti imekatika baadhi ya viungo je viungo vyake tunafata utaratibu gani katika kumuosha na kumkafini?
Soma Zaidi...Misingi ya fiqh
Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu.
Soma Zaidi...