image

Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri

Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a.

Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri

Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri


Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a.s) aliendelea kwa hima kulingania Dini ya Allah(s.w) na kuuweka wazi msimamo wake kama ifuatavyo:


“Wasomee habari za Nuhu alipowaambia watu wake: Enyi watu wangu! Ikiwa kukaa kwangu na nyinyi na kukumbusha kwangu Aya za Mwenyezi Mungu kunakuchukizeni, basi mimi nategemea kwa Mwenyezi Mungu. Nanyi kusanyeni mambo yenu na hao washirika wenu. (Kusanyikeni mje kunidhuru, mimi sijali).

Tenashauri lenu hilo lisifichikane kwenu (fanyeniu kwa dhahiri; mimi sijali tu). Kisha mpitishe kwangu (hilo mnalotaka kupitisha). Wala msinipe nafasi (hata kidogo. Mimi sijali, namtegemea Mwenyezi Mungu tu).” (10:71)

Nabii Nuhu(a.s) aliendelea kuwausia watu wake na kudhihirisha msimamo wake.


“Na enyi watu wangu! Mimi sikuombeni mali juu ya (jambo) hili; sina ujira wangu ila kwa Mwenyezi Mungu; na mimi sitawafukuza walioamini (kama mnavyotaka kwangu niwafukuze hao madhaifu ndipo msilimu nyinyi watukufu. Sitafanya hivyo); maana wao watakutana na Mola wao (awalipe kwa mema yao na mabaya yao). Lakini mimi nakuoneni nyinyi ni watu mnaofanya ujinga. (Mnakataa kuifuata haki kwa kuwa imefuatwa na madhaifu)! (11:29).

Kwa ufupi tunajifunza kuwa:

• Nabii Nuhu(a.s) hakumchelea yeyote au chochote katika kulingania Dini ya Allah(s.w), bali alimtegemea Allah(s.w).
• Alilingania Dini ya Allah kwa kutarajia malipo kutoka kwake tu.
• Aliwapokea na kuwakumbatia wote waliomuamini bila ya ubaguzi wa aina yoyote.


Ushindi wa Nabii Nuhu(a.s) na Wale Walioamini Pamoja Naye.


Nabii Nuhu(a.s)alilingania Uislamu katika mazingira magumu ya upinzani mkubwa bila ya kukata tamaa kwa muda wa miaka 950.

Alipoona kuwa viongozi wa makafiri wanazidi kuweka mikakati ya kuzuia watu kusilimu kila uchao na kuwashinikiza kurudi kwenye ukafiri hata wale walioamini kwa kuwafanyia vitimbi mbalimbali, Nabii Nuhu(a.s) alilazimika kuomba msaada wa Allah(s.w) dhidi ya makafiri kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:

“Na (wakumbushe) Nuhu alipotulingania zamani (kutuomba) nasi tukamuitikia, na tukamuokoa yeye na watu wake katika shida (msiba) kubwa hiyo.(21:76)


Na tukamnusuru juu ya watu waliozikadhibisha aya zetu. Hakika wao walikuwa watu wabaya. Basi tukawatotesha (gharikisha) wote.” (21:77)

Kabla yao kama tulivyoona watu wa Nuhu walikadhibisha nao. Walimkadhibisha mja Wetu na wakasema ni mwendawazimu; na akawa anatolewa maneno makali. Ndipo akamuomba Mola wake (akasema): “Kwa hakika mimi nimeshindwa, basi ninusuru.(54:9-10)

Mara tukaifungua milango ya mbingu kwa maji yanayomiminika (kwa nguvu kabisa). Na tukazibubujisha maji chemchem zilizo katika ardhi; na maji (ya juu na chini) yakakutana kwa jambo lililokadiriwa (na Mungu).(54:11-12)


Na Tukamchukua (Nabii Nuhu) katika ile(jahazi) iliyotenge nezwa kwa mbao na misumari. Ikawa inakwenda mbele ya macho, (hifadhi) Yetu. Hii ni tunzo (tuzo) kwa yule aliyekuwa amekataliwa (amekanushwa). (54:13-14)

Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa Nabii Nuhu(a.s) pamoja na waumini wachache aliokuwa nao walipata ushindi mkubwa juu ya makafiri waliokuwa wengi na uwezo mkubwa kwa msaada wa Allah(s.w). Allah(s.w) alitumia jeshi la “maji” kuwaangamiza makafiri na akawanusuru waumini kwa jahazi. Hii inatukumbusha kuwa:

“Na majeshi ya mbingu na ardhi ni ya Mwenyezi Mungu; na
Mwenyezi Mungu ni mwenye nguvu, mwenye hikima.” (48:7)



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 372


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)
(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s. Soma Zaidi...

NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua. Soma Zaidi...

Historia ya Al-Khidhri
Jina Al-Khidhri halikutajwa mahali popote katika Qur’an. Soma Zaidi...

tarekh 09
KULELEWA NA BABU YAKE:Mzee ‘Abdul Al-Muttalib alimchukuwa mjukuu wake na wakarejea Makkah na aliendelea kuishinae na kumlea kwa mapenzi makubwa sana. Soma Zaidi...

Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7 Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME ZAKARIA(A.S) NA YAHYA(A.S)
Zakaria(a. Soma Zaidi...

tarekh 3
KUCHIMBWA UPYA KISIMA CHA ZAMZAMKwa kifupi ni kuwa Abdul-Muttalib alipata agizo kutoka ndotoni kuwa achimbe kisima cha zamzam, na akaelekezwa sehemu ya kupachimba. Soma Zaidi...

Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud
Vita vya Uhudi. Soma Zaidi...

MTUME(S.A.W) KULINGANIA UISLAMU MAKKA
Historia ya harakati za Mtume(s. Soma Zaidi...

Mbinu Alizozitumia Nabii Shu’ayb(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe Wake
Soma Zaidi...

Kufunguliwa Yusufu(a.s) Kutoka Gerezani
Yusufu(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUZALIWA KWA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) NA MAMA AMINA MKE WA ABDALLAH MTOTO WA ABDUL-AL MUTALIB
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...