Malaika ni nani?
Malaika ni katika waja na viumbe wa Allah(SW) walioumbwa kutokana na nuru. Tunafahamishwa katika hadithi ifuatayo kuwa:
Aysha (r.a.) amesimulia kuwa Mtume (s.a.w.) amesema: Malaika wameumbwa na nuru na majini wameumbwa kutokana na ndimi za moto na Adamu ameumbwa kwa udongo kama ilivyoelezwa kwenu (katika Qur’an). (Muslim)Na katika Qur’an tukufu, Allah(SW) anatubainishia kuwa, katika maumbile yao halisi, malaika ni viumbe wenye mbawa.
“Sifa zote njema ni za Allah, Muumba wa mbingu na ardhi. Aliyewafanya malaika kuwa wajumbe wenye mbawa mbili-mbili, na tatu tatu, na nne nne. Huzid is ha katika kuumba apendavyo. Bila shaka ni mwenye uweza juu ya kila kitu”. (35:1)
Je malaika wanaishi wapi?Katika Qur,an tunafahamishwa kuwa Malaika wanayo makazi maalumu lakini si hapa duniani. Allah(SW) anawanukuu malaika wakisema:Hakuna yoyote miongoni mwetu ila anapo mahali pake mahususi. Na kwa yakini katika sisi wapo wajipangao safu. Na wako katika sisi wamtukuzao(Mwenyezi Mungu)(3 7:1 64-1 66)
Kutokana na kazi zao, Malaika wengi tunaishi nao humu hum u duniani na wako nasi muda wote.Kila mtu ana malaika wawili wenye kuandika amali zake.
Hakika juu yenu kuna wenye kuwatunza, malaika watukufu wenye kuandika. Wanayajua yote mnayoyatenda(82:1 0-12)
Aidha, tunafahamishwa katika Qur,an kuwa kila mmoja wetu ana kundi la malaika mbele na nyuma yake.Ana (kila mtu) kundi (la malaika) mbele yake na nyuma yake. Wanam linda kw a amri ya Mw enyezi Mungu. (13 :11)
Kwanini hatuwaoni Malaika?
Pengine mtu aweza akauliza kuwa kama tumezungukwa na malaika mbele na nyuma, kulia na kushoto, kwanini basi hatuwaoni? Jibu ni kwamba, mwanadamu yupo kwenye mtihani. Mtihani wenyewe ni kufanya mema kwa kutaraji malipo ya Allah(SW) na kuacha maovu kwa kuogopa adhabu zake.
Ametukuka yule ambaye Mkononi mwake umo ufalme(w ote); naye ni mwenye uw eza juu ya kila kitu. Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni; ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye msamaha(67:1-2)Malaika ndio wasimamizi wa mtihani huu, na wamefanywa wasionekane machoni petu ili kila mtu atumie uhuru wake wa ama kumuogopa Allah(SW) kwa kutenda mema au kumkufuru Allah(SW) kwa kumuasi. Lau malaika wangelionekana, watu wengi wangelitenda mema kinafiki(ria) badala ya kufanya kwa ikhilaswi.
Mfano wake, ingekuwa kama vile watu wenye dhamira za kufanya uhalifu wanavyojidai watu wema pale wanapokuwepo askari waliovalia rasmi. Utendaji kazi wa malaika ni kama mashushushu au askari kanzu. Mtu muovu anapanga na kutenda maovu akidhani yupo peke yake, kumbe malaika wapo wanaandika. Na ndiyo maana muovu atakapoona kila jambo lake limerikodiwa, atashangaa siku ya kiama kuwa alijulikanaje?
Na madaftari yatawekwa mbele yao. Utawaona wabaya wanayaogopa kwasababu ya yale yaliyomo; na watasema: “Ole wetu! Namna gani madaftari haya! Ha lia ch i dogo w ala ku bw a ila yam e lidh ib iti.Na watakuta yote yale w aliyoyafanya yamehudhuria hapo; na Mola wako hamdhulumu yeyote(18:49)
Siku mtu atakapowaona malaikaKuna siku na muda maalumu ambapo kila mtu binafsi ataanza kuwaona malaika katika umbile lao halisi.
(a) Siku ya kukata roho
Hii ni siku na saa ambayo dakika chache baada ya hapo mtu hukata roho na kuiaga dunia. Kwa watu wema, watakuja malaika wa kuwaliwaza: Hao huwateremkia Malaika “msigope wala msihuzunike, na furahini kwa pepo mliyokuwa mkia hid iwa. Sisi ni vipenzi vyenu katika maisha ya
dunia na (huku) katika Akhera ”.(41 :30-32)
Watu wanaotenda maovu watapata mshituko mkubwa na kujawa na huzuni kubwa mno pale watakapowaona Malaika. Watasikitika sana kwa jinsi walivyokuwa wakijidanganya nafsi zao, wakatenda maovu kwa kudhania kuwa hakuna Malaika wanaorekodi matendo yao waliyokuwa wakiyafanya hadharani na mafichoni. Watafadhaika na kusema:
....Mola wangu! Nirudishe(duniani). Ili nifanye mema sasa badala ya yale niliyoyaacha. (Malaika watamwambia): “Hapana! Hakika hili ni neno tu analosema yeye(mtu muovu)....(23:99-100)
(b) Siku ya kiyama
Kuanzia pale mtu anapowaona malaika hakutakuwa tena na kizuizi cha kutowaona kama ilivyokuwa hapa duniani. Kuonekana Malaika siku ya kiama itakuwa ni ishara mbaya kwa watu waovu kuwa umeshafika wakati wa wao kuhukumiwa naAllah(s.w) na kuanza kutumikia adhabu za kudumu katika Moto wa Jahannam. Qur’an inatufahamisha kuwa:
Siku w atakayow aona Malaika haitakuw a furaha siku hiyo kwa wenye makosa; na watasema:“(Mungu) atuepushie mbali adhabu hii iliyotukabili(lakini haitawafaa kitu dua hiyo)(25:22)
(c) Motoni na Peponi
Malaika watahudhuria katika uwanja wa hukumu siku ya Kiyama. Kila mtu atawaona wamejipanga safu wakisubiri amri ya Mwenyezi Mungu.Siku ambayo zitasimama Roho na Malaika safu safu; hatasema siku hiyo ila yule ambaye(Allah) Mwingi wa rehema amempa idhini, na atasema yaliyo sawa(78:38)
Wakipewa amri na Allah(s.w) malaika watawakamata waovu na kuwachungachunga kuelekea motoni kuadhibiwa.
Na waliokufuru watapelekwa katika Jahannam m akundi m akundi mpaka w atakapoifikia; itafunguliw a milango yake; w alinzi w ake(malaika) w ataw aambia: Je! haw akukujieni Mitum e m iongoni mw enu w akikusom eeni aya za Mola w enu na kukuonyeni juu ya makutano ya siku yenu hii(39: 71)
Watu wema watasindikizwa na malaika mpaka kwenye pep o tukufu, na malaika wa huko watawakaribisha.
Na w alinzi wake (mala ika) watawaambia: Amani juu yenu, furahini, na ingieni humu mkae milele(39:73)
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tawhid Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1446
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani
👉2 Simulizi za Hadithi Audio
👉3 Kitau cha Fiqh
👉4 Kitabu cha Afya
👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6 kitabu cha Simulizi
Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.
Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s. Soma Zaidi...
ALAMA YA MUUMINI WA UKWELI KATIKA UISLAMU
عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "مَنْ كَانَ يُؤْمِنُ بِاَللَّهِ وَالْيَوْمِ... Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu
Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu. Soma Zaidi...
Kwa namna gani nabii Musa na Bi Mariam waliweza kuzungumza na Allah nyuma ya pazia
Nabii Musa na Mama yake nabii Isa bi Mariam waliweza kuwasiliana na Allah nyuma ya pazia. Soma Zaidi...
jamii muongozo
Haja ya Mwongozo kutoka kwa Allah (s. Soma Zaidi...
Sifa za Allah Mwenyezi Mungu
Soma Zaidi...
Dalili Kubwa za kukaribia Siku ya kiama
Soma Zaidi...
Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu) Soma Zaidi...
Njia anazotumia Mwenyezi Mungu (s.w) kuwafundisha na kuwasiliana na wanaadamu
Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu) Soma Zaidi...
Kutowatii Wazazi katika kumuasi Allah (s.w)
"Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii; lakini kaa nao kwa wema hapa duniani (Maadamu ni wazee wako, ila usiwafuate tu mwenendo wao mbaya); Shika mwenendo wa wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu Soma Zaidi...
Kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila dini?
Mwanadamu hawezi kuishi bila dini, kwani dini imekusanya mfumo mzima wa maisha yake. Soma Zaidi...
(c)Vipawa vya Mwanaadamu
Vipawa vya mwanaadamu ni sababu nyingine inayomfanya mwanaadamu asiweze kuishi bila ya kufuata dini moja au nyingine. Soma Zaidi...