image

Kitabu cha Afya 03

Yajuwe mambo yanayoathiri afya ya miili yetu, jifunze mambo mengi kuhusu afya.

Kitabu cha Afya 03

DARASA LA AFYA

SEHEMU YA TATU
YANAYOATHIRI AFYA (sehemu ya kwanza)

YANAYOATHIRI AFYA
Afya yamtu inaweza kuathiriwa kuwa njema au kuwa mbovu kwa kuzingatia mambo kadhaa wakadhaa. Hapa nimechagua mambo makuu matano ambayo nitakwenda kuyaangalia ambayo ni;-
A).vyakula
B)Mazingira
C)Shughuli za kila siku
D)Tabia na mazoea
E)Vizazi, familia ama kurithi.

1.VYAKULA
Vyakula ni katika sababu kubwa ambazo husaidia kwa kiwango kikubwa kuathiri afya za watu. Wataalamu wa afya leo wanaeleza na kutaja magonjwa mengi sana ambayoyo yanapatikana kwa kupitia vyakula. Pia yapo magonjwa ambayo huambukizwa kwa kupitia ulaji wa chakula. Hivyo magonjwa mengi na hatari zaidi yamekuwa na mahusiano na vyakula vyetu. Chakula kinaweza kuwa msaada kwako au kuwa ni chanzo cha matatizo ya afya yako.

Mfano mzuri ni kuwa leo wataalamu wa afya anaeleza kuwa mamilioni ya watu wanakufa kwa ugonjwa wa saratani kila mwaka. Tafiti zinaonesha kuwa miongoni mwa sababu za ugonjwa huu ni vyakula. Vyakula ambavyo tunavila leo sio rafiki kwa afya zetu. Tumekuwa tukila vyakula ambavyo vimejaa kemikali nyingi na matatizo kadha wakadha.

Mfano wa pili ni ugonjwa wa kisukari, huu ugonjwa umekuwa ukienea kwa kasi sana duniani leo. Kuanzia watoto, vijana wazee na wajawazito wote wapo hatarini kuapata maradhi haya. Wataalamu wa afya wanataja kuwa vyakula ni katika sababu mjawapo ya kupata maradhi haya. Kuongezeka kwa uzito nje ya uzito wa kawaidi ni katika sababu za kutokea kwa kisukari. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa vyakula ni sababu ya kuongezeka kwa uzito mwilini na kutofanya mazoezi ijapokuwa zipo sababu zingine.

Magonjwa ya moyo kama shinikizo la damu (presha) pamoja na shambulio la moyo (heart attack) ni katika magonjwa yanayowapata watu weng duniani na kusababisha vifo vingi sana. Wataalamu wa afya wanaeleza katika sababu kubwa za kutokea kwa maradhi haya ni vyakula. Hususan vyakula vyenye mchanganyiko mkubwa wa mafuta ya viwandani.

Maradhi ya utapiamlo kama matege, baadhi ya matatizo ya macho, unyafuzi na kwashiakoo pamoja na kudumaa ni katika maradhi ambayo husababishwa na vyakula. Majeraha kutokupona haraka, kuchelewa kupona kwa vidonda na makovu, ngozi kupasuka na kutokwa na vidonda kwenye mdomo ni katika baadhi ya matatizo yanayosababishwa na vyakula

Kwa ufupi ni kuwa vyakula ni katika sababu kubwa sana ya maradhia mabayo tuanayapata. Tutazungumzia kwa undani zaidi somo hili kwenye kurasa zijazo na tutaona kwa undani vipi vyakula vinaweza kusababisha yote hayo.

2.MAZINGIA
Mazingira yamekuwa leo ni sababu ya kupata maradhi mengi sana. Maradhi mengi yanayotupata kutokana na mazingira yetu yanaweza kusababishwa na uchafu wa mazingira. Ijapokuwa mazingira yanaweza kuwa safi na pia yakasababisha maradhi. Mazingira pia yanaweza kuwa msaada kwetu kwa kuweza kulinda na kuimarisha afya zetu. Ila kwa ufupi hapa tutazungumzia tuu mazingira yanavyoathizi afya zetu kuwa dhoofu.

Mfano mzuri ni maradhi ya malaria ambayo leo yamekuwa yakipelekea mamilioni ya vifo duniani hususani watoto waliopo chini ya umri wa miaka mitano. Malaria yanaenezwa na mbu aina ya anofelesi na mbu huyu ni jike. Mbu hawa wanazaliana sehemu zenye majimaji. Mbu hawa hawahitaji maji mengi sana, hapana hata tone moja linamtosha yeye kutaga na kutoa watoto. Mbu hawa wamekuwa wakipatikana kwenye mazingira yetu. Wataalamu wa afya wanaeleza usafi wa mazingira kama kufyeka nyasi na kufukia madimbwi ni katika njia za kupambana na maradhi haya.

Mfano mwingine ni m aradhi ya kipindupindu, haya yamekuwa yakisababishwa na bakteria ambao wanaingia mwilini kwa njia ya chakula. Mazingira yanaweza kuwa njia ya kuenezxa maradhi haya kama usafi wa mazingira hautazingatiwa. Nzi wanaweza kubeba vijidudu vya maradhi na kuvipeleka kwingine katika mazingira yasiyokuwa safi.

Maradhi ya mafua yamekuwa ji kawaida sana kwa nchi zilizopo kwenye tropic. Maradhi yaya yanaweza kupatikana sana kwenye mazingira yenye vumbi sana. Pia kupitia hewa kutoka mgonjwa kwenda mtu mzima. Hivyo tunaweza sema mafua yanaenezwa sana kwenye mazingira kupitia hewa.

Wataalamu wa afya wanaeleza maradhi mengi sana ambayo hupatikana kwenye mazingira yetu yakila siku. Mazingira haya yanaweza kuwa kwenye maji kama maradh ya kichocho, kwenye hewa kama kifua kikuu na mafua au mazingira ya chini kama vile maradhi ya kipindupindu.

3.SHUGHULI ZA KILA SIKU
HAlikadhalika shughuli zetu za kila siku zinaweza kuwa sababu mojawapo ya kupata maradhi mablimbali za kutafutia riziki zinaweza kuwa sababu tosha ya kupata maradhi. Wataalamu wanaeleza maradhi kazaa ambayo yanaweza kuwa chanzo chake ni shughuli zetu za kila siku.

Vifaa vya kufanyia kazi kama visipotumika ipasavyo kwa mfano kuvaa viatu maalumu na nguo maalumi kwa ambao wanafanya kazi viwanda vya kemikali, wanaweza kupata madhara. Wafanyaji kazi sehemu zenye mionzi hatari kama x-ray wasipovaa mavazi maalumu kwa utaratibu husikwa wanaweza kuapata madhara.

Muda wa kufanya kazi usipizingatiwa pia madhara yanaweza kuapatikana. Kwa mfano sehemu zenye mionzi mikali kama x-ray kuna muda maalumu wa kufanya kazi na ukipita anatakiwa aingie mtu mpya. Hivyo jkazi kama hizi muda usipizingatiwa madhara ya kiafya yanaweza kutokea.

Halikadhalika teknolojia inayotumika kufanyika kazi kama haitakuwa katika hali nzuri inaweza kusababisha madhara. Vifaa vya kisasa vinatakiwa vitumike zaidi kwa ajili ya usalama kuliko kuendelea na vile vya zamani vinavyohitaji nguvu nyingi na kufanya kazi mazingira ya hatari.
v Hivyo shughuli zetu za kufanyia kazi zsipowekwa katika hali nzuri zinaweza kuwa ni sababu ya sisi kuapata madhara makubwa kama kupiteza mali, kupoteza uhai au kupoteza viungo vya miili yetu. Somo hili tutaliona kwa undani zaidi kwnye kurasa zijazo.



         › WhatsApp ‹ Whatsapp





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 285


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

darasa la lishe
Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe Soma Zaidi...

AINA ZA VYAKULA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Jinsi ya kuepuka magonjwa ya figo
Figo ni moja katika orgn zenye umuhimu sana mwilini na endapo itaatirika kwa namna yeyote ile, madhara makubwa kwenye mwili yanaweza kutokea na hata kifo. Katika post hii utajifunza jinsi ya kulinda mwili wako dhidi ya matatizo ya figo Soma Zaidi...

DALILI ZA KUTOKA AU KUHARIBIKA KWA MIMBA
Tafiti zinaonesha kuwa karibia asilimia 10% mpaka 25% ya wanawake wanaopata ujauzito, mimba zao hutoka. Soma Zaidi...

Umoja wa mataifa unazungumziaje afya
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo ya kiafya yanayozungumzwa na umoja wa mataifa Soma Zaidi...

MAZINGIRA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

KITABU CHA MATUNDA
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...

dondoo 100 za Afya
Basi tambua haya;- 61. Soma Zaidi...

Umuhimu wa kuvaa nguo za upasuaji.
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa nguo za upasuaji, tunajua wazi kuwa, wakati wa upasuaji tunapaswa kusafisha chumba na mazingira yake lengo ni kuhakikisha kuwa tunazuia wadudu wasisambae au kuingia kwenye mwili wa binadamu. Soma Zaidi...

AFYA NA MAGONJWA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

MAZINGIRZ
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

kitabu cha matunda
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...