VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE

6.VIDONDA VYA TUMBO
Ni vidonda vinavyotokea katika ukuta wa tumbo. Vidonda hivi tumezoea kuviita vidonda vya tumbo ila hapa nitataja kitaalamu kuwa vidonda hivi hufahamika kama peptic ulcers. Vidonda hivi hutokea kutokana na mashambulizi ya bakteria wanaoitwa H.pylori au kulika kwa ukuta wa tumbo kutokanana na athari za tindikali zilizopo tumboni (stomach acids) kama vile tindikali ya hydrocloric yaani hydrocloric acid. Kwa wakati tulio nao hili ni tatizo la kawaida maana limewapata watu wengi na halisabababishi vifo vya watu wengi kama maaradhi ya saratani na kisukari.

Vidonda hivi vimegawanyika katika makundi makuu matatu ambayo ni:-
1.gastric ulcers hivi hutokea ndani ya tumbo la chakula
2.Esophageal ulcers hivi hutokea ndani ya esophagus. Hii ni sehemu inayounganisha kati ya koo la chakula na tumbo la chakula.
3.Duodenal ulcers hivi hutokea kwenye sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayoitwa duodenum

Sababu za kutokea vidonda hivi
1.mashambulizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori (H.pylori). Hawa bakteria wanaweza kusabababisha mashambulizi na kuathiri sehemu tajwa hapo juuu na kusababisha vidonda hivi.
2.Matumizi ya baadhi ya aina za madawa mara kwa mara. Kuna aina za dawa ambazo kwa sasa zimepigiwa marufuku lakini hutumika kwa njia za panya. Madawa haya huweza kusababisha vidonda hivi kwa mfano aspirin, ibuprofen na naproxene n.k
3.Uvutaji wa sigara
4.Kunywa pombe kupita kiasi
5.Athari ya miozi
6.Saratani ya tumbo
7.Misongo ya mawazo (stress)
8.Kukaa na njaa kwa muda mrefu.

DALILI ZA VIDONDA HIVI.
Dalili hizi hutofautiana kulingana na aina za vidonda. Ila hapa nitaorodhesha baadhi ambazo ni kawaida kwa vidonda hivi.
1.maumivu ya tumbo kutokea kitomvuni mpaka kifuani
2.Kukosa hamu ya kula
3.Kutoka na damu na kupata choo cheusi sana
4.Kupungua uzito bila sababu
5.Kutapika
6.Maumivu ya kifua
7.Tumbo kujaa.
8.Kuchoka ana

KUTHIBITI VIDONDA HIVI
1.wacha au punguza kunywa pombe
2.Usichanganye vilevi na madawa mengine
3.Punguza kutumia madawa aina ya aspirin n.k
4.Osha mikono yako mara kwa mara kuepuka maambukizi ya bakteria
5.Punguza misongo ya mawazo
6.Kula katika muda uleule.

Vidonda vya tumbo vinatibika bila ya shaka. Mgonjwa amuone mtaalamu wa afya na atimize masharti na ale dozi kulingana na kipimo husika. Pia kama sehemu imeharibika sana mgonjwa anaweza kufanyiwa upasuaji. Kwa ambaye aansumbuliwa na vidonda hivi anashauriwa pia anywe maziwa.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Jiunge nasi WhatsApp
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 664

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA

Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles.

Soma Zaidi...
dondoo 100 za Afya

Basi tambua haya;- 61.

Soma Zaidi...
AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuepuka magonjwa ya figo

Figo ni moja katika orgn zenye umuhimu sana mwilini na endapo itaatirika kwa namna yeyote ile, madhara makubwa kwenye mwili yanaweza kutokea na hata kifo. Katika post hii utajifunza jinsi ya kulinda mwili wako dhidi ya matatizo ya figo

Soma Zaidi...
MAZINGIRA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kupiga push up kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupiga push up kiafya, ni mambo au faida zipatikanazo ki afya kwa wapigaji wa push up kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
kitabu cha afya

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
hathari zitokanazo na uvutaji wa sigara ,pombe na madawa ya kulevya na mbinu za kujikinga nayo

Posti hii inahusu zaidi utumiaji wa pombe na sigara pamoja na madawa katika jamii.

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...