VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE

VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Download Post hii hapa

VIJUE VIDONDA VYA TUMBO, SABABU ZAKE NA DALILI ZAKE

6.VIDONDA VYA TUMBO
Ni vidonda vinavyotokea katika ukuta wa tumbo. Vidonda hivi tumezoea kuviita vidonda vya tumbo ila hapa nitataja kitaalamu kuwa vidonda hivi hufahamika kama peptic ulcers. Vidonda hivi hutokea kutokana na mashambulizi ya bakteria wanaoitwa H.pylori au kulika kwa ukuta wa tumbo kutokanana na athari za tindikali zilizopo tumboni (stomach acids) kama vile tindikali ya hydrocloric yaani hydrocloric acid. Kwa wakati tulio nao hili ni tatizo la kawaida maana limewapata watu wengi na halisabababishi vifo vya watu wengi kama maaradhi ya saratani na kisukari.

Vidonda hivi vimegawanyika katika makundi makuu matatu ambayo ni:-
1.gastric ulcers hivi hutokea ndani ya tumbo la chakula
2.Esophageal ulcers hivi hutokea ndani ya esophagus. Hii ni sehemu inayounganisha kati ya koo la chakula na tumbo la chakula.
3.Duodenal ulcers hivi hutokea kwenye sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayoitwa duodenum

Sababu za kutokea vidonda hivi
1.mashambulizi ya bakteria aina ya Helicobacter pylori (H.pylori). Hawa bakteria wanaweza kusabababisha mashambulizi na kuathiri sehemu tajwa hapo juuu na kusababisha vidonda hivi.
2.Matumizi ya baadhi ya aina za madawa mara kwa mara. Kuna aina za dawa ambazo kwa sasa zimepigiwa marufuku lakini hutumika kwa njia za panya. Madawa haya huweza kusababisha vidonda hivi kwa mfano aspirin, ibuprofen na naproxene n.k
3.Uvutaji wa sigara
4.Kunywa pombe kupita kiasi
5.Athari ya miozi
6.Saratani ya tumbo
7.Misongo ya mawazo (stress)
8.Kukaa na njaa kwa muda mrefu.

DALILI ZA VIDONDA HIVI.
Dalili hizi hutofautiana kulingana na aina za vidonda. Ila hapa nitaorodhesha baadhi ambazo ni kawaida kwa vidonda hivi.
1.maumivu ya tumbo kutokea kitomvuni mpaka kifuani
2.Kukosa hamu ya kula
3.Kutoka na damu na kupata choo cheusi sana
4.Kupungua uzito bila sababu
5.Kutapika
6.Maumivu ya kifua
7.Tumbo kujaa.
8.Kuchoka ana

KUTHIBITI VIDONDA HIVI
1.wacha au punguza kunywa pombe
2.Usichanganye vilevi na madawa mengine
3.Punguza kutumia madawa aina ya aspirin n.k
4.Osha mikono yako mara kwa mara kuepuka maambukizi ya bakteria
5.Punguza misongo ya mawazo
6.Kula katika muda uleule.

Vidonda vya tumbo vinatibika bila ya shaka. Mgonjwa amuone mtaalamu wa afya na atimize masharti na ale dozi kulingana na kipimo husika. Pia kama sehemu imeharibika sana mgonjwa anaweza kufanyiwa upasuaji. Kwa ambaye aansumbuliwa na vidonda hivi anashauriwa pia anywe maziwa.


                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Afya File: Download PDF Views 398

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

YANAYOATHIRI AFYA KATIKA VYAKULA
YANAYOATHIRI AFYA KATIKA VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
MAZINGIRA
MAZINGIRA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
ITAMBUE SARATANI CHANZO CHAKE, DALILI NA KUKABILIANA NAYO
ITAMBUE SARATANI CHANZO CHAKE, DALILI NA KUKABILIANA NAYO

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumsaidia Mtoto mdogo aliyekabwa na kitu kooni
Jinsi ya kumsaidia Mtoto mdogo aliyekabwa na kitu kooni

Mfano wa kitu kinachoweza kumaba mtoto kooni ni kama chagula kigumu, pesa ya sarafu, kijiwe na mengineyo. Endapo hili litataokea msaada wa haraka unahitajika kwa ulazima.

Soma Zaidi...
Fahamu mtindo mzuri wa maisha
Fahamu mtindo mzuri wa maisha

Postei hizi inahusu zaidi mtindo mzuri wa maisha, yaani mtu ale ki vipi au afanyeni nini ili kuweza kuboresha afya yake.

Soma Zaidi...
KITABU CHA MATUNDA
KITABU CHA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
darasa la lishe
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
madhara ya tezi dume
madhara ya tezi dume

Endapo tezi dume haitatibiwa ama itachlewa kutibiwa basi mtu anaweza kupata madhara. katika post hii utakwenda kuyajuwa madhara ya tezi dume kwenye Mwili

Soma Zaidi...