image

ITAMBUE SARATANI CHANZO CHAKE, DALILI NA KUKABILIANA NAYO

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

ITAMBUE SARATANI CHANZO CHAKE, DALILI NA KUKABILIANA NAYO

2.SARATANI (CANCER)
Saratani ni ugonjwa unaotokana na kukuwa kwa seli ndani ya mwili bila ya mpangilio maalumu. Kukuwa huku kunashindwa kuthibitika ndani ya mwili. Seli hizi hukuwa na kusababisha kitu kinachoitwa kitaalamu tumor. Hii ni mkusanyiko wa hizi seli ambazo zimekuwa bila ya mpangilio maalumu ndani ya mwili. Hizi tumor husababisha kutokea kwa malignant tumor na hii ni mkusanyiko mkubwa wa hizi seli ambao huuwa seli nyingine za mwili na tishu. Hutokea wakati mwingine huu mkusanyiko ukawepo ila ukawa hauna madhara kwa seli nyingine, huu utaitwa benign tumor ila zikikuwa zaidi huweza kuathiri tishu za mwili. Hizi tumor zinaweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kuenea sehemu zingine za mwili.

Seli za saratani ni hatari zaidi kwani zinaweza kuharibu tishu na viungo vingine vya mwili kama ubongo na maini. Kiti hatari zaidi kwenye seli hizi ni kuwa zinaweza kuhama sehemu moja ya mwili kwenda sehemu nyingine. Kwa mfano saratani ya maini inaweza kuenea kwenye ubongo na kusababisha saratani ya ubongo. Saratani ya matiti na korodani inaweza kuenea kwenye mifupa na kusababisha saratani ya mifupa.

Hali hii hufanya seli hizi ziwe hatari zaidi. Mchakato huu wa kuhama sehemu moja kwenda nyingine huitwa kitaalamu metastasisi.

Seli ya saratani ya kwanza hutokea pale gene zinapopata hitilafu. Gene ni chembechembe ambazo huhusika katika kutengenezwa kwa selimmpya. Mtu anaweza kurithi gene hizi ambazo zimeharibiwa toka kuzaliwa ama akawa anazo zimeharibiwa kwa sababi zingine. Ila mtu huyu aliyerithi gene ambazo zina hitilafu ni rahisi kwake kupata saratani zaidi kuliko huyu ambaye hajarithi. Kama tulivyoona juu kule kuna mawakala wa kueneza maradhi, hali kama hii kuna mawakala wa kusababisha saratani ambao huitwa carcinogens hawa pia huhusika katika kutia hitilafu kwenye genes. Mifano ya mawakala hawa (carcinogens ) ni ;-
1.Aina flani ya virusi kama vile papilloma virus (HPV)
2.Mionzi kama radio na ulteraviolent (UV) na mionzi mingineyo.
3.Kemikali zinazopatikana kwenye tumbaku kama arsenic, benzene na formaldehyde
4.Asbestos haya ni malighafi zinazotumika kutengezea vifaa vya umeme na vifaa vingine vya nyumba kama vya kuzuia moto.

Ni vigumu sana kuepukana na mawakala hawa kwenye maisha, kwani huweza kupatokana kwwenye vyakula vyetu, shuhuli zetukwenye maji na hewa. Ila tutakujaona kwamba unaweza kujiepusha na hatari za saratani kwani karibia mawakala walotajwa hapo juu hueneza saratani ila kwa uchache ila tumbaku ni kwa kiasi kikubwa sana.

Unaweza ukagunduwa saratani kwa kutumia vifaa vya kitaalamu kama MRI, x-rays, biospy, na DNA test. Pia unaweza ukajijua mwenyewe kama una tumor kwa kujishika sehemu husika na kuona kama kuna uvimbe wowote usio wa kawaida. Pia ijulikane kuwa zipo tiba za saratani ijapokuwa kuimaliza kabisa mwilini ni kazi mzito ila ukweli ni kuwa karibia aina zote za saratani zinaweza kutibiwa kama mtu atawahi kwa haraka.baadhi ya njia wanazotumia kupambana na saratani ni kama
A)kufanyiwa upasuaji, hufanyika kwa ufasaha zaidi kama saratani haijaenea zaidi
B)Kufanya chemotherapy ni matumizi ya dawa kwa ajili ya kuuwa seli za saratani, ila kwa bahati mbaya njia hii pia huuwa seli nyingine za mwili
C)Radiation therapy ni kutumia mionzi kwa ajili ya kuuwa seli za saratani

NJIA ZA KUPAMBANA NA SARATANI
1.Wacha kuvuta. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa kuna kemikali nyingi kwenye tumbaku ambazo ni hatari.
2.Wacha kunywa pombe
3.Kula mboga za majani kwa wingi na punguza kula mafuta, kula matunda kwa wingi hii husaidia kupunguza hatari ya kupata saratani
4.Fanya mazoezi na udhibiti afya yako 5.Linda ngozi yako


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 152


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

MZUNGURUKO WA DAMU
6. Soma Zaidi...

Umuhimu wa kupiga push up kiafya
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupiga push up kiafya, ni mambo au faida zipatikanazo ki afya kwa wapigaji wa push up kama ifuatavyo. Soma Zaidi...

madhara ya tezi dume
Endapo tezi dume haitatibiwa ama itachlewa kutibiwa basi mtu anaweza kupata madhara. katika post hii utakwenda kuyajuwa madhara ya tezi dume kwenye Mwili Soma Zaidi...

kitabu cha matunda
Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho Soma Zaidi...

utaratibu wa lishe
Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe Soma Zaidi...

JIFUNZE NAMNA YA KUKABILIANA NA UGONJWA WA MAFUA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

NAMNA AMBAZO MWILI HUPAMBANA NA MARADHI
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

UGONJWA WA MALARIA NA TAKWIMU ZA ATHARI YAKE KIDUNIA
Malaria ni katika maradhi ambayo husambazwa na na mbu jike aina ya anopheles. Soma Zaidi...

MARADHI YASABABISHWAYO NA HALI ZA MAISHA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

Kitabu cha Afya 02
Kama tulivyosema hapo juu kuwa afya ni kuwa mzima kimwili na kiakili. Soma Zaidi...

dondoo 100 za Afya
Basi tambua haya;- 61. Soma Zaidi...

NYANJA ZA AFYA
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...