Ijue rangi ya mkojo isiyo ya kawaida

Ijue rangi ya mkojo isiyo ya kawaida

Post hii inahusu zaidi rangi isiyo ya kawaida kwenye mkojo, kawaida mkojo huwa na rangi ya kahawia Ila ukiona rangi zifuatazo Kuna shida kwenye mkojo.

Rangi ya mkojo isiyo ya kawaida.

1. Mkojo ambao una damu ndani yake, hii ni rangi ambayo siyo ya kawaida kwenye mkojo, hali hii utokea ambapo mkojo uwa na rangi nyekundu ambayo hapaswi kuwa rangi ya mkojo.

 

2. Mkojo kuwa na damu ndani yake uwa ni ishara ya vitu vifuatavyo kama vili maambukizi kwenye figo au pengine ni kwa sababu ya kichocho maana wadudu wanaoambukiza kichocho wakiwa wengi kwenye kibofu Cha mkojo utafuna sehemu za kibofu Cha mkojo na kusababisha kutoa damu kwenye mkojo na kusababisha madhara mengine makubwa kwenye mwili wa binadamu.

 

3.vile vile hali ya kuwepo kwa damu kwenye mkojo usababishwa na Maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo na pengine maambukizi kwenye urethra kama Kuna maambukizi kwenye sehemu hizo wadudu utafuna sehemu mbalimbali za kwenye kibofu Cha mkojo na kusababisha maambukizi ambayo usababisha mkojo kuwa na damu.

 

 4.pengine rangi ya mkojo uwa nyeusi. Hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa sehemu mbalimbali za bile (nyongo), kwa hiyo kama Kuna bile kwenye mkojo, mkojo huwa na rangi nyeusi,kwa hiyo hii si rangi rasmi ya mkojo kwa hiyo kiwango Cha bili pigment kwenye mkojo kinapaswa kuwa Cha kawaida na kufanya  rangi ya mkojo kuwa kawaida kwa hiyo rangi nyeusi siyo rangi ya mkojo.

 

5.Madawa mbalimbali usababisha rangi ya mkojo kubadilika sana , kwa mfano wagonjwa wanaotumia dawa ya rifampicin mkojo wao huwa mwekundu na wakati mwingine huwa wa orange hii ni kwa sababu ya Aina ya dawa kwa hiyo watu wanaotumia madawa ya Aina hii wanapaswa kunywa sana maji ili kufanya mkojo wao uwe na rangi ya kahawia Bali sio rangi  nyekundu au rangi ya orange.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views: 2451

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 web hosting     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Njia za kuingiza chanjo mwilini

Posti hii inahusu njia mbalimbali ambazo utumika kupitisha chanjo, njia hizo utegemea na kazi ya chanjo kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini

Soma Zaidi...
Nini husababisha kizunguzungu?

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo mbalimbali ambayo husababisha kizunguzungu.

Soma Zaidi...
Njia za kujikinga na vidonda vya tumbo

Kama unahitaji kujuwa namna ya kuweza kujikinga na vidonda vya tumbo, basi makala hii ni kwa ajili yako. Hapa utaweza kuzijuwa hatuwa zote za kujikinga na kupata vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa

Posti hii inahusu namna ya kumsafisha mgonjwa kinywa,ni njia unazopaswa kufuata wakati unamsafisha mgonjwa kinywa hasa wale walio mahututi.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu.

Posti hii inahusu zaidi mgawanyo wa matibabu ya kifua kikuu, tunajua kubwa kifua kikuu ni Ugonjwa ambao utumia mda mrefu kidogo katika matibabu kwa hiyo mgawanyiko wake uko kwenye sehemu mbili muhimu kama tutajavyoona

Soma Zaidi...