Dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria
Posti hii inahusu zaidi dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ,ni dawa ambayo utumiwa na watu wengi kwa matibabu ya ugonjwa wa Malaria.
Kazi za ALU katika kutibu ugonjwa wa Malaria.
1. ALU ni dawa inayotumiwa kutibu ugonjwa wa Malaria kwa Lugha nyingine huitwa mseto, ALU kwa kirefu chake ni Artemether Lumefantrine, hili ni Jina la kitaalamu ambalo Lina dawa mbili ya kwanza ni Artemether yenye gram ya 20 mg na nyingine ni Lumefantrine yenye milligram ya 120 jumla dawa hii ya ALU Ina milligram 140 mg ambazo utumiwa kulingana na utaratibu inayotolewa na wataalamu wa afya kama vile madaktari, wauguzi na waphamasia kulingana na utaratibu unapaswa kutumiwa kwa mgonjwa.
2.Dawa hii ya Mseto utumiwa na wagonjwa ambao Wana malaria ya kawaida hii dawa siyo ya wagonjwa wenye malaria kali, utawafahamuje wagonjwa wenye Malaria ya kawaida kwa kuangalia dalili mbalimbali kama vile Homa kwa mtu wenye malaria, kuuma kwa joint, kutapika kwa Mgonjwa, maumivu ya kichwa kwa mgonjwa, mwili mzima kuishiwa nguvu, kuharisha kwa mgonjwa lakini sio sana kukosa hamu ya kula chakula, hizi dalili zinatokea kwa Mgonjwa na zinakuwa hazina nguvu sana kwa mgonjwa kwa hiyo mgonjwa akipata dalili kama hizi anapaswa kwenda hospitalini kwa ajili ya vipimo na akigundua kuwa ni malaria anaweza kutumia Mseto kwa sababu hizi na dalili za kawaida.
3. Dawa hizi za Mseto pia hazipaswi kutumiwa na wanawake wajawazito kwa sababu zinaweza kuleta madhara makubwa kwa kwa mtoto akiwa tumboni kwa hiyo akina Mama wajawazito wanapaswa kujua hili na walizingatie na kujua kuwa wanapaswa kutumia dawa zao za SP wakiwa wajawazito Ili kuzuia maambukizi ya malaria kwa mtoto, kwa hiyo elimu inabidi kutolewa kwa akina Mama hasa wajawazito Ili kuepuka matatizo yanayoweza kutokea, pia dawa hii hakipaswi kutumiwa na watu wenye Allergy nayo kwa hiyo labda mtu mwingine anaweza kuitumia akawa na vi upele na matokea ambayo yanaweza kujitokeza na kumweka mtu katika hali ya hatari hasitumie.
4. Dawa hii ya Mseto inaweza kuwa na matokea mbalimbali kama vile kichwa kuuma, kizunguzungu,kutapika kuishiwa nguvu, kukosa hamu ya kula mgonjwa hasishangae au kuogopa haya na maudhi madogo madogo madogo yanatokea kwa mgonjwa ni kwa sababu dawa inakuwa inapambana na bakteria Ambao wapo kwenye mwili.
5. Kwa hiyo mgonjwa akitumia dawa hii anapaswa kula na kushiba kunywa maji mengi, kwa kufanya hivyo dawa ufanya kazi vizuri na matokea mengine kama vile kukosa nguvu anaweza hasiyapate na kumeza dawa zake Huku akiendekea na kazi zake za kawaida katika jamii. Kwa hiyo saw hii ya Mseto ikitumiwa vyema mtu anaweza kupona haraka na iwapo atazingatia masharti katika matumizi yake.kwa hiyo Mseto ni dawa nzuri na ya uhakika katika kutibu ugonjwa wa Malaria.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Umuhimu wa kutumia dawa za ARV
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kutumia dawa za ARV kwa wathirika wa virusi vya ukimwi .pia tutangalia kwa undani mambo ya kuzingatia kwa wathirika wanaotumia ARV .pamoja na kujali watu wanaotumia dawa hizo .
Soma Zaidi...Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital
Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.
Soma Zaidi...Dawa na matibabu ya presha ya kushuka
Hapa utajifuanza dalili za presha ya kushuka, na dawa ya presha ya kushuka na nJia za kuzuiaama kudhibiti presha ya kushuka
Soma Zaidi...Dawa ya fangasi na dalili za fangasi
hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu dawa ya Albendazole
Post hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia kutibu minyoo, na pia imefanikiwa sana kadri ya watumiaji wa dawa hiyo.
Soma Zaidi...