picha

Dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria

Posti hii inahusu zaidi dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ,ni dawa ambayo utumiwa na watu wengi kwa matibabu ya ugonjwa wa Malaria.

Kazi za ALU katika kutibu ugonjwa wa Malaria.

1. ALU ni dawa inayotumiwa kutibu ugonjwa wa Malaria kwa Lugha nyingine huitwa mseto, ALU kwa kirefu chake ni Artemether  Lumefantrine, hili ni Jina la kitaalamu ambalo Lina dawa mbili ya kwanza ni Artemether yenye gram ya 20 mg na nyingine ni Lumefantrine yenye milligram ya 120 jumla dawa hii ya ALU Ina milligram 140 mg ambazo utumiwa kulingana na utaratibu inayotolewa na wataalamu wa afya kama vile madaktari, wauguzi na waphamasia kulingana na utaratibu unapaswa kutumiwa kwa mgonjwa.

 

2.Dawa hii ya Mseto utumiwa na wagonjwa ambao Wana malaria ya kawaida hii dawa siyo ya wagonjwa wenye malaria kali, utawafahamuje wagonjwa wenye Malaria ya kawaida kwa kuangalia dalili mbalimbali kama vile  Homa kwa mtu wenye malaria, kuuma kwa joint, kutapika kwa Mgonjwa, maumivu ya kichwa kwa mgonjwa, mwili mzima kuishiwa nguvu, kuharisha kwa mgonjwa lakini sio sana kukosa hamu ya kula chakula,  hizi dalili zinatokea kwa Mgonjwa na zinakuwa hazina  nguvu sana kwa mgonjwa kwa hiyo mgonjwa akipata dalili kama hizi anapaswa kwenda hospitalini kwa ajili ya vipimo na akigundua kuwa ni malaria anaweza kutumia Mseto kwa sababu hizi na dalili za kawaida.

 

3. Dawa hizi za Mseto pia hazipaswi kutumiwa na wanawake wajawazito kwa sababu zinaweza kuleta madhara makubwa kwa kwa mtoto akiwa tumboni kwa hiyo akina Mama wajawazito wanapaswa kujua hili na walizingatie na kujua kuwa wanapaswa kutumia dawa zao za SP wakiwa wajawazito Ili kuzuia maambukizi ya malaria kwa mtoto, kwa hiyo elimu inabidi kutolewa kwa akina Mama hasa wajawazito Ili kuepuka matatizo yanayoweza kutokea, pia dawa hii hakipaswi kutumiwa na watu wenye Allergy nayo kwa hiyo labda mtu mwingine anaweza kuitumia akawa na vi upele na matokea ambayo yanaweza kujitokeza na kumweka mtu katika hali ya hatari hasitumie.

 

4. Dawa hii ya Mseto inaweza kuwa na matokea mbalimbali kama vile kichwa kuuma, kizunguzungu,kutapika kuishiwa nguvu, kukosa hamu ya kula mgonjwa hasishangae au kuogopa haya na maudhi madogo madogo madogo yanatokea kwa mgonjwa ni kwa sababu dawa inakuwa inapambana na bakteria Ambao wapo kwenye mwili. 

 

5. Kwa hiyo mgonjwa akitumia dawa hii anapaswa kula na kushiba kunywa maji mengi, kwa kufanya hivyo dawa ufanya kazi vizuri na matokea mengine kama vile kukosa nguvu anaweza hasiyapate na kumeza dawa zake Huku akiendekea na kazi zake za kawaida katika jamii. Kwa hiyo saw hii ya Mseto ikitumiwa vyema mtu anaweza kupona haraka na iwapo atazingatia masharti katika matumizi yake.kwa hiyo Mseto ni dawa nzuri na ya uhakika katika kutibu ugonjwa wa Malaria.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 5039

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 web hosting     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Dawa ya fangasi na dalili za fangasi

hapa utajifunza dalili za fangasi, dawa ya fangasi na aina za fangasi, pia nitakujuza njia za kukabiliana na fangasi

Soma Zaidi...
Njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake

Posti hii inahusu zaidi njia ya kupitisha dawa kwenye mdomo na vipengele vyake, hii njia dawa umengenywa kwenye tumbo na kupitia kwenye utumbo mdogo na baadae kwenye damu,

Soma Zaidi...
Dawa za maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za maumivu ya jino

Soma Zaidi...
IJUE DAWA YA AMOXLINE (antibiotic) NA MATUMIZI YAKE

Posti hii inahusu zaidi dawa ya amoxline .jinsi inavyofanya kazi mwilini.pamoja na matumizi yake.

Soma Zaidi...
Fahamu kazi za homoni katika kupamba na kansa.

Post hii inahusu zaidi homoni mbalimbali ambazo upambana na kansa, hizi homoni zikitumika vizuri matokeo yake huwa na mazuri pia kwa wagonjwa wa kansa.

Soma Zaidi...
Chini ya Tumbo langu Kuna uchungu lakini si sana shinda ni ni?

Nini kinasababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu?

Soma Zaidi...