picha

Dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria

Posti hii inahusu zaidi dawa ya ALU kama Dawa inayotibu Ugonjwa wa Malaria ,ni dawa ambayo utumiwa na watu wengi kwa matibabu ya ugonjwa wa Malaria.

Kazi za ALU katika kutibu ugonjwa wa Malaria.

1. ALU ni dawa inayotumiwa kutibu ugonjwa wa Malaria kwa Lugha nyingine huitwa mseto, ALU kwa kirefu chake ni Artemether  Lumefantrine, hili ni Jina la kitaalamu ambalo Lina dawa mbili ya kwanza ni Artemether yenye gram ya 20 mg na nyingine ni Lumefantrine yenye milligram ya 120 jumla dawa hii ya ALU Ina milligram 140 mg ambazo utumiwa kulingana na utaratibu inayotolewa na wataalamu wa afya kama vile madaktari, wauguzi na waphamasia kulingana na utaratibu unapaswa kutumiwa kwa mgonjwa.

 

2.Dawa hii ya Mseto utumiwa na wagonjwa ambao Wana malaria ya kawaida hii dawa siyo ya wagonjwa wenye malaria kali, utawafahamuje wagonjwa wenye Malaria ya kawaida kwa kuangalia dalili mbalimbali kama vile  Homa kwa mtu wenye malaria, kuuma kwa joint, kutapika kwa Mgonjwa, maumivu ya kichwa kwa mgonjwa, mwili mzima kuishiwa nguvu, kuharisha kwa mgonjwa lakini sio sana kukosa hamu ya kula chakula,  hizi dalili zinatokea kwa Mgonjwa na zinakuwa hazina  nguvu sana kwa mgonjwa kwa hiyo mgonjwa akipata dalili kama hizi anapaswa kwenda hospitalini kwa ajili ya vipimo na akigundua kuwa ni malaria anaweza kutumia Mseto kwa sababu hizi na dalili za kawaida.

 

3. Dawa hizi za Mseto pia hazipaswi kutumiwa na wanawake wajawazito kwa sababu zinaweza kuleta madhara makubwa kwa kwa mtoto akiwa tumboni kwa hiyo akina Mama wajawazito wanapaswa kujua hili na walizingatie na kujua kuwa wanapaswa kutumia dawa zao za SP wakiwa wajawazito Ili kuzuia maambukizi ya malaria kwa mtoto, kwa hiyo elimu inabidi kutolewa kwa akina Mama hasa wajawazito Ili kuepuka matatizo yanayoweza kutokea, pia dawa hii hakipaswi kutumiwa na watu wenye Allergy nayo kwa hiyo labda mtu mwingine anaweza kuitumia akawa na vi upele na matokea ambayo yanaweza kujitokeza na kumweka mtu katika hali ya hatari hasitumie.

 

4. Dawa hii ya Mseto inaweza kuwa na matokea mbalimbali kama vile kichwa kuuma, kizunguzungu,kutapika kuishiwa nguvu, kukosa hamu ya kula mgonjwa hasishangae au kuogopa haya na maudhi madogo madogo madogo yanatokea kwa mgonjwa ni kwa sababu dawa inakuwa inapambana na bakteria Ambao wapo kwenye mwili. 

 

5. Kwa hiyo mgonjwa akitumia dawa hii anapaswa kula na kushiba kunywa maji mengi, kwa kufanya hivyo dawa ufanya kazi vizuri na matokea mengine kama vile kukosa nguvu anaweza hasiyapate na kumeza dawa zake Huku akiendekea na kazi zake za kawaida katika jamii. Kwa hiyo saw hii ya Mseto ikitumiwa vyema mtu anaweza kupona haraka na iwapo atazingatia masharti katika matumizi yake.kwa hiyo Mseto ni dawa nzuri na ya uhakika katika kutibu ugonjwa wa Malaria.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 5287

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Fahamu antibiotics ya asili.

Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida.

Soma Zaidi...
Kazi za Dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria

Posti hii inahusu zaidi kazi za dawa ya Artesunate katika kutibu Malaria kali, ni dawa ambayo inatumika sana kutibu Malaria kali.

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Soma Zaidi...
Dawa ya Rifampicin na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Dawa ya penicillin ambayo uzuia asidi ya bakteria.

Post hii inahusu zaidi dawa ya phenoxy-methyl penicillin ambayo upambana na aina ya bakteria ambao utoa sumu Ili kuzuia dawa isifanye kazi.

Soma Zaidi...
Matibabu ya ugonjwa wa uti wa mgongo

Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mgonjwa wa uti wa mgongo, kwa kawaida tunajua kuwa homa hii ya uti wa mgongo usababisha na wadudu mbalimbali kama vile bakteria, virus, fungasi, sumu mbalimbali kama vile madini ya lead na arseni, na vitu kama vile Mag

Soma Zaidi...