Utaratibu wa kuzuru makaburi na dua zinazosomwa wakati wa kuzuru kaburi


image


Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika katika kuzuru kaburi la muislamu.


UTARATIBU NA DUA YA KUZURU MAKABURI

Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi. Ni katika matendo yanayotukumbusha kifo. Hata mtume allikuwa akienda kuzuru makaburi mara kadhaa. Hata mwishoni mwa siku za mwisho za uhai wake alikwenda kuzuru makaburi na kuwaaga waliokufa na kuwaombea dua.
 
 
 
Hapo mwanzo wanawake walikatazwa kuzuru makaburi kwa maneno ya Mtume aliposema “wamelaaniwa wanawake wenye kuzuru makaburi”. lakini baadaye mtume akawaruhusu wanawake kuzuru makaburi. Kwa ufupi ibada hii ni kwa waislamu wote na haina siku maalumu ama wakati maalumu. Kwani Mtume alikuwa anakwenda kuzuru makaburi hadi wakati wa usiku.
 
 
 
Kuzuru makaburi sio lakima uwe na udhu. Unaweza kuzuru hata ukiwa hupo twahara. Ukifika kwanza unaanza kusalimia (kutoa salamu) kisha unaomba dua pia ukiwa makaburini unaweza kulimia ama kusafishai kaburi ama makaburi. Ama kujazia udongo haya yote sio ya lazima. Kisha utaomba dua
 
 
 
Dua ya kuzuru kaburi
لسَّلامُ عَلَـيْكُمْ أَهْلَ الدِّيارِ مِنَ المؤْمِنيـنَ وَالْمُسْلِمينَ، وَإِنّا إِنْ شاءَ اللهُ بِكُـمْ لاحِقُـونَ، (وَيَرْحَمُ اللَّهُ الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنَّا وَالْمُسْتَأْخِرِينَ) أَسْـاَلُ اللهَ لَنَـا وَلَكُـمْ العَـافِيَةَ.
 
Assalaamu ’alaykum ahlad-diyaar minal Mu-uminiyna wal Muslimiyn, wainnaa In Shaa Allaahu bikum laahiquwn. (Wa yarhamu-Allaahu al-mustaqdimiyna minnaa wal musta-akhiriyna). As-alu-Allaaha lanaa walakumul-’aafiyah
 
 
Amani ishuke juu yenu watu wa nyumba za Waumini na Waislamu, nasi apendapo Allaah tutakutana nanyi (Na Allaah Awarehemu wa mwanzo na wa mwisho). Namuomba Allaah Atupe sisi nanyi Al-’Aafiyah
al-hidaayah.com
 
 
Mwenye kuzuru makaburi anaruhusiwa kwenda akiwa peke yake ama akiwa na wenzie. Halikadhalika hakuna mavazi ya rangi maalumu wakati wa kuzuru ama kuzika. Hakuna haja ya kunyoa nywele wana kuandaa vyakula. Hairuusiwi kuyataja mabaya ya aliuyefariki ama kukaa juu ya kaburi. Pia hairuhusiwi kuzungumza mabo maovu maeneo ya makaburi.
 
 
Kwa hakika kuzuru makaburi ni ibada inayotaka utulivu wa nafsi. Kwani inatakikana moyo upate mawaidha kutokana na kutembelea kaburi. Mwenye kuzuru kaburi apate athari ya kuyaogopa mauti ili apate kufanya maandalizi.
 
 



Sponsored Posts


  👉    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       👉    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       👉    3 Madrasa kiganjani offline       👉    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma
Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma. Soma Zaidi...

image Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali
Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali. Soma Zaidi...

image Jinsi ambavyo msafiri anatakiwa aswali akiwa safarini
Postvhiibinakwenda kukufundisha kuhusu swala ya msafiri na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Taratibu za kuchaguwa mchumba katika uislamu
Hapa utajifunza hatuwa kwa hatuwa za kuchaguwa mchumba kulingana na sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

image Zijuwe aina kuu 6 za talaka katika uislamu
Talaka zimegawanyika katika makundi mengi. Katika somo hili utakwenda kukifunza aina kuu za talaka katika uislamu. Soma Zaidi...

image Dhana ya kumiliki raslimali katika uislamu
Ni ipi raslimali ya halali kuimiliki katika uislamu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swwla ya dhuha na faida zake
Post hii inakwenda kukufunza kuhusu swala ya dhuha, faida zake wakati wa kuiswali swala ya dhuha na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Mambo yanayobatilisha funga au yanayoharibu swaumu.
Hapa utajifunza mambo ambayo akiyafanya mtu aliyefunga, basi funga yake itaharibika. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuoga josho la kiislamu ( janaba, hedhi na nifasi)
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kuoga josho kisheria. Soma Zaidi...

image Historia ya adhana na Iqama na jinsi ya kuadhini.
Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu. Soma Zaidi...