Jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kujitwaharisha kutokana na najisi.

Kujitwaharisha Kutokana na Najisi

Kutokana na uzito wa kujitwaharisha tutazigawanya najisi katika makundi matatu
(a)Najisi ndogo.
(b)Najisi kubwa na
(c)Najisi hafifu
(a)Najisi Ndogo.

 


Najisi Ndogo
Inahusu najisi zote isipokuwa najisi ya mbwa na nguruwe. Namna ya kujitwaharisha kutokana na najisi ndogo ni kuosha paliponajisika kwa maji safi mpaka iondoke rangi na harufu ya najisi.

 


Kama tunatumia maji machache ambayo huharibika mara tu yatakapoingiwa na japo najisi ndogo, hatuna budi kutumia kata au chombo kingine cha kuchotea maji na kujitwaharisha pembeni kwa kujimiminia maji kupitia sehemu ile yenye najisi mpaka najisi hiyo iondoke.

 


Katika hali ya kawaida, maji safi hutumika kwa kustanjia. Tunazitwaharisha sehemu zetu za siri kwa mkono wa kushoto mpaka tuhakikishe kuwa najisi imeondoka. Katika hali ya dharura ya kukosa maji au ugonjwa usioruhusu kutumia maji, tunaruhusiwa kustanji kwa kutumia vitu vikavu kama vile karatasi laini (toilet paper), mawe, n.k. Tukistanji kwa vitu vikavu, kama vile mawe makavu tutapangusa sehemu zetu za siri kwa mawe matatu. Kama najisi ingalipo, tutaongeza mawe mawili mawili mpaka turidhike kuwa najisi imeondoka.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1233

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Swala ya Istikhara na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya Istikhara

Soma Zaidi...
Sharti za kutoa zaka

Masharti ya Utoaji wa Zakat na Swadaqat Utoaji katika njia ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Aina ya biashara zilizo haramu kwenye uislamu

Hapa utajifunza aina za biashara ambazo ni haramu.

Soma Zaidi...
Waislamu wanaolazimika kufunga

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala

Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria.

Soma Zaidi...
Lengo la kusimamisha swala

Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Uzuri wa Benki za kiislamu

Kwa nini benki za kiislamu ni bora kuliko benki nyingine?

Soma Zaidi...