picha

Kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi.

(b)Najisi Kubwa:

Najisi hii imeitwa kubwa kutokana na uzito unaochukuliwa katika kujitwah aris ha.
Namna ya kujitwaharisha kutokana na najisi ya mbwa na nguruwe ni kuikosha sehemu hiyo mara saba na mojawapo katika hayo makosho saba iwe kwa kusugua kwa udongo safi. Hivi ndivyo Mtume (s.a.w) alivyotufundisha kama inavyobainika katika Hadithi zifu atazo:

 


Abu Hurairah amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) amesema: Kutw aharisha chombo cha yeyote kati yenu, baada ya kulambwa na mbwa ni kukikosha mara saba, ukitumia udongo katika safari ya kwanza. (Muslim)

 


Ibn Mughafal amesimulia kuwa Mtume (s.a.w) aliamuru kuuawa mbwa (wenye ugonjwa au wasio na waangalizi) kisha akaulizwa: “Vipi juu ya mbwa wengine?” Kisha akaruhusu kufuga mbwa kwa ajili ya kuwindia, kuchungia (na ulinzi kwa ujumla) na akasema: Mbwa atakapolambachombo, kioshe mara saba na kisugue na udongo kwa mara ya nane”. (Muslim)

 


Hadithi hizi zinatupa msimamo wa Uislamu juu ya mbwa, ufugaji wake na namna ya kujitwaharisha kutokana na naye. Tumejifunza kuwa japo mbwa ni mnyama najisi tunaruhusiwa kumfuga kwa ajili ya kuwindia, na ulinzi wa nyumbani. Kama itabidi tufuge mbwa kwa ajili ya madhumuni haya, tutalazimika kuwafunza na kuwatayarishia makao yao yasiyohusiana na watu kwa malazi, chakula au ukaribu wowote.

 


Katika utafiti uliofanywa na Daktari mmoja huko Marekani (1978) iligundulika kuwa mbwa (na nguruwe) ni wachukuzi wa vijidudu vya magonjwa mbali mbali. Baadhi ya vijidudu hivyo havifi kwa dawa yoyote isipokuwa udongo

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Views 2108

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰2 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰4 ai web app     ๐Ÿ‘‰5 Dua za Mitume na Manabii     ๐Ÿ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Faida za kuswali swala za sunnah

Posti hii inakwenda kukufundisha kuhush swala za sunnah.

Soma Zaidi...
Sharti za kutoa zaka

Masharti ya Utoaji wa Zakat na Swadaqat Utoaji katika njia ya Allah (s.

Soma Zaidi...
Hatua za kinga za ugumba na Utasa.

Ugumba ni รขโ‚ฌล“ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasaร‚ย  kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba.

Soma Zaidi...