Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaid
Dalili za kifafa
Kifafa kina dalili ambazo huonekana na mtu ukiziangalia unajua kuwa Ni mojawapo ya kifafa na dalili hizo Ni pamoja na;
1.mwenye kifafa lazima ataonyesha dalili ya kupoteza fahamu ; yaani hawezi kusikia,hawezi kuona, hawezi kusikia maumivu kwa huo muda yaani hatakuwa na ushirikiano wowote ule (unresponsive).
2.lazima atupe au kurusha rusha mikono na miguu,pamoja na kichwa kukigeuza geuza na huo muda mauvu anakuwa hasikii kabisa.
3.kuchanganyikiwa kwa mda
4.mate yenye mchanganyiko wa mapovu kutoka Mdomoni kwa huo muda aliopata kifafa( udenda)
5. Mwenye dalili za kifafa huwa anaduwaa kipindi kifafa kinamtokea.
Sababu za kifafa
1.kurithi; kifafa huweza Kurithi kutoka kizazi hadi kizazi.
2.magonjwa ya kuambukiza Kama vile ukimwi,au uti wa mgongo huweza kusababisha kifafa.
3.madhara kwenye ubongo; Kama vile maji kujaa kwenye ubongo, uvimbe kwenye ubongo, bacteria na virusi vinavyoshambilia ubongo husababisha kifafa pia.
4. Kichwa kuumia (head injury) mfano ukipata ajali ya kichwa pia husababisha kifafa.
Huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa
Kifafa huweza kutibiwa nyumbani na kupona Kama hakijawa sugu au ikiwa Ni kifafa kilichopo na huwa mnamfanyia huduma ya kwanza anapona , namna ya kumpatia huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa;
1.hakikisha sehemu aliyoangukia Ni Safi na Haina vitu vya kumuumiza ili anapopata fahamu asiwe na maumivu ya kuchomwa na kitu .
2.mgeuze mgonjwa alale upande (kiubavu) ili akicheua,akimeza mate au kutapika asipate shida maana yanaweza kurudi kwenye Koo la hewa na kumsababishia shida nyingine au yanaweza kumkaba.
3.mwekee kitu kilaini kwenye kichwa ili awe vizuri (comfortable).
4.mkague Kama amevaa hereni,cheni,au kitu kinachoweza kumuumiza umtoe .
5.mwache mgonjwa apate hewa watu wasimzunguke maana anaweza akakosa hewa.
6.usimzuie mgonjwa kurusha miguu na mikono hauruhusiwi kumshika mwache arushe akipata fahamu ataacha.
7. Usimpatie au kuweka chochote Mdomoni mwake Mana anawaze kutapika, kukabwa, au kurudi kwenye Koo la hewa na kupaliwa.
8.kaa na mgonjwa mapaka atakaporudi katika Hali yake na umuangalie yupo katika Hali gani Kama Ni mzuri au mbaya.
9kama mgonjwa Yuko katika Hali mbaya Sana au amechuku muda mrefu zaidj ya lisaa limoja haja pata fahamu fanya mipango sasa ya kumpeleka hospitali kwaajili ya matibabu .
Mwisho; Kama mgonjwa wa kifafa ndio Mara yake ya kwanza au ameanguka akachukua mda mrefu na Kama ana Hali ya kifafa na hajawahi kwenda hospitalini kwaajili ya uchunguzi Ni vyema kumpeleka akafanyiwe uchunguzi na vipimi na ushauri zaidi.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu hasa jinsi uchafu, wadudu na vitu vingine vinavyoweza kuingia machoni.macho ni mojawapo ya milango mitano ya fahamu ambapo kazi yake ni kuona.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu anayetokwa na damu ya pua
Soma Zaidi...Jiamini A ni katika vitamini inayojulikana sana kuboresha na kuimarisha afya vya macho na uoni. Tafiti zinaonyesha kuwa kuna kundi kubwa la watoto wanaopata tayizobla kutokuona kutokana na ukosefu wa vitamini A vya kutosha.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi athari za kutotibu maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo, nimatazito yanayoweza kutokea iwapo ugonjwa huu hautatibika.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi viwango vitatu vya kuungua. Ili tuweze kujua mtu ameunguaje Kuna viwango vitatu vya kujua kiasi na namna mtu alivyoungua
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi kutoa huduma ya kwanza kwa mtu aliyekula chakula chenye sumu, kula sumu ni kitendo Cha kula kitu chochote kama dawa,pombe, kemikali na chakula kichafu.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa maji mwilini
Soma Zaidi... Maumivu ya kifua yanayosababishwa na kupungua kwa mtiririko wa damu kwenye misuli ya moyo, kitaalamu huitwa Angina ni dalili ya Ugonjwa wa ateri ya Coronary. Ugonjwa huu kawaida hufafanuliwa kama kufinya, shinikizo, uzito, kubana au maumivu kwenye
Soma Zaidi...Makala hii itakwenda kukufundisha kazi 5 za maafu mwilimi. Wengi tunajuwa tu kuwa mapafu yanafanya kazi ya kupumuwa. ila si hivyo tu yapo mengi zaidi.
Soma Zaidi...