Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaid
Dalili za kifafa
Kifafa kina dalili ambazo huonekana na mtu ukiziangalia unajua kuwa Ni mojawapo ya kifafa na dalili hizo Ni pamoja na;
1.mwenye kifafa lazima ataonyesha dalili ya kupoteza fahamu ; yaani hawezi kusikia,hawezi kuona, hawezi kusikia maumivu kwa huo muda yaani hatakuwa na ushirikiano wowote ule (unresponsive).
2.lazima atupe au kurusha rusha mikono na miguu,pamoja na kichwa kukigeuza geuza na huo muda mauvu anakuwa hasikii kabisa.
3.kuchanganyikiwa kwa mda
4.mate yenye mchanganyiko wa mapovu kutoka Mdomoni kwa huo muda aliopata kifafa( udenda)
5. Mwenye dalili za kifafa huwa anaduwaa kipindi kifafa kinamtokea.
Sababu za kifafa
1.kurithi; kifafa huweza Kurithi kutoka kizazi hadi kizazi.
2.magonjwa ya kuambukiza Kama vile ukimwi,au uti wa mgongo huweza kusababisha kifafa.
3.madhara kwenye ubongo; Kama vile maji kujaa kwenye ubongo, uvimbe kwenye ubongo, bacteria na virusi vinavyoshambilia ubongo husababisha kifafa pia.
4. Kichwa kuumia (head injury) mfano ukipata ajali ya kichwa pia husababisha kifafa.
Huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa
Kifafa huweza kutibiwa nyumbani na kupona Kama hakijawa sugu au ikiwa Ni kifafa kilichopo na huwa mnamfanyia huduma ya kwanza anapona , namna ya kumpatia huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa;
1.hakikisha sehemu aliyoangukia Ni Safi na Haina vitu vya kumuumiza ili anapopata fahamu asiwe na maumivu ya kuchomwa na kitu .
2.mgeuze mgonjwa alale upande (kiubavu) ili akicheua,akimeza mate au kutapika asipate shida maana yanaweza kurudi kwenye Koo la hewa na kumsababishia shida nyingine au yanaweza kumkaba.
3.mwekee kitu kilaini kwenye kichwa ili awe vizuri (comfortable).
4.mkague Kama amevaa hereni,cheni,au kitu kinachoweza kumuumiza umtoe .
5.mwache mgonjwa apate hewa watu wasimzunguke maana anaweza akakosa hewa.
6.usimzuie mgonjwa kurusha miguu na mikono hauruhusiwi kumshika mwache arushe akipata fahamu ataacha.
7. Usimpatie au kuweka chochote Mdomoni mwake Mana anawaze kutapika, kukabwa, au kurudi kwenye Koo la hewa na kupaliwa.
8.kaa na mgonjwa mapaka atakaporudi katika Hali yake na umuangalie yupo katika Hali gani Kama Ni mzuri au mbaya.
9kama mgonjwa Yuko katika Hali mbaya Sana au amechuku muda mrefu zaidj ya lisaa limoja haja pata fahamu fanya mipango sasa ya kumpeleka hospitali kwaajili ya matibabu .
Mwisho; Kama mgonjwa wa kifafa ndio Mara yake ya kwanza au ameanguka akachukua mda mrefu na Kama ana Hali ya kifafa na hajawahi kwenda hospitalini kwaajili ya uchunguzi Ni vyema kumpeleka akafanyiwe uchunguzi na vipimi na ushauri zaidi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepaliwa
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukujulisha njia za kushusha presha iliyopanda.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe, ni kipindi ambacho ni kutoka utotoni kwendea ujana.
Soma Zaidi...Post hii inahusu Aina za kuungua, kuungua ni Hali ya kubabuka kwa ngozi ya mwili na kusababisha madhara mbalimbali
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.
Soma Zaidi...Degedege ni ugonjwa unaoshambulia sana watoto chini ya miaka mitano,na uwaletea matatizo mengi pamoja na kuwepo kwa ulemavu na vifo vingi vinavyosababishwa na ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi Imani potofu juu ya chanjo kwa watoto na akina Mama, ni baadhi ya Imani waliyonayo watu juu ya chanjo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini
Soma Zaidi...