Kifafa hakiambukizi na ugonjwa wa ubongo lakini kifafa pia hakiathiri akili au ubongo Ila kikiwa kifafa Cha kudumu na Cha nguvu ndio huweza kuadhiri. Pia Kuna kifafa Cha mimba na kifafa Cha kawaida.kifafa Cha mimba ndio kinahatari Sana kuliko Cha Kawaida.
Dalili za kifafa
Kifafa kina dalili ambazo huonekana na mtu ukiziangalia unajua kuwa Ni mojawapo ya kifafa na dalili hizo Ni pamoja na;
1.mwenye kifafa lazima ataonyesha dalili ya kupoteza fahamu ; yaani hawezi kusikia,hawezi kuona, hawezi kusikia maumivu kwa huo muda yaani hatakuwa na ushirikiano wowote ule (unresponsive).
2.lazima atupe au kurusha rusha mikono na miguu,pamoja na kichwa kukigeuza geuza na huo muda mauvu anakuwa hasikii kabisa.
3.kuchanganyikiwa kwa mda
4.mate yenye mchanganyiko wa mapovu kutoka Mdomoni kwa huo muda aliopata kifafa( udenda)
5. Mwenye dalili za kifafa huwa anaduwaa kipindi kifafa kinamtokea.
Sababu za kifafa
1.kurithi; kifafa huweza Kurithi kutoka kizazi hadi kizazi.
2.magonjwa ya kuambukiza Kama vile ukimwi,au uti wa mgongo huweza kusababisha kifafa.
3.madhara kwenye ubongo; Kama vile maji kujaa kwenye ubongo, uvimbe kwenye ubongo, bacteria na virusi vinavyoshambilia ubongo husababisha kifafa pia.
4. Kichwa kuumia (head injury) mfano ukipata ajali ya kichwa pia husababisha kifafa.
Huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa
Kifafa huweza kutibiwa nyumbani na kupona Kama hakijawa sugu au ikiwa Ni kifafa kilichopo na huwa mnamfanyia huduma ya kwanza anapona , namna ya kumpatia huduma ya kwanza kwa mwenye kifafa;
1.hakikisha sehemu aliyoangukia Ni Safi na Haina vitu vya kumuumiza ili anapopata fahamu asiwe na maumivu ya kuchomwa na kitu .
2.mgeuze mgonjwa alale upande (kiubavu) ili akicheua,akimeza mate au kutapika asipate shida maana yanaweza kurudi kwenye Koo la hewa na kumsababishia shida nyingine au yanaweza kumkaba.
3.mwekee kitu kilaini kwenye kichwa ili awe vizuri (comfortable).
4.mkague Kama amevaa hereni,cheni,au kitu kinachoweza kumuumiza umtoe .
5.mwache mgonjwa apate hewa watu wasimzunguke maana anaweza akakosa hewa.
6.usimzuie mgonjwa kurusha miguu na mikono hauruhusiwi kumshika mwache arushe akipata fahamu ataacha.
7. Usimpatie au kuweka chochote Mdomoni mwake Mana anawaze kutapika, kukabwa, au kurudi kwenye Koo la hewa na kupaliwa.
8.kaa na mgonjwa mapaka atakaporudi katika Hali yake na umuangalie yupo katika Hali gani Kama Ni mzuri au mbaya.
9kama mgonjwa Yuko katika Hali mbaya Sana au amechuku muda mrefu zaidj ya lisaa limoja haja pata fahamu fanya mipango sasa ya kumpeleka hospitali kwaajili ya matibabu .
Mwisho; Kama mgonjwa wa kifafa ndio Mara yake ya kwanza au ameanguka akachukua mda mrefu na Kama ana Hali ya kifafa na hajawahi kwenda hospitalini kwaajili ya uchunguzi Ni vyema kumpeleka akafanyiwe uchunguzi na vipimi na ushauri zaidi.
Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa
Author Tarehe 2021/12/11/Saturday - 05:46:01 pm Share On Facebook or WhatsApp Imesomwa mara 1519
Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kulia Soma Zaidi...
Dalili na ishara za shambulio la moyo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo. Soma Zaidi...
Matokeo ya maumivu makali.
Posti hii inahusu zaidi matokeo ya maumivu makali , kuna wakati mwingine mgonjwa anapata maumivu makali ya viungo na dawa mbalimbali uweza kutolewa kwa mgonjwa huyo lakini matokeo yake huwa ni kuendelea kwa maumivu kwa hiyo yafuatayo ni matokeo ya maumivu makali. Soma Zaidi...
Dalili za UTI kwa wanaume
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UTI upande wa wanaume Soma Zaidi...
Imani potofu kuhusu uzazi wa mpango
Post hii inahusu zaidi imani potofu kuhusu uzazi wa mpango, ni imani walizonazo Watu kuhusu matumizi ya uzazi wa mpango. Soma Zaidi...
Zijue sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji
Post hii inahusu zaidi sehemu kuu nne za chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji kina sehemu kuu nne na sehemu hizo ufanya kazi tofauti tofauti kama ifuatavyo. Soma Zaidi...
Dawa za kutibu kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za kutibu kiungulia Soma Zaidi...
Dalili na ishara za Ugonjwa wa kuambukiza.
Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe vinaweza kusababisha ugonjwa. Soma Zaidi...
Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu
Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutumia kama ifuatavyo. Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kuporomoka kwa mapafu (pneumothorax)
Posti hii inazungumzia Ugonjwa wa mapafu ambao hujulikana Kama pafu lililoporomoka (Pneumothorax) hutokea wakati hewa inavuja kwenye nafasi kati ya mapafu yako na ukuta wa kifua. Hewa hii hutoka nje ya pafu lako. Ugonjwa huu unaweza kusababishwa na jeraha butu au la kupenya la kifua, taratibu fulani za matibabu zinazohusisha mapafu yako, au uharibifu kutokana na ugonjwa wa msingi wa mapafu. Au inaweza kutokea bila sababu dhahiri. Dalili kwa kawaida hujumuisha'maumivu ya ghafla ya kifua'na upungufu wa kupumua. Soma Zaidi...
Sababu za mtu kuwa na mfadhaiko au wasiwasi
Post hii inahusu sababu za mtu kuwa na mfadhaiko na wasiwasi, mfadhaiko ni nguvu fulani anayoisikia ndani mwake kwa sababu ya tukio la kushutushwa linalomfanya afikilie sana, Soma Zaidi...
mkewang alikuwa anasumbuliwa na tumbo kama siku tatu lika tuliya saivi analalamika kiuno na mgongo vina muuma nini tatizo tockt
Maumivu ya tumbo nakiuno kwa mwanamke yanahitaji uangalizi wakina. Kwani kuna sababu nyingi ambazo zinawezakuwa ni chanzo. Soma Zaidi...