Jinsi macho yanavyoweza kuzungumza kuhusu afya yako ya kimwili na kiakili

Jinsi macho yanavyoweza kuzungumza kuhusu afya yako ya kimwili na kiakili

MACHO YANAFAFANUA KUHUSU AFYA:


Macho ya mwanadamu yanaweza kuwa ni malango wa kufahamu afya ya mtu kiakili na kimwili. Kupitia macho p[olisi na wapelelezi wanaweza kufahamu mhalifu ni nani. Kupitia macho daktari anaweza kufahamu matatizo kadhaa katika afya ya mtu. Makala hii itakwenda kukufahamisha ni kwa namna gani macho yako yanaweza kuweka wazi kuhusu afya yako. Hapa tutakwenda kuona macho katika nyanja hizi:-
A.Umbo
B.Rangi
C.Michubuko
D.Na kama kuna vinyama vilivyoota kwenye macho.



Baada ya kusoma makala hii utaweza kufanya uchunguzi kuhusu afya yako wewe mwenyewe kabla hujakwenda hospitali. Unaweza kutumia kioo ama mtu aliye karibu nawe. Makala hii sio kipimo cha mwisho, hakikisha kuwa majibu kuhusu afya yako utayapata kwa daktari.



1.Mzunguruko wa macho. Kama kwenye mzunguko wa macho yako kwa nje kuna uvimbe hii inaweza kuashiria kuwa mtu huyu atakuwa anasumbuliwa na aleji. Pia inaweza kuwa ama infection (mashambulizi ya bakteria) kwenye machi yake. Hali hii pia inaweza kuashiria matatizo kwenye figo. Hali hii inaweza kuandamana na dalili kama macho kuwa mekundu, miwasho kwenye macho, kuvimba kwa macho. Daktari ataweza kupima mkojo wako ili kupata taarifa juu ya afya ya figo.


2.Kope; kope inaweza kuwa ni kioo cha kuonyesha afya ya mtu. Kama kwenye maoteo ya kupe kuna rangi nyekundu huashiria kuwa huwenda mtu anasumbuliwa na ugonjwa wa naemia (upungufu wa damu). dalili kuu ya ugonjwa huu ni kupauka kwa ngozi ya ndani ya kope. Kama mtu atashindwa kufunga na kufunguwa kope zake vyema itaweza kuashiria shida kwenye mfumo wa neva.



3.Mijongeo ya macho; misuli inayotumika katika mijongeo ya macho, (kwenda kulia, kushoto, juu na chini) ina mahusiano moja kwa moja na mfumo wa neva yaani mfumo wa fahamu hivyo kuwa na mahusiano ya moja kwa moja na ubongo. Sasa endapo mfumo wa fahamu na ubongo utakuwa na matatizo huweza kuathiri misuli hii na kusababisha mtu ,ushindwa kujongesha macho yake kwa ufasaha. Kwa mfamo mtu anaweza kushindwa kupeleka jicho lakoe upande mmoja kama wa kulia ama kushoto.



4.Mahala lilipo jicho lako; jicho lipo kwenye sehemu yake maalumu na linafiti vyema hapo. Sasa wakati mwingine jicho la mtu unaweza kuliona kama limeingia ndani sana ama wengine utaliona limetokeza nje sana. Sasa endapo mtu anasumbuliwa na upungufu wa maji mwilini utakuta macho yeke yameingia ndani. Na endapo macho yake yametokeza nje sana huwenda mtu uyu anasumbuliwa na shida ya tezi ya thyroid.



5.Mboni ya jicho lako; Mara nyingi utaona madaktari wanamulika jicho lako. Kinachoangaliwa ni namna ambavyo mboni ya jicho lako itafanya nini baada ya kumulikwa. Kikawaida mboni inatanuka na kusinyaa kulingana na mwanga ulioifikia. Hivyo endapo jicho lako litashindwa kufanya haya itaonyesha shida kwenye mfumo wa fahamu unaoungana kwenye macho.



6.Ndani ya jicho lako; ndani ya jicho kuzungukia hilo jiduara jeupe unalolioa ambalo ndio jicho kuna vimishipa vingi sana vya damu vimelishikilia. Kwa watu wenye hali mbaya ya shinikizo la juu la damu na wale wenye kisukari huweza kuathiri jisho na kusababisha uoni hafifu. Kufanya uchunguzi wa kina juu ya swala hili kunahitaji ujuzi zaidia, wakati mwingine datkari hutumua kimiminika maalumu ili kulegeza jicho. Dakatari ataweza kuchunguza zadi mpaka sehemu yenye makutano ya neva zinazopelekea taarifa kwenye ubongo



Kama kutakuwa na presha kubwa kwenye fuvu huwenda kutokana na stoke, uvimbe wa ubongo ama maradhi mengine, sehemu ya makutano ya mishipa ya neva (disc) kutakuwa na rangi ya mpaiko na vijimishipa vya damu vitakuwa na rangi ya utofauti.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Huduma Main: Afya File: Download PDF Views 1391

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu vitamini D na kazi zake mwilini

Hapa utajifunza kuusu vitamini D, kazi zake, upungufu wake na chanzo cha kupata vitamini D.

Soma Zaidi...
Utajuwaje kama kidonda kupona

Posti hii inahusu zaidi juu ya kuhakiki kama kidonda kimepona kwa mgonjwa mwenye vidonda, kwanza kabisa tunajua kuwa vidonda uwanyima Watu raha na pengine kuwafanya wakate tamaa kama wapo hospitalini kwa hiyo tunapaswa kutumia njia zifuatazo ili kuweza ku

Soma Zaidi...
Kazi za mifupa mwilinj

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa mifupa mwilini, mifupa ni mojawapo ya tushy zilizounganika na ufanya kazi kubwa kwenye mwili.

Soma Zaidi...
Zijue sababu za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo,ni sababu mbalimbali hasa za kiafya kama tutakavyoona hapo mbeleni

Soma Zaidi...
HUDUMA YA KWANZA KWA MTU ALIYEZIMIA (CARDIOPULMONARYRESUSCITATION) AU CPR

Kuzimia ni hali ya kupoteza fahamu ambako kunaendana na kutokuhema.

Soma Zaidi...
Hatua za kufuata baada ya kuhisi kuwa umeambukizwa na virusi vya HIV

Posti hii inahusu zaidi hatua za kufuata unapohisi umeambukizwa na virus vya ukimwi. Kwa sababu watu wengi wanakuwa na kiwewe anapohisi ameambukizwa na virus vya ukimwi kwa hiyo wanapaswa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Choo kisichokuwa cha kawaida

Posti hii inahusu zaidi Aina ya choo kisichokuwa cha kawaida, ni dalili za choo ambacho siyo Cha kawaida, Ina maana ukiona dalili za choo Cha Aina hii ni vizuri kwenda hospitalini Ili kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe

Post hii inahusu zaidi mabadiliko kwa wavulana wakati wa kubarehe, ni kipindi ambacho ni kutoka utotoni kwendea ujana.

Soma Zaidi...
Namna ya kutumia vidonge vya ARV

Post hii inahusu zaidi matumizi ya vidonge vya ARV, ni vidonge vinavyotumiwa na wagonjwa waliopata ugonjwa wa Ukimwi

Soma Zaidi...
Madhara ya kuchelewa kutibu tatizo la kiafya

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea endapo tatizo halijatibiwa.

Soma Zaidi...