Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii


image


Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?


Je, Mahari inashusha hadhi ya mwanamke?

Kama tulivyojifunza katika Qur-an (4:4), mahari ni hidaya kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w). Kwa maana nyingine, mahari ni mali anayoitoa mwanamume kumpa mwanamke anayetaka kumuoa kwa ajili ya kutafuta radhi za Mwenyezi Mungu (s.w) aliyemuamrisha kutoa mali hiyo iii kumhalalishia mwanamke anayemtaka awe mkewe wa ndoa. Na mwanamke anapokea mahari hayo ikiwa ni zawadi kutoka kwa Mwenyezi Mungu (s.w). Kwa mtazamo huu wa Uislamu mwanamume anapotoa mahari hatakuwa na hata chembe ya hisia kuwa ni bei ya mwanamke anayemuoa. Hali kadhalika, kwa mtazamo huu, mwanamke atakapopokea mahari yake hatakuwa na hata chembe ya hisia kuwa amejiuza kwa mume anayemuoa.

 


llivyo, ni kwamba katika jamii nyingi zisizo za Kiislamu, mahari imefanywa kama bei ya kumnunulia mke inayotozwa na wazazi au walezi wa mwanamke anayeolewa. Ni katika mtizamo huu wa biashara unaowafanya wale wajiitao watetezi wa Haki na Hadhi ya Mwanamke, waishutumu mahari kuwa imetoa mchango mkubwa katika kumnyanyasa mwanamke katika jamii. Ni kweli kabisa kuwa mwanamke, kwa kisingizio cha mahari, amekandamizwa na kunyanyaswa kiasi kikubwa na wanaume katika jamii nyingi za Kikafiri.

 

Lakini, ni kweli kuwa mahari waliyotoa wanaume katika jamii hizi ndio hasa sababu ya kuwashusha wanawake hadhi zao na kuwakandamiza? Je, mahari yakiondolewa kama watetezi wa haki za wanawake wanavyodai, wanawake watapata haki zao na hadhi yao ikarudi mahali pake? Ukweli ni kwamba tatizo haliko kwenye mahari bali tatizo liko kwenye kukiuka maamrisho na makatazo ya Mwenyezi Mungu (s.w) katika utoaji wa hayo mahari na katika kuendesha maisha ya kila siku kwa ujumla.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Taratibu za mirathi katika zama za ujahilia
Kabla ya kuhubiriwa uislamu watu wa Maka walikuwa na tarayibu zenye dhuluma ndani yake katika ugawaji wa mirathi. Soma Zaidi...

image Mambo ambayo hayafunguzi funga
Hii ni orodha ya mambo ambayo hayawezi kuharimu funga yako endapo utayafanya. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl
Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl Soma Zaidi...

image Ni nini maana ya Talaka katika uislamu
Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha. Soma Zaidi...

image Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu
Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha Soma Zaidi...

image Kwa nini imefaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani
Unaweza kijiuliza ni kwa nini hasa kimepelekea kufaradhishwa kufunga mwezi wa Ramadhani. Soma Zaidi...

image Yaliyo haramu kwa mwenye hadathi kubwa.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ya haramu kwa mwenye hadathi kubwa Soma Zaidi...

image Nini maana ya funga na ni lipi lengo lake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu lengo la funga na maana yake katika uislamu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kutekeleza funga za sunnah
Hapa utajifunza muda wa kutia jia katika funga za sunnah. Pia utajifunza kuhusu uhuru ulio nao Soma Zaidi...

image Swala ya jamaa na taratibu zake
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu swala ya jamaa na taratibu zake. Soma Zaidi...