Uchumi wa uislamu umeweka taratibu mbalimbali katika kuchuma mali.
Haki na Uhuru wa kuchuma katika Uislamu
Kwa kuwa kuchuma kwa njia za halali ni wajibu kwa kila mwenye uwezo wa kufanya kazi, hapana budi kila mtu kupewa uhuru kamili wa kutumia juhudi yake na vipawa vyake katika kuchuma kwa njia za halali. Katika Uislamu ni kosa kubwa kwa serikali au Dola kuweka vikwazo vya kuwazuia watu wasitumie vipaji vyao na uwezo wao wote katika kuchuma kwa njia za halali. Kinyume chake, serikali au dola ya Kiislamu ina wajibu wa kuondoa vikwazo vyote vinavyowazuia watu kutumia vipawa vyao vyote katika kuchuma na inawajibu pia wa kutoa motisha na vishawishi vya kuwavutia watu binafsi au watu waliojiunga katika vikundi wajiingize katika sekta mbali mbali za uchumi kwa juhudi kubwa na maarifa.
Pamoja na uhuru kamili uliotolewa na Uislamu wa kuchuma kwa njia za halali kwa kadri ya uwezo wa kila mtu, pia unampa kila mtu haki ya kumiliki kila alichokichuma kwa njia za halali kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:
“Wala msitamani vile ambavyo Mwenyezi Mungu amewafadhilisha baadhi yenu kuliko wengine wanaume wanayo sehemu (kamili) ya vile walivyovichuma, na wanawake nao wanayo sehemu (kamili) ya vile walivyovichuma. Na mwombeni Mwenyezi Mungu fadhila zake. Hakika Mw enyezi Mungu ni Mjuzi w a kila kitu. (4:32)
Umeionaje Makala hii.. ?
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukufundisha maana ya neno talaka katika uislamu kisheria na kilugha.
Soma Zaidi...Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya Twahara Kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu
Soma Zaidi...Hadithi hii inakwenda kukufundisha historia fupi ya adhana pia utakwenda kujifunza jinsi ya kuadhini na kuqimu.
Soma Zaidi...Talaka zimegawanyika katika makundi mengi. Katika somo hili utakwenda kukifunza aina kuu za talaka katika uislamu.
Soma Zaidi...