Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya
? DONDOO NAMBA 1 - 20
? Basi tambua haya;-
1.asilimia 50-90 ya mwili wa kiumbe hai ni maji. Hivyo mtu anaweza kupoteza uhai kwa haraka zaidi kwa upungufu wa maji.
2.Tende zina oxytocin hii husaidia katika kurahisisha mama wakati wa kujifungua. Hivyo ni vyema mjamzito kutumia tunda hili. Pia tende huongeza kiwango cha maziwa.
3.Hakuna madhara kwenye mafuta ya samaki, isipikuwa kunafaida kubwa. Katika mafuta haya kuna omega3 fat acidi. Hii hjulukana kwa uwezo wake wa kuupa mwili nguvu na uwezo wa kufanya kazi. Pia husaidia katika ichakato ya kikemikali mwilini.
4.Ulaji wa samaki hupunguza hatari ya kupata matatizo ya magonjwa ya moyo na shambulio la moyo.
5.Kufanya mazoezi ni jambo lililolazimishwa na wataalamu wa afya. Angalau kwa wiki mtu afanye mazoezi. Mazoezi huweza kuupa mwili afya na uwezo wa kupambana na maradhi.
6.Usinywe maji punde utokapo masoezini, subirika kidogo kama dakika kadhaa mwili kupoa.
7.Hakikisha unapofanya mazoezi jasho likaukie mwilini hasa kwa wale wenye track sut. Jasho husaidia kukausha mafuta yaliyoganya kwenye ngozi.
8.Kuoga pia ni lazima kwa mwanadamu, kuoga husaidia kuondoa stress yaani misongo ya mawazo.
9.Kuoga ni tiba ya matatizo ya kisaikilojia.
10.Kuna katika ulimi wa mwanadamu bakteria, hawa husaidia katika kuzuia hatari ya vyakula vyenye sumu hasa vile vyenye nitrate kama nyama.
11.Ni vyema kupata muda wa kutosha kwa ajili ya kulala. Mwuli huhitajia muda huo kwa ajili ya kurekebisha mifumo ya mwili na kupona kwa majeraha, pia na kupumzika.
12.Mtu anapolala huwa anageuka geuka, kitendo hiki ni muhimu kwa ajili ya afya. Kama mgonjwa hawezi kugeukageukja anatakiwa ageuzwe upande kila baada ya muda..
13.wakati wa usiku mwili hutoa homini iiitwayo melatonin. Hii husaidia katika kuuandaa mwili kulala. Mapigo ya miyo hushuka.
14.Kutokupata muda wa kutosha kulala lkunaweza kusabababisha mwili kupoteza uwezo wake wa kupambana na maradhi.
15.Kama mtu atakosa muda wa kulala kwa miusiku miwili anaweza kupoteza uwezo wa kufanya kazi kwa ufasaha na kuwa na uwezo mdogo wa kufikiri.
16.Mtu akikosa muda wa kulala kwa miusiku mitatu atapata matatizo ya kuona maluelue na atapoteza uwezo wa kufikiri vizuri.
17.Utafiti uliofanywa marekani umeonesha kuwa watu ambao hawana dini au imani ya mungu wapo hatarini kwa asilimia 60% kupata magonjwa ya moyo kuliko ambao wana imani.
18.Pia wataalamu hawa wa Saikolojia wakaongeza kuwa watu wasio na dini maisha yao ni mafupi sana kuliko qenye dini. Halikadhalika watu hawa wanasumbuliwa na maradhi mara kwa mara.
19.Pia tafiti nyingine zimeonesha kuwa watu ambao wanasamehe au wana uwezo wa kusamehe wanakuwa na afya njema ya mwili na akili kuliko ambao hawasamehe au hawana uwezo wa kusamehe. Hivyo ni vyema kujifunza kusamehe.
20.Pia wameongezea kuwa hasira ni hatari kwa afya ya moyo
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Katika somo hili utakwenda kuzinuwa faida za kufunga kitaalamu. Hapa hatutaangalia mtazamo wa dini yeyote
Soma Zaidi...Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua?
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya mambo ya kujiandaa kwa ajili ya kumuona daktari
Soma Zaidi...Zijue kanuni 100 za afya ambazo watu wengi hawazijui. Laiti wangelizijua kwa hakika wangefaidika sana.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu Mambo ya kiafya yanayozungumzwa na umoja wa mataifa
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Kwa kuimarisha afya ya ubongo unaweza kuimarisha kumbukumbu, Kinga za mwili na mengineyo mengi ambayo utajifunza kwenye makala hii
Soma Zaidi...