picha

Dondoo za afya 1-20

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

? DONDOO NAMBA 1 - 20

? Basi tambua haya;-

1.asilimia 50-90 ya mwili wa kiumbe hai ni maji. Hivyo mtu anaweza kupoteza uhai kwa haraka zaidi kwa upungufu wa maji.

2.Tende zina oxytocin hii husaidia katika kurahisisha mama wakati wa kujifungua. Hivyo ni vyema mjamzito kutumia tunda hili. Pia tende huongeza kiwango cha maziwa.

3.Hakuna madhara kwenye mafuta ya samaki, isipikuwa kunafaida kubwa. Katika mafuta haya kuna omega3 fat acidi. Hii hjulukana kwa uwezo wake wa kuupa mwili nguvu na uwezo wa kufanya kazi. Pia husaidia katika ichakato ya kikemikali mwilini.

4.Ulaji wa samaki hupunguza hatari ya kupata matatizo ya magonjwa ya moyo na shambulio la moyo.

5.Kufanya mazoezi ni jambo lililolazimishwa na wataalamu wa afya. Angalau kwa wiki mtu afanye mazoezi. Mazoezi huweza kuupa mwili afya na uwezo wa kupambana na maradhi.

6.Usinywe maji punde utokapo masoezini, subirika kidogo kama dakika kadhaa mwili kupoa.

7.Hakikisha unapofanya mazoezi jasho likaukie mwilini hasa kwa wale wenye track sut. Jasho husaidia kukausha mafuta yaliyoganya kwenye ngozi.

8.Kuoga pia ni lazima kwa mwanadamu, kuoga husaidia kuondoa stress yaani misongo ya mawazo.

9.Kuoga ni tiba ya matatizo ya kisaikilojia.

10.Kuna katika ulimi wa mwanadamu bakteria, hawa husaidia katika kuzuia hatari ya vyakula vyenye sumu hasa vile vyenye nitrate kama nyama.

11.Ni vyema kupata muda wa kutosha kwa ajili ya kulala. Mwuli huhitajia muda huo kwa ajili ya kurekebisha mifumo ya mwili na kupona kwa majeraha, pia na kupumzika.

12.Mtu anapolala huwa anageuka geuka, kitendo hiki ni muhimu kwa ajili ya afya. Kama mgonjwa hawezi kugeukageukja anatakiwa ageuzwe upande kila baada ya muda..

13.wakati wa usiku mwili hutoa homini iiitwayo melatonin. Hii husaidia katika kuuandaa mwili kulala. Mapigo ya miyo hushuka.

14.Kutokupata muda wa kutosha kulala lkunaweza kusabababisha mwili kupoteza uwezo wake wa kupambana na maradhi.

15.Kama mtu atakosa muda wa kulala kwa miusiku miwili anaweza kupoteza uwezo wa kufanya kazi kwa ufasaha na kuwa na uwezo mdogo wa kufikiri.

16.Mtu akikosa muda wa kulala kwa miusiku mitatu atapata matatizo ya kuona maluelue na atapoteza uwezo wa kufikiri vizuri.

17.Utafiti uliofanywa marekani umeonesha kuwa watu ambao hawana dini au imani ya mungu wapo hatarini kwa asilimia 60% kupata magonjwa ya moyo kuliko ambao wana imani.

18.Pia wataalamu hawa wa Saikolojia wakaongeza kuwa watu wasio na dini maisha yao ni mafupi sana kuliko qenye dini. Halikadhalika watu hawa wanasumbuliwa na maradhi mara kwa mara.

19.Pia tafiti nyingine zimeonesha kuwa watu ambao wanasamehe au wana uwezo wa kusamehe wanakuwa na afya njema ya mwili na akili kuliko ambao hawasamehe au hawana uwezo wa kusamehe. Hivyo ni vyema kujifunza kusamehe.

20.Pia wameongezea kuwa hasira ni hatari kwa afya ya moyo

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 3612

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 ai web app     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Kitabu Cha Afya na Lishe

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
JIFUNZE NAMNA YA KUKABILIANA NA UGONJWA WA MAFUA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dondoo za afya 21-40

Somo Hili linakwenda kukuletea dondoo mbalimbali za afya

Soma Zaidi...
AINA ZA VYAKULA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Safari ya damu kwa Kila siku

Posti hii inakwenda kukuletea mfumo wa damu mwilini na safari zake za Kila siku

Soma Zaidi...