UPUNGUFU WA VYAKULA VYA MADINI

UPUNGUFU WA VYAKULA VYA MADINI

2.

Download Post hii hapa

UPUNGUFU WA VYAKULA VYA MADINI

2.UPUNGUFU WA VYAKULA HIVI NA MADHARA YAKE.
Kama tulivyosema huko awali kuwa upungufu wa chochote katika vyakula hivi unaweza kuleta madhara zaidi. Halikadhalika kuzidi kwa baadhi ya virutubisho mwilini kunaweza kusababisha madhara. Kwa mfano madini ya chumvi yakizidi zaidi mwilini yanaweza kusababisha presha ya kushuka. Halikadhalika madini ya chuma yakizidi pia ni hatari.

Mwili unahitaji virutubisho hivi kwa kiwango maalumu. Na mwili wenyewe unafanya kazi hii ya kuchukua kiwango unachohitaji na kinachozidi kinatoka kwa njia ya haja kubwa au ndogo. Sasa hebu tuone kwa ufupi vyakula hivi vinaleta adhari gani pindi virutubisho vikipungua.
v 1.UPUNGUFU WA VYAKULA VYA MADINI
1.Madini ya sodium (table salt) Upungufu wa madini haya utapelekea udhaifu wa misuli na udhaifu wa mifupa. Pia mapigo ya moyo kutokuenda vizuri husababishwa na upungufu wa madini haya.

2.Madini ya chuma. Upungufu wa madini haya hupelekea matatizo katika mfumo wa damu. Ugonjwa wa anaemia unamahusiano ya moja kwa moja na upungufu wa madini ya chuma. Madini ya zink, hupatikana kwenye kamba, kaa, nyama na hamira. Husaidia pia katika afya njemaya mfumo wa kinga (immune system) na uponaji wa majeraha.

3.Madini ya kashiam(calcium). Madini haya yakipunguwa mwilini mifupa na meno huwa na udhaifu. Halikadhalika damu hutoka kwa muda mrefu baada ya jeraha kabla ya kuganda.

4.Madini ya phosphorus,Husaidia katika uimarishwaji wa mifupa, meno,misuli na shughuli za mfumo wa fahamu na utengenezwajiwa genetic materials.

5.Madini ya Potashiam (potassium) husaidia katika kurekebisha kiwango cha majimaji mwilini. Upungufu wa madini haya unaweza kupelekea matatizo katika misuli.

6.Madini yakopa ( copper) Upungufu wa madini haya unaweza ukapelekea urahisi katika kupasuka kwa mishipa ya damu, matatizo mkatika mifupa na viungio (joints).

7.Madini ya manganese Upungufu wa madini haya unaweza ukapelekea kupoteza kwa joto mwilini, mifupa kuwa nyepesi, kutokwa na damu za pua na kupata kizunguzungu.

8.Madini ya iodine Husaidia katika uzalishaji wa homoni ya thyroid. Ugonjwa wa goita (goiter) husababishwa na upungufu wa madini haya.


                   

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Vyakula Main: Afya File: Download PDF Views 865

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Boga (pumpkin)
Boga (pumpkin)

Somo hili linakwenda kukuletea faida za kiafya za kula maboga

Soma Zaidi...
Faida za kula Karoti
Faida za kula Karoti

Umeshawahi kula karoti mbichi, ama ya kupikwa, je unazijuwa faida zake? soma makala hii

Soma Zaidi...
Vyakula vya protini
Vyakula vya protini

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya protini

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula samaki
Faida za kiafya za kula samaki

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula samaki

Soma Zaidi...
Sio salama kwa mtoto wa umri chini ya mwaka mmoja kupewa asali
Sio salama kwa mtoto wa umri chini ya mwaka mmoja kupewa asali

Kwa nini hutakiwi kumpa mtoto wa umri wa chini ya mwaka mmoja kumpa asali?

Soma Zaidi...
Matunda yenye vitamin C kwa wingi
Matunda yenye vitamin C kwa wingi

Somo hili linakwenda kukuletea matunda yenye vitamin C kwa wingi

Soma Zaidi...
Faida za kiafya za kula topetope/ accustard apple
Faida za kiafya za kula topetope/ accustard apple

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za kiafya za kula topetope/ accustard apple

Soma Zaidi...
Vyakula kwa wenye matatizo ya macho
Vyakula kwa wenye matatizo ya macho

Posti hii inahusu zaidi vyakula ambavyo wanapaswa kutumia watu wenye matatizo ya macho,ni vyakula ambavyo uhimalisha mishipa na sehemu nyingine za jicho na kufanya jicho lisiwe na matatizo kwa sababu tunajua wazi kuwa vyakula ni dawa.

Soma Zaidi...