picha

Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Ifahamu dawa ya furosemide.

1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo imo kwenye kundi la diuretics, dawa hii ni maarufu kwa kuzalisha mkojo na kusababisha sumu  kuondoka kwenye mwili na kusababisha moyo kufanya kazi yake kawaida, na pengine dawa hii utolewa kwa wagonjwa hata wasio na tatizo la moyo kabla ya kuwawekea damu, kwa hiyo ni dawa inayosaidia Sana kwenye matibabu.

 

2. Dawa hii pia ufanya Kazi haraka inapotolewa kwa kupitia kwenye mishipa ya damu na  ndani ya saa moja inakuwa imeshaanza kufanya kazi kwenye mwili wa binadamu. Tunafahamu kabisa kwamba kama Kuna kiwango kikubwa cha chumvi kwenye damu usababisha matatizo mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo, kwa hiyo kwa matumizi ya furosemide uhakikisha chumvi hiyo inatolewa kwenye moyo kwa kuhakikisha kwamba mgonjwa anakojoa ,kwa hiyo dawa hii ufanya Kazi kupitia kwenye Figo, na kwa kupitia katika hali ya kutoa mkojo usababisha sumu kutolewa mwilini.

 

3. Vile vile dawa hii huwa na maudhi madogo madogo wakati wa kutumia ,na sio maudhi tu dawa hii upunguza kiwango cha madini mwilini,na vile kuongeza kiwango cha sukari mwilini kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanapaswa kuwa makini hasa wale wenye tatizo la sukari kupanda, na pia wale wenye tabia ya kupungukiwa na madini wanapaswa kuwa makini pindi watumiapo dawa hii, au kama Kuna tatizo kubwa kwa wagonjwa wa sukari na wenye upungufu wa madini ni vizuri kabisa kutumia dawa chini ya uangalizi maalumu.

 

4. Kwa hiyo dawa hii inawezekana kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la sukari ya kupanda na wenye tatizo la upungufu wa madini wanapaswa kuitumia kwa utaratibu wa wataalamu wa afya, na vile dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela Bali utumika kulingana na wataalamu wa afya.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 3423

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 ai web app     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Fahamu matumizi ya Ampicillin.

Ampicillin ni antibiotic yenye msingi wa penicillin ambayo inafanya kazi kupambana na maambukizi ya ndani ya bakteria. Ampicillin hufanya kazi ya kuharibu kuta za kinga ambazo bakteria huunda ndani ya mwili wako na kuzuia bakteria wapya kutokeza. Ampici

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za 5-fluorouracil,Tegafur na uracili

Post hii inahusu zaidi dawa za 5-fluorouracil, Tegafur na uracili katika kupambana na kansa.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu maumivu ya jino

Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Fahamu dawa ya Prednisone katika kupambana na aleji

Post hii inahusu zaidi dawa ya Prednisone ambayo usaidia katika kupambana na aleji.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya potassium sparing

Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...
Namna ya kutumia tiba ya jino.

Posti hii inahusu zaidi namna au njia ya kufanya Ili kuweza kutumia tiba hii ya jino, kwa sababu ya mchanganyiko ambao umekwisha kuwepo kwa hiyo unachumua mchanganyiko unafanya kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...