picha

Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Ifahamu dawa ya furosemide.

1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo imo kwenye kundi la diuretics, dawa hii ni maarufu kwa kuzalisha mkojo na kusababisha sumu  kuondoka kwenye mwili na kusababisha moyo kufanya kazi yake kawaida, na pengine dawa hii utolewa kwa wagonjwa hata wasio na tatizo la moyo kabla ya kuwawekea damu, kwa hiyo ni dawa inayosaidia Sana kwenye matibabu.

 

2. Dawa hii pia ufanya Kazi haraka inapotolewa kwa kupitia kwenye mishipa ya damu na  ndani ya saa moja inakuwa imeshaanza kufanya kazi kwenye mwili wa binadamu. Tunafahamu kabisa kwamba kama Kuna kiwango kikubwa cha chumvi kwenye damu usababisha matatizo mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo, kwa hiyo kwa matumizi ya furosemide uhakikisha chumvi hiyo inatolewa kwenye moyo kwa kuhakikisha kwamba mgonjwa anakojoa ,kwa hiyo dawa hii ufanya Kazi kupitia kwenye Figo, na kwa kupitia katika hali ya kutoa mkojo usababisha sumu kutolewa mwilini.

 

3. Vile vile dawa hii huwa na maudhi madogo madogo wakati wa kutumia ,na sio maudhi tu dawa hii upunguza kiwango cha madini mwilini,na vile kuongeza kiwango cha sukari mwilini kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanapaswa kuwa makini hasa wale wenye tatizo la sukari kupanda, na pia wale wenye tabia ya kupungukiwa na madini wanapaswa kuwa makini pindi watumiapo dawa hii, au kama Kuna tatizo kubwa kwa wagonjwa wa sukari na wenye upungufu wa madini ni vizuri kabisa kutumia dawa chini ya uangalizi maalumu.

 

4. Kwa hiyo dawa hii inawezekana kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la sukari ya kupanda na wenye tatizo la upungufu wa madini wanapaswa kuitumia kwa utaratibu wa wataalamu wa afya, na vile dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela Bali utumika kulingana na wataalamu wa afya.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 3854

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 web hosting     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Fahamu antibiotics ya asili.

Post hii inahusu zaidi antibiotics ya asili, ni antibiotics inayotumia vitu vya kila siku na ya kawaida na mtu akaweza kupona kabisa na kufanya kazi kama antibiotics ya vidonge vya kawaida.

Soma Zaidi...
Dawa mbadala za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa mbadala za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
dawa ya minyoo, dalili za minyoo na sababu na vyanzo vya minyoo

MWISHO Mwisho tunapenda kusema kuwa unapohisi una minyoo kutokana na dalili ambazo tumezitaja humu, nenda kituo cha afya ukapate ushauri zaidi.

Soma Zaidi...
Vyakula vya wanga

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya wanga

Soma Zaidi...
Ifahamu dawa ya kutibu kifua kikuu

Post hii inahusu zaidi dawa ya Rifampin kama dawa mojawapo ya kutibu kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Faida za vidonge vya antroextra

Posti hii inahusu zaidi faida za vidonge vya antroextra, ni vidonge kwa ajili ya mifupa, viungo na gegedu, hivi vidonge vimetumiwa na watu wengi na matokeo yake ni mazuri sana, kwa hiyo zifuatazo ni faida za vidonge hivi.

Soma Zaidi...