picha

Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Ifahamu dawa ya furosemide.

1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo imo kwenye kundi la diuretics, dawa hii ni maarufu kwa kuzalisha mkojo na kusababisha sumu  kuondoka kwenye mwili na kusababisha moyo kufanya kazi yake kawaida, na pengine dawa hii utolewa kwa wagonjwa hata wasio na tatizo la moyo kabla ya kuwawekea damu, kwa hiyo ni dawa inayosaidia Sana kwenye matibabu.

 

2. Dawa hii pia ufanya Kazi haraka inapotolewa kwa kupitia kwenye mishipa ya damu na  ndani ya saa moja inakuwa imeshaanza kufanya kazi kwenye mwili wa binadamu. Tunafahamu kabisa kwamba kama Kuna kiwango kikubwa cha chumvi kwenye damu usababisha matatizo mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo, kwa hiyo kwa matumizi ya furosemide uhakikisha chumvi hiyo inatolewa kwenye moyo kwa kuhakikisha kwamba mgonjwa anakojoa ,kwa hiyo dawa hii ufanya Kazi kupitia kwenye Figo, na kwa kupitia katika hali ya kutoa mkojo usababisha sumu kutolewa mwilini.

 

3. Vile vile dawa hii huwa na maudhi madogo madogo wakati wa kutumia ,na sio maudhi tu dawa hii upunguza kiwango cha madini mwilini,na vile kuongeza kiwango cha sukari mwilini kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanapaswa kuwa makini hasa wale wenye tatizo la sukari kupanda, na pia wale wenye tabia ya kupungukiwa na madini wanapaswa kuwa makini pindi watumiapo dawa hii, au kama Kuna tatizo kubwa kwa wagonjwa wa sukari na wenye upungufu wa madini ni vizuri kabisa kutumia dawa chini ya uangalizi maalumu.

 

4. Kwa hiyo dawa hii inawezekana kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la sukari ya kupanda na wenye tatizo la upungufu wa madini wanapaswa kuitumia kwa utaratibu wa wataalamu wa afya, na vile dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela Bali utumika kulingana na wataalamu wa afya.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 3769

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 web hosting     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dawa ya Rifampicin na kazi zake

Posti hii inahusu zaidi Dawa ya Rifampicin na kazi zake, hii ni dawa mojawapo inayotibu kifua kikuu kati ya Dawa zilizoteuliwa kutibu ugonjwa wa kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Dawa ya maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukuletea dawa ya maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Fahamu dawa za kutuliza kifafa inayoitwa phenobarbital

Post hii inahusu dawa za kutuliza kifafa, zipo dawa mbalimbali za kutuliza kifafa Leo tutaona dawa mojawapo inayoitwa phenobarbital katika kutuliza kifafa.

Soma Zaidi...
Mebendazole kama dawa ya kutibu Minyoo.

Post hii inahusu zaidi dawa ya Mebendazole kama Dawa ya kutibu Minyoo, ni dawa inayotumiwa na watu wengi pale wanapokuwa na minyoo, walio wengi wamefanikiwa kupona kwa kutumia Dawa hii.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya Albendazole

Post hii inahusu zaidi dawa ya Albendazole ni mojawapo ya dawa ambazo usaidia kutibu minyoo, na pia imefanikiwa sana kadri ya watumiaji wa dawa hiyo.

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa ya potassium sparing

Post hii inahusu zaidi dawa ya potassium sparing katika matibabu ya magonjwa ya moyo.

Soma Zaidi...