picha

Ifahamu dawa ya furosemide.

Post hii inahusu zaidi dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo ipo kwenye kundi la diuretics na kwa jina linguine huitwa lasix

Ifahamu dawa ya furosemide.

1. Kama tulivyoona hapo mwanzoni dawa ya furosemide ni mojawapo ya dawa ambayo imo kwenye kundi la diuretics, dawa hii ni maarufu kwa kuzalisha mkojo na kusababisha sumu  kuondoka kwenye mwili na kusababisha moyo kufanya kazi yake kawaida, na pengine dawa hii utolewa kwa wagonjwa hata wasio na tatizo la moyo kabla ya kuwawekea damu, kwa hiyo ni dawa inayosaidia Sana kwenye matibabu.

 

2. Dawa hii pia ufanya Kazi haraka inapotolewa kwa kupitia kwenye mishipa ya damu na  ndani ya saa moja inakuwa imeshaanza kufanya kazi kwenye mwili wa binadamu. Tunafahamu kabisa kwamba kama Kuna kiwango kikubwa cha chumvi kwenye damu usababisha matatizo mbalimbali hasa kwa wagonjwa wa moyo, kwa hiyo kwa matumizi ya furosemide uhakikisha chumvi hiyo inatolewa kwenye moyo kwa kuhakikisha kwamba mgonjwa anakojoa ,kwa hiyo dawa hii ufanya Kazi kupitia kwenye Figo, na kwa kupitia katika hali ya kutoa mkojo usababisha sumu kutolewa mwilini.

 

3. Vile vile dawa hii huwa na maudhi madogo madogo wakati wa kutumia ,na sio maudhi tu dawa hii upunguza kiwango cha madini mwilini,na vile kuongeza kiwango cha sukari mwilini kwa hiyo kwa watumiaji wa dawa hii wanapaswa kuwa makini hasa wale wenye tatizo la sukari kupanda, na pia wale wenye tabia ya kupungukiwa na madini wanapaswa kuwa makini pindi watumiapo dawa hii, au kama Kuna tatizo kubwa kwa wagonjwa wa sukari na wenye upungufu wa madini ni vizuri kabisa kutumia dawa chini ya uangalizi maalumu.

 

4. Kwa hiyo dawa hii inawezekana kutumiwa na watu mbalimbali ila wale wenye tatizo la sukari ya kupanda na wenye tatizo la upungufu wa madini wanapaswa kuitumia kwa utaratibu wa wataalamu wa afya, na vile dawa hii haipaswi kutumiwa kiholela Bali utumika kulingana na wataalamu wa afya.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Dawa Main: Post File: Download PDF Views 3894

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 web hosting     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Nani anapaswa kutumia vidonge vya zamiconal.

Posti hii inahusu zaidi watu ambao wana uwezo wa kutumia vidonge vya zamiconal, ni baadhi ya watu au makundi yanayoweza kutumia vidonge hivi.

Soma Zaidi...
DAWA YA FANGASI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za fangasi

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu ugonjwa wa PID

PID ni mashambulizi ya bakteria kwenye mfumo wa uzazi kwa wanawake. Hapa nitakujulisha dawa

Soma Zaidi...
Dawa ya vidonda vya tumbo

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu dawa za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu dawa za kutibu minyoo

Post hii inahusu zaidi dawa mbalimbali za kutibu minyoo, tunafahamu kabisa minyoo ni ugonjwa ambao uwapata watu mbalimbali hasa watoto.

Soma Zaidi...
Dawa ya kutibu macho

Hizi ndio dawa za macho yenye ukavu, kuwasha ama kutoa machozi

Soma Zaidi...