Huduma kwa mama mwenye mimba ambayo inataka kutoka.

Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba inataka kutoka, mimba za aina hiyo kwa kitaalamu huitwa inevitable pregnant ni lazima itoke tu hata kama kuna juhudi mbalimbali za wataalamu mimba hii utoka kabisa.

Huduma kwa mama mwenye mimba inayotaka kutoka.

1. Kwanza kabisa napenda kuwakumbushia kwamba aina ya mimba hii huwa na dalili zote za mimba kutoka ambazo ni pamoja na kutokwa kwa damu nyingi ambayo uandamana na maumivu makali ya tumbo hasa tumbo la chini.kama mama ataangaliwa na wataalamu wa afya mimba uonekane kwenye mlango wa kizazi na mara nyingi kichanga kinakuwa kimeshakufa tayari kwa hiyo mama ufanyiwa uangalizi wa karibu ili kuhakikisha kwamba mimba inatoka kwa utaratibu bila kuasili maisha ya mama.

 

 

 

 

2. Kama mimba iko chini ya miezi mitatu au wiki kumi na mbili kusafishwa kunapaswa kufanyika  kwa kutumia njia ya kitaalam ambayo inaitwa manual vacuum evacuation, kwa hiyo ni vizuri kabisa akina Mama kuelewa siku zao za mimba ili kuweza kupata huduma inayofaa endapo matatizo kama haya yakitokea.

 

 

 

 

3 . Kama mimba ipo zaidi ya miezi minne au zaidi ya wiki kumi na mbili mama anapaswa kupewa dawa za kuanzisha uchungu ili kuweza kujifungua kawaida dawa hizo huitwa oxtocini na siku zote upitishwa kwenye mirija ya damu, mama anapaswa kupewa taarifa zote hatua kwa hatua na pia aambiwe lengo la kupewa dawa za kuanzisha uchungu.

 

 

 

 

 

4. Pia mama anapaswa kutiwa moyo na kumhakikishia usalama na kumwambia kwamba ni hali ambayo utokea akina Mama wengi na pia urudia hali ya kawaida.

 

 

 

 

5. Pia jamii na watu wa karibu wa mama wanapaswa kumtia moyo  mama na kuachana na mila na desturi za kwamba mimba kutoka ni aibu kwa ukoo kwa hiyo wasimtenge mama bali na wenyewe wapewe elimu kuhusu namna ya kumsaidia na kumtunza mama pale atakaporudi kwa hali ya kawaida.

 

 

 

 

6. Pia mama anapaswa kuambiwa wazi wazi siku za kubeba mimba nyingine na afahamu kwamba baada ya mimba kutoka ndani ya siku ishirini na moja anaweza kubeba mimba nyingine kwa hiyo anapaswa kutumia uzazi wa mpango ili kuepuka kubeba mimba nyingine kabla ya viungo havijawa na nguvu kuweza kutunza mimba, kwa hiyo mama akitoa mimba anapaswa kubeba mimba nyingine baada ya miezi sita.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1630

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Fahamu kuhusu fangasi za ukeni

Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.

Soma Zaidi...
Mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili pamoja na mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua kwa Wanaume

Soma Zaidi...
Dalili za Utasa wa wanaume

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Utasa wa Mwanaume hutokana na uzalishaji mdogo wa mbegu za kiume, utendakazi usio wa kawaida wa manii au kuziba kwa manii ambayo huzuia utoaji wa mbegu za kiume. Magonjwa, majeraha, matatizo ya kiafya sugu, u

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia ugumba

Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia ugumba, ni njia ambazo utumiwa na wapenzi ambao wameshindwa kupata watoto hasa kwa wale ambao wamezaliwa wakiwa na uwezo wa kupata watoto lakini kwa sababu tofauti tofauti wanashindwa kupata watoto kwa hiyo njia zifu

Soma Zaidi...
Uchafu unaotoka ukeni na rangi zake.

Posti hii inahusu zaidi uchafu unaotoka ukeni na rangi zake, kwa kawaida ukeni utolewa uchafu, uchafu huo unaweza kuwa kawaida na unaweza kuwa na rangi mbalimbali kutokana na kuwepo kwa Maambukizi.

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa Mama

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuangalia maendeleo ya mtoto akiwa tumboni mwa mama, zoezi hili ufanyika kila mwezi pale mama anapokuja kwenye mahudhurio kwa kufanya hivyo tunaweza kuja maendeleo ya mtoto kwa kila mwezi.

Soma Zaidi...
Dalili za ongezeko la homoni ya estrogen

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo mtu anaweza kupata ikiwa homoni ya estrogen imeongezeka, hizi dalili zikitokea mama anapaswa kuwahi hospital ili kuweza kupata matibabu au ushauri zaidi.

Soma Zaidi...
faida za tendo ka ndoa wakati wa ujauzito

Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia mimba zisiharibike.

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuzuia mimba zisiharibike, kwa sababu kila mama anayebeba mimba anategemea kupata mtoto kwa hiyo na sisi hamu yetu ni kuhakikisha kwamba mtoto anazaliwa kwa kuzuia mimba kuharibik

Soma Zaidi...