Huduma kwa mama mwenye mimba ambayo inataka kutoka.

Post hii inahusu zaidi huduma kwa mama ambaye mimba inataka kutoka, mimba za aina hiyo kwa kitaalamu huitwa inevitable pregnant ni lazima itoke tu hata kama kuna juhudi mbalimbali za wataalamu mimba hii utoka kabisa.

Huduma kwa mama mwenye mimba inayotaka kutoka.

1. Kwanza kabisa napenda kuwakumbushia kwamba aina ya mimba hii huwa na dalili zote za mimba kutoka ambazo ni pamoja na kutokwa kwa damu nyingi ambayo uandamana na maumivu makali ya tumbo hasa tumbo la chini.kama mama ataangaliwa na wataalamu wa afya mimba uonekane kwenye mlango wa kizazi na mara nyingi kichanga kinakuwa kimeshakufa tayari kwa hiyo mama ufanyiwa uangalizi wa karibu ili kuhakikisha kwamba mimba inatoka kwa utaratibu bila kuasili maisha ya mama.

 

 

 

 

2. Kama mimba iko chini ya miezi mitatu au wiki kumi na mbili kusafishwa kunapaswa kufanyika  kwa kutumia njia ya kitaalam ambayo inaitwa manual vacuum evacuation, kwa hiyo ni vizuri kabisa akina Mama kuelewa siku zao za mimba ili kuweza kupata huduma inayofaa endapo matatizo kama haya yakitokea.

 

 

 

 

3 . Kama mimba ipo zaidi ya miezi minne au zaidi ya wiki kumi na mbili mama anapaswa kupewa dawa za kuanzisha uchungu ili kuweza kujifungua kawaida dawa hizo huitwa oxtocini na siku zote upitishwa kwenye mirija ya damu, mama anapaswa kupewa taarifa zote hatua kwa hatua na pia aambiwe lengo la kupewa dawa za kuanzisha uchungu.

 

 

 

 

 

4. Pia mama anapaswa kutiwa moyo na kumhakikishia usalama na kumwambia kwamba ni hali ambayo utokea akina Mama wengi na pia urudia hali ya kawaida.

 

 

 

 

5. Pia jamii na watu wa karibu wa mama wanapaswa kumtia moyo  mama na kuachana na mila na desturi za kwamba mimba kutoka ni aibu kwa ukoo kwa hiyo wasimtenge mama bali na wenyewe wapewe elimu kuhusu namna ya kumsaidia na kumtunza mama pale atakaporudi kwa hali ya kawaida.

 

 

 

 

6. Pia mama anapaswa kuambiwa wazi wazi siku za kubeba mimba nyingine na afahamu kwamba baada ya mimba kutoka ndani ya siku ishirini na moja anaweza kubeba mimba nyingine kwa hiyo anapaswa kutumia uzazi wa mpango ili kuepuka kubeba mimba nyingine kabla ya viungo havijawa na nguvu kuweza kutunza mimba, kwa hiyo mama akitoa mimba anapaswa kubeba mimba nyingine baada ya miezi sita.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 1541

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Dalili za tezi dume na sababu za kutokea kwa tezi dume.

dalili za ugonjwa wa tezi dume, na sababu za kutokea kwa tezi dume, maana ya tezi dume na athari zake

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu fangasi za ukeni

Posti hii inahusu zaidi fangasi za ukeni, hili ni tatizo kubwa ambalo linawakumba watoto, akina dada na wanawake kwa hiyo na vizuri kujua Dalili zake na kuweza kuchukua hatua mapema.

Soma Zaidi...
Maji ya Amniotic

Posti hii inahusu zaidi maji ya Amniotic ni maji ambayo uzunguka mtoto na kufanya kazi mbalimbali kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi

Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi, tunajua kabisa wakati wa hedhi damu inapaswa kuwa nyepesi na ya kawaida ila kuna wakati mwingine inakuwa na mabonge zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kupata mtoto wa kiume

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nadharia ya kupata mtoto wa kiume.

Soma Zaidi...
Mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili pamoja na mambo yanayosababisha nguvu za kiume kupungua kwa Wanaume

Soma Zaidi...
Je nitahakikisha vipi Kama Nina ujauzito

Somo hili linakwenda kukueleza njia za kuhakiki Kama u-mjamzito

Soma Zaidi...
Kutoka kwa mimba, sababu za kutoka kwa mimba, dalili za kutoka mimba na kuzuia mimba kuoka

Mimba inapotoka ina dalili, na zipo sababu kadhaa za kutoka kwa mimba. Je utazuiaje mimba kutoka. Soma makala hii

Soma Zaidi...
Kwa nini hujapata siku zako za hedhi.

Unaweza kupitiliza siku zako za hedhi kwa sababu nyingi. Post hii itakueleza ni kwa nini umechelewa kupata siku zako.

Soma Zaidi...