HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA

Mtume Lut(a.

HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA

HISTORIA YA NABII LUT(A.S) NA WATU WA SODOMA NA GOMORA


Mtume Lut(a.s) ni mpwawe Ibrahiim(a.s) waliohama pamoja yeye kutokea Iraq. Lut(a.s) alitumwa kuulingania Uislamu katika miji miwili ya Sodoma na Gomora katika nchi ya Transjodan.



Tabia ya Watu wa Miji ya Sodoma na Gomora
Jamii aliyoikuta Mtume Lut(a.s) ilikuwa imeanguka sana kimaadili. Walifikia hali ya kuwa waovu zaidi ya wanyama licha ya kuwa maumbile yao yalikuwa ya binaadamu. Walizama kwenye kufanya maovu matatu mazito kama yanavyotajwa katika Qur-an:



Na (wakumbushe Nabii) Lut; alipowaambia watu wake: “Bila shaka nyinyi mnafanya uovu (ambao) hakuna yoyote aliyekutangulieni kwa (uovu) huo katika walimwengu.(29:28)




“Je, mnawaendea wanaume, na mnawakatia njia (watu kwa kuwaua na kuwanyang’anya njiani) na mnafanya maovu katika mikusanyiko yenu?” basi halikuwa jawabu ya watu wake ila kusema: “Tuletee adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa umiongoni mwa wasemao kweli!” (29:29)”



Katika aya hizi tunafahamishwa kuwa watu wa jamii ya Lut (a.s) walikuwa wakifanya maovu mazito yafuatayo:


1) Walikuwa wakiwaendea wanaume wenzao katika kutosheleza matamanio yao ya ngono.

2) Walikuwa wakifanya uharamia na uporaji wa mali za watu.

3) Walikuwa wakifanya maovu haya hadharani na kwa ufahari.

Naapa kwa umri wako! Hakika wao walikuwa katika ulevi wao (wa maovu); wanahangaika ovyo. (15:72)



Je, jamii yetu hivi leo haifanyi haya na zaidi ya haya tena kwa ufahari. Hivi leo kuna mashindano ya U-miss ambayo wasichana vigoli hujitokeza jukwaani mbele ya hadhara ya watazamaji wanaume kwa wanawake wakiwa wamevaa viguo visivyo sitiri mwili. Hali ni hiyo hiyo kwenye kumbi za dansi, disko na hata kwenye sherehe za kiserikali. Na wengine wameenda mbele zaidi hata kufikia wanawake kusoma taarifa za habari katika television wakiwa uchi wa mnyama na kufikia wengine kucheza sinema za wanawake na wanaume wakifanya ngono hadharani.



Leo hii baadhi ya nchi za magharibi zimepitisha sheria yakuruhusu ndoa baina ya wanaume kwa wanaume wakifanya ushenzi ule ule wa mabaradhuli wa miji ya Sodoma na Gomora.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 3335

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana: