Mtume Lut(a.
Mtume Lut(a.s) ni mpwawe Ibrahiim(a.s) waliohama pamoja yeye kutokea Iraq. Lut(a.s) alitumwa kuulingania Uislamu katika miji miwili ya Sodoma na Gomora katika nchi ya Transjodan.
Tabia ya Watu wa Miji ya Sodoma na Gomora
Jamii aliyoikuta Mtume Lut(a.s) ilikuwa imeanguka sana kimaadili. Walifikia hali ya kuwa waovu zaidi ya wanyama licha ya kuwa maumbile yao yalikuwa ya binaadamu. Walizama kwenye kufanya maovu matatu mazito kama yanavyotajwa katika Qur-an:
Na (wakumbushe Nabii) Lut; alipowaambia watu wake: “Bila shaka nyinyi mnafanya uovu (ambao) hakuna yoyote aliyekutangulieni kwa (uovu) huo katika walimwengu.(29:28)
“Je, mnawaendea wanaume, na mnawakatia njia (watu kwa kuwaua na kuwanyang’anya njiani) na mnafanya maovu katika mikusanyiko yenu?” basi halikuwa jawabu ya watu wake ila kusema: “Tuletee adhabu ya Mwenyezi Mungu ikiwa umiongoni mwa wasemao kweli!” (29:29)”
Katika aya hizi tunafahamishwa kuwa watu wa jamii ya Lut (a.s) walikuwa wakifanya maovu mazito yafuatayo:
1) Walikuwa wakiwaendea wanaume wenzao katika kutosheleza matamanio yao ya ngono.
2) Walikuwa wakifanya uharamia na uporaji wa mali za watu.
3) Walikuwa wakifanya maovu haya hadharani na kwa ufahari.
Naapa kwa umri wako! Hakika wao walikuwa katika ulevi wao (wa maovu); wanahangaika ovyo. (15:72)
Je, jamii yetu hivi leo haifanyi haya na zaidi ya haya tena kwa ufahari. Hivi leo kuna mashindano ya U-miss ambayo wasichana vigoli hujitokeza jukwaani mbele ya hadhara ya watazamaji wanaume kwa wanawake wakiwa wamevaa viguo visivyo sitiri mwili. Hali ni hiyo hiyo kwenye kumbi za dansi, disko na hata kwenye sherehe za kiserikali. Na wengine wameenda mbele zaidi hata kufikia wanawake kusoma taarifa za habari katika television wakiwa uchi wa mnyama na kufikia wengine kucheza sinema za wanawake na wanaume wakifanya ngono hadharani.
Leo hii baadhi ya nchi za magharibi zimepitisha sheria yakuruhusu ndoa baina ya wanaume kwa wanaume wakifanya ushenzi ule ule wa mabaradhuli wa miji ya Sodoma na Gomora.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 2468
Sponsored links
👉1
Kitau cha Fiqh
👉2
kitabu cha Simulizi
👉3
Kitabu cha Afya
👉4
Simulizi za Hadithi Audio
👉5
Madrasa kiganjani
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...
Historia ya vita vya Muta
hii ni historia ya vita vya Muta. Katika makala hii utajifunza sababu ya vita hivi na yaliyojiri katika uwanja wa vita. Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Shu’ayb(a.s).
Kutokana na kisa cha Nabii Shu’ayb(a. Soma Zaidi...
UTARATIBU WA KULEA MIMBA
Soma Zaidi...
HISTORIA YA NABII LUTI
Soma Zaidi...
HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.): Ndoto ya nabii Yusufu
Mtume Yusufu(a. Soma Zaidi...
Imam Abu Hanifa: Nuuman Ibn Thabit
Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Soma Zaidi...
Maswali kuhusu Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Hijra ya Mtume(s.a.w) Kwenda Madinah
Njama za Kumuua Mtume(s. Soma Zaidi...