Njia ambazo VVU huambukizwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa
NJIA AMBAZO VVU HUAMBUKIZWA;
Kuna nadharia nyingi zinaelezea ni namna gani ambazo VVU huambukizwa. Katika hizo kuna mbazo ni Imani potofu kabisa na hazifai kukubaliwa. Hapa nitakuletea njia ambazo zinaambukiza VVU. Njia hizo ni:-
1.Kwa kufanya mapenzi (ngono). Unaweza kuambukizwa ikiwa unafanya ngono ya uke, ya mkundu au ya mdomo na mwenzi aliyeambukizwa VVU ambaye damu yake au shahawa zake au majimaji ya ukeni huingia mwilini mwako kwa kupitia michubuko midogo, ama vidonda ama mikato ama sehemu iliyowazi inayoruhusi kufikiwa damu kwa urahisi. Na hii ndiyo njiainayoongoza katika kuambukiza VVU
2. Kwa kuongezewa damu kutoka kwa aliye athirka. Katika namn nyingine, virusi vinaweza kuambukizwa kupitia kuongezewa damu. Kwa sasa si sana njia hii maana damu anayopatiwa mgonjwa itapitia uchunguzi wa kina kabla ya kuongezewa ijapokuwa madhaifu ya kibinadamu yanaweza kufanyika.
3. Kwa kushirikiana matumizi ya sindano na vitu vyenye ncha kali kama visu na viwembe. VVU vinaweza kuambukizwa kupitia sindano, inaweza kutokea wakatiwa matibabu yatakayofayika chini ya utaratibu. Inaweza pia kuwa watumiaji a madawa ya kulevya hushirikiana sana matumizi ya sindano. Endapo mtumiaji wa kwana ana VVU na akajidunga ama kujikata, kisha akachukuwa mtumiaji mwinine na kujidunga ama kujikata muda mfupi toka mtumiaji wenye VVU kutumia.
4. Wakati wa ujauzito au kujifungua au kupitia kunyonyesha. Mama walioambukizwa VVU wanaweza kuambukiza watoto wao endapo hwatakuwa makini. Mama mjamzito mwenye VVU anatakiwa atumie dozi haraka iwezekanavyo ili kuepushamaambukizi kwa mtoto. Hata hivypo inampasa azalie hospitali ili uangalifu zaidi ufanyike wakati a kujifunguwa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 ai web app 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Je fangasi ikikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa ina madhara gani?
Je umeshawaho kujiuliza maswali mengi kihusu fangasi?. Huyu hapa ni mmoja katika waulizaji waliopata kuuliza rundo la maswali haya. Soma post hii kuona nini ameuliza
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa kipindupindu
Post hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa kipindupindu.Ni dalili zinzojitokeza kwa magonjwa wa kipindupindu.
Soma Zaidi...Homa ya manjano kwa watoto wachanga: Nini kifanyike?
Homa ya manjano ni hali ya kawaida kwa watoto wachanga ambapo ngozi na sehemu nyeupe ya macho hubadilika na kuwa na rangi ya manjano. Hali hii hutokea pale kiwango cha bilirubin—kemikali ya manjano inayotokana na kuvunjika kwa seli nyekundu za damu—kinapokuwa kikubwa mwilini kuliko uwezo wa ini la mtoto kuiondoa. Ingawa mara nyingi si hatari, ni muhimu kuifuatilia kwa karibu ili kuzuia madhara kwa mfumo wa neva wa mtoto.
Soma Zaidi...Dalili za Upungufu wa Damu kwa Watoto
Upungufu wa damu kwa watoto (Anemia) ni hali inayotokea wakati mwili wa mtoto unapokuwa na kiwango kidogo cha chembechembe nyekundu za damu au protini ya hemoglobin kuliko kawaida. Hali hii ikiachwa bila kutibiwa inaweza kuathiri ukuaji wa kimwili, kiakili, na mfumo wa kinga wa mtoto. Makala hii inaelezea dalili kuu za upungufu wa damu kwa watoto na hatua za kuchukua ili kuwasaidia.
Soma Zaidi...Dalili ya pressure ya kupanda
Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya
Soma Zaidi...Kichwa kinaniuma mbele sielewi nini
Zijuwe sababu za kuumwa nankichwa upande mmoja wa kichwa.
Soma Zaidi...