Njia ambazo VVU huambukizwa

Njia ambazo VVU huambukizwa

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia ambazo VVU huambukizwa

NJIA AMBAZO VVU HUAMBUKIZWA;

Kuna nadharia nyingi zinaelezea ni namna gani ambazo VVU huambukizwa. Katika hizo kuna mbazo ni Imani potofu kabisa na hazifai kukubaliwa. Hapa nitakuletea njia ambazo zinaambukiza VVU. Njia hizo ni:-

1.Kwa kufanya mapenzi (ngono). Unaweza kuambukizwa ikiwa unafanya ngono ya uke, ya mkundu au ya mdomo na mwenzi aliyeambukizwa VVU ambaye damu yake au shahawa zake au majimaji ya ukeni huingia mwilini mwako kwa kupitia michubuko midogo, ama vidonda ama mikato ama sehemu iliyowazi inayoruhusi kufikiwa damu kwa urahisi. Na hii ndiyo njiainayoongoza katika kuambukiza VVU

 

2. Kwa kuongezewa damu kutoka kwa aliye athirka. Katika namn nyingine, virusi vinaweza kuambukizwa kupitia kuongezewa damu. Kwa sasa si sana njia hii maana damu anayopatiwa mgonjwa itapitia uchunguzi wa kina kabla ya kuongezewa ijapokuwa madhaifu ya kibinadamu yanaweza kufanyika.

 

3. Kwa kushirikiana matumizi ya sindano na vitu vyenye ncha kali kama visu na viwembe. VVU vinaweza kuambukizwa kupitia sindano, inaweza kutokea wakatiwa matibabu yatakayofayika chini ya utaratibu. Inaweza pia kuwa watumiaji a madawa ya kulevya hushirikiana sana matumizi ya sindano. Endapo mtumiaji wa kwana ana VVU na akajidunga ama kujikata, kisha akachukuwa mtumiaji mwinine na kujidunga ama kujikata muda mfupi toka mtumiaji wenye VVU kutumia.

 

4. Wakati wa ujauzito au kujifungua au kupitia kunyonyesha. Mama walioambukizwa VVU wanaweza kuambukiza watoto wao endapo hwatakuwa makini. Mama mjamzito mwenye VVU anatakiwa atumie dozi haraka iwezekanavyo ili kuepushamaambukizi kwa mtoto. Hata hivypo inampasa azalie hospitali ili uangalifu zaidi ufanyike wakati a kujifunguwa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu Rajabu
Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views: 3797

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 web hosting     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Homa ya dengue: Dalili na jinsi inavyoenezwa na mbu.

Homa ya Dengue ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyoambukizwa kwa binadamu kupitia kuumwa na mbu aina ya Aedes aegypti. Ugonjwa huu ni tishio kubwa katika maeneo ya kitropiki na mikoa yenye joto. Ingawa visa vingi ni vya wastani, baadhi ya watu wanaweza kupata Dengue kali (Dengue Hemorrhagic Fever) ambayo inahitaji uangalizi wa haraka wa kimatibabu. Makala hii inaelezea mzunguko wa uenezaji wa virusi hivi na umuhimu wa usafi wa mazingira katika kudhibiti mbu.

Soma Zaidi...
Je, unaweza kupata mimba siku chache baada ya hedhi kuisha?

Jibu fupi ni ndiyo, inawezekana. Ingawa watu wengi huamini kuwa huwezi kupata ujauzito mara tu baada ya hedhi, uhalisia wa kibiolojia unaonyesha kuwa dirisha la uzazi linaweza kufunguka mapema kuliko unavyotarajia. Makala hii inaelezea jinsi mzunguko wa hedhi unavyofanya kazi na kwa nini ni muhimu kuwa makini wakati wote.

Soma Zaidi...
Jifunze kuhusu ugonjwa wa bawasiri na dalili zake

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu ugonjwa wa Bawasiri na dalili zake. Pia utajifunza njia za kujilinda nao.

Soma Zaidi...
Makosa Yanayofanywa na Wapenzi Wengi

Mahusiano ni safari ya kujifunza kila siku. Makala hii inachambua makosa ya kawaida yanayoweza kuathiri ustawi wa mahusiano, ikitoa mwongozo wa jinsi ya kuyatambua na kuyafanyia kazi ili kujenga uhusiano imara na wenye furaha.

Soma Zaidi...
Maajabu ya damu na mzunguuko wake mwilini.

Ukistaajabu ya Musa utastaajabu ya Firauni. Haya ni maneno ya wahenga. Sasa hebu njoo u staajabu ya damu

Soma Zaidi...