Dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo
Zijuwe dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo, kama kiungulia, tumbo kujaa, maumivu ya umbo..

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo huweza kutokea ndani ya tumbo kutokana na mashambulizi ya bakteria aina ya H.pylori, ama kutokana na athari za madawa flani ama mashambulizi ya wadudu wengineo ama kwa sababu ya ugonjwa wa saratani. Makala hii inakwenda kukuletea dalili duu za vidonda vya tumbo.
1.Maumivu ya tumbo; hii pengine ndio katika dalili kuu zaidi ambazo wengi wenye vidonda vya tumo wanaipata. Maumivu haya yanawza kuwa makali sana wakati mgonjwa akiwa na njaa.Tumbo hili ni tofauti na tumbo la ngiri ama chango. Maumivu haya yanaweza kuanzia chini ya kitomvu na kupanda juu hadi kifuani. Maumivu haya yanaweza kufuatana na dalili zifuatazo hapo chini.
2.Tumbo kujaa; tumbo linaweza kujaa gesi hata akashindwa kula vyema. Huenda mgonjwa akajihisi ameshiba badala ya kuka kidogo. Uhalisia si kwamba ameshiba ila tumbo ndio limejawa na gesi.
3.Kukosa hamu ya kula; hii ni katika dalili ya hatari sana, maana umuhimu wa chakula unafahamika vyema. Mgonjwa anaumwa na tumbo na anakosa kabisa hamu ya kula pia anahisi tumbo kujaa.
4.Kupata kiungulia cha mara kwa mara. Kiungulia unaweza kukitibu kwa kutumia dawa, kwani hazina tabu kwa vidonda vya tumbo. Pia unaweza kulamba majivu, hii ni tiba mbadala ambayo inatumka kutibu kiungulia. Lakini epuka kula vyakula vyenye gesi.
5.Kupungua uzito; vidonda vya tumbo vinaweza kusababisha mtu kupungua uzito, bila ya kujuwa sababu maalumu. Inaweza kuwa ni kutokana na kutokula kwake kwa sababu ya kukosa hamu ya kula.
6.Kichefuchefu na kutapika. mgonjwa wa vidonda vya tumbo wakati mwingine anapata kichefuchefu kisicho na sababu maalumu. Hali hii inaweza kumpelekea akatapika ama asitapike. Na wakati mwingine anaweza kuona dmau kwenye matapishi yake.
7.Mapadiliko kwenye kinyesi. Mgonjwa anaweza kuona mabadiliko kwenye rangi ya kinyesi chake. Kinaweza kuwa cheusi sana na chenye harufu mbaya sana. Na wakati mwingine kinaweza kuwa na damu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 ai web app π3 Kitabu cha Afya π4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π5 Kitau cha Fiqh π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Soma Zaidi...Kuumwa na mgongo: Matatizo ya disc na jinsi ya kuepuka upasuaji.
βMaumivu ya mgongo ni mojawapo ya changamoto kubwa za kiafya zinazomkabili binadamu wa karne ya 21. Kati ya visababishi vikuu, matatizo ya diski za mgongo (spinal disc issues) yanashika nafasi ya juu. Makala hii inatoa mwongozo wa kina kuhusu namna diski zinavyofanya kazi, nini kinatokea zinapoharibika, na muhimu zaidi, mikakati ya kitabibu na mazoezi yanayoweza kukusaidia kuepuka njia ya upasuaji na kurejesha ubora wa maisha yako.
Soma Zaidi...Walio katika hatari ya kupata homa ya inni
Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata homa ya ini,kwa sababu ya hali zao mbalimbali wanaweza kupata ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Ninashida Kuna mtu anaumwa pressure Kila anap pima Iko juu il mwil aumuumi at kidg n dawa anatumia unawez kunisaidiaj
Kama unasumbuliwa na presha post hii ni kwa ajili yako. Hapa tutakuoatia ushauri kutokana na swali alilouliza mdau wetu.
Soma Zaidi...Dalili za fangasi uken
Posti hii inahusu zaidi dalili za fangasi uken, hizi ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la fangasi uken.
Soma Zaidi...Kaswende isiyotibiwa: Athari zake kwenye ubongo na moyo.
βKaswende ni ugonjwa wa zinaa (STI) unaosababishwa na bakteria Treponema pallidum. Ingawa ugonjwa huu hupona kirahisi kwa kutumia dawa za antibayotiki (kama Penicillin) katika hatua za awali, kuupuza dalili au kutokumaliza dozi husababisha bakteria kusambaa mwilini na kuathiri mifumo muhimu ya viungo. Makala hii inachunguza hatua ya tatu ya ugonjwa huu (Tertiary Syphilis) na uharibifu wa kudumu inaoweza kusababisha kwenye mfumo wa neva na moyo.
Soma Zaidi...