Dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo
Zijuwe dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo, kama kiungulia, tumbo kujaa, maumivu ya umbo..

DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo huweza kutokea ndani ya tumbo kutokana na mashambulizi ya bakteria aina ya H.pylori, ama kutokana na athari za madawa flani ama mashambulizi ya wadudu wengineo ama kwa sababu ya ugonjwa wa saratani. Makala hii inakwenda kukuletea dalili duu za vidonda vya tumbo.
1.Maumivu ya tumbo; hii pengine ndio katika dalili kuu zaidi ambazo wengi wenye vidonda vya tumo wanaipata. Maumivu haya yanawza kuwa makali sana wakati mgonjwa akiwa na njaa.Tumbo hili ni tofauti na tumbo la ngiri ama chango. Maumivu haya yanaweza kuanzia chini ya kitomvu na kupanda juu hadi kifuani. Maumivu haya yanaweza kufuatana na dalili zifuatazo hapo chini.
2.Tumbo kujaa; tumbo linaweza kujaa gesi hata akashindwa kula vyema. Huenda mgonjwa akajihisi ameshiba badala ya kuka kidogo. Uhalisia si kwamba ameshiba ila tumbo ndio limejawa na gesi.
3.Kukosa hamu ya kula; hii ni katika dalili ya hatari sana, maana umuhimu wa chakula unafahamika vyema. Mgonjwa anaumwa na tumbo na anakosa kabisa hamu ya kula pia anahisi tumbo kujaa.
4.Kupata kiungulia cha mara kwa mara. Kiungulia unaweza kukitibu kwa kutumia dawa, kwani hazina tabu kwa vidonda vya tumbo. Pia unaweza kulamba majivu, hii ni tiba mbadala ambayo inatumka kutibu kiungulia. Lakini epuka kula vyakula vyenye gesi.
5.Kupungua uzito; vidonda vya tumbo vinaweza kusababisha mtu kupungua uzito, bila ya kujuwa sababu maalumu. Inaweza kuwa ni kutokana na kutokula kwake kwa sababu ya kukosa hamu ya kula.
6.Kichefuchefu na kutapika. mgonjwa wa vidonda vya tumbo wakati mwingine anapata kichefuchefu kisicho na sababu maalumu. Hali hii inaweza kumpelekea akatapika ama asitapike. Na wakati mwingine anaweza kuona dmau kwenye matapishi yake.
7.Mapadiliko kwenye kinyesi. Mgonjwa anaweza kuona mabadiliko kwenye rangi ya kinyesi chake. Kinaweza kuwa cheusi sana na chenye harufu mbaya sana. Na wakati mwingine kinaweza kuwa na damu.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Mwenye Kikohozi
Kikohozi ni njia ya asili ya mwili kujisafisha, lakini kwa mtoto, inaweza kuwa chanzo cha usumbufu mkubwa na wasiwasi kwa wazazi. Post hii inatoa mbinu salama na za nyumbani za kumsaidia mtoto kupata nafuu, huku ikielekeza dalili za hatari zinazohitaji msaada wa kitabibu haraka.
Soma Zaidi...Athari za kula vyakula vyenye sukari nyingi kila siku.
Katika ulimwengu wa sasa, sukari imekuwa kiungo kikuu katika vyakula vingi vilivyosindikwa, hali inayochangia kwa kiasi kikubwa magonjwa yasiyoambukiza. Makala haya yanachambua athari za muda mrefu za ulaji wa sukari nyingi, ikizingatia afya ya moyo, uzito wa mwili, na utendaji wa kimetaboliki, huku ikitoa mikakati ya kitaalamu ya kupunguza matumizi ya sukari kwa maisha marefu na yenye tija.
Soma Zaidi...Uzito kupita kiasi (Obesity): Hatari zake kiafya.
Uzito kupita kiasi, au unene uliokithiri (obesity), si suala la mwonekano wa nje pekee, bali ni changamoto kubwa ya kiafya inayoongeza hatari ya kupata magonjwa sugu ambayo yanaweza kupunguza umri wa kuishi. Hali hii hutokea wakati kiasi cha mafuta mwilini kinapozidi kiwango cha kawaida na kuanza kuathiri utendaji kazi wa viungo muhimu. Makala haya yanaelezea hatari za kiafya zinazohusiana na uzito kupita kiasi na umuhimu wa kuchukua hatua za haraka ili kulinda afya yako.
Soma Zaidi...Vyanzo vya sumu mwilini.
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya kuwepo kwa sumu mwilini, kwa sababu kuna wakati mwingine tunapata magonjwa na matatizo mbalimbali ya ki afya tunaangaika huku na huko kumbe sababu kubwa ni kuwepo kwa sumu mwilini na vyanzo vya sumu hiyo ni kama ifuatavy
Soma Zaidi...Dalili za maambukizi kwenye nephroni
Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye nephroni, uweza kutokea kwenye figo Moja au zote mbili.
Soma Zaidi...Bipolar disorders
Bipolar disorder ni hali ya afya ya akili inayohusisha mabadiliko makubwa katika hisia, nishati, na shughuli za kila siku za mtu. Dalili za bipolar disorder zinaweza kuwa kwenye kipindi cha mania na kipindi cha unyogovu, zifuatazo ni dalili za ugonjwa wa bipolar.
Soma Zaidi...