picha

Dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo

Zijuwe dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo, kama kiungulia, tumbo kujaa, maumivu ya umbo..

Dalili kuu 7 za vidonda vya tumbo



DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO



Vidonda vya tumbo huweza kutokea ndani ya tumbo kutokana na mashambulizi ya bakteria aina ya H.pylori, ama kutokana na athari za madawa flani ama mashambulizi ya wadudu wengineo ama kwa sababu ya ugonjwa wa saratani. Makala hii inakwenda kukuletea dalili duu za vidonda vya tumbo.


1.Maumivu ya tumbo; hii pengine ndio katika dalili kuu zaidi ambazo wengi wenye vidonda vya tumo wanaipata. Maumivu haya yanawza kuwa makali sana wakati mgonjwa akiwa na njaa.Tumbo hili ni tofauti na tumbo la ngiri ama chango. Maumivu haya yanaweza kuanzia chini ya kitomvu na kupanda juu hadi kifuani. Maumivu haya yanaweza kufuatana na dalili zifuatazo hapo chini.


2.Tumbo kujaa; tumbo linaweza kujaa gesi hata akashindwa kula vyema. Huenda mgonjwa akajihisi ameshiba badala ya kuka kidogo. Uhalisia si kwamba ameshiba ila tumbo ndio limejawa na gesi.


3.Kukosa hamu ya kula; hii ni katika dalili ya hatari sana, maana umuhimu wa chakula unafahamika vyema. Mgonjwa anaumwa na tumbo na anakosa kabisa hamu ya kula pia anahisi tumbo kujaa.


4.Kupata kiungulia cha mara kwa mara. Kiungulia unaweza kukitibu kwa kutumia dawa, kwani hazina tabu kwa vidonda vya tumbo. Pia unaweza kulamba majivu, hii ni tiba mbadala ambayo inatumka kutibu kiungulia. Lakini epuka kula vyakula vyenye gesi.


5.Kupungua uzito; vidonda vya tumbo vinaweza kusababisha mtu kupungua uzito, bila ya kujuwa sababu maalumu. Inaweza kuwa ni kutokana na kutokula kwake kwa sababu ya kukosa hamu ya kula.


6.Kichefuchefu na kutapika. mgonjwa wa vidonda vya tumbo wakati mwingine anapata kichefuchefu kisicho na sababu maalumu. Hali hii inaweza kumpelekea akatapika ama asitapike. Na wakati mwingine anaweza kuona dmau kwenye matapishi yake.


7.Mapadiliko kwenye kinyesi. Mgonjwa anaweza kuona mabadiliko kwenye rangi ya kinyesi chake. Kinaweza kuwa cheusi sana na chenye harufu mbaya sana. Na wakati mwingine kinaweza kuwa na damu.




                   


Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 6517

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio     ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya     ๐Ÿ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game     ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     ๐Ÿ‘‰5 Madrasa kiganjani     ๐Ÿ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri

Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri

Soma Zaidi...
Dalili za kikohozi cha muda mrefu (Kifua kikuu - TB).

Kifua Kikuu (TB) ni ugonjwa unaoambukiza unaosababishwa na bakteria aina ya Mycobacterium tuberculosis. Ingawa ugonjwa huu huathiri zaidi mapafu, unaweza kushambulia sehemu nyingine za mwili kama uti wa mgongo, figo, au ubongo. Kikohozi cha muda mrefu ni dalili kuu ya TB ya mapafu, ambayo ikiachwa bila kutibiwa, inaweza kusababisha madhara makubwa ya kiafya na kueneza maambukizi kwa watu wengine katika jamii.

Soma Zaidi...
NJIA YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA VIRUSI VYA VYA UKIMWI NA ATHARI ZAKE

Posti hii inahusisha maambukizi ya virusi vya ukimwi .piaย  tutangaliaย  njia za kujikinga naย  ugonjwa wa UKIMWI

Soma Zaidi...
Jinsi ya kupunguza maumivu ya hedhi kwa njia asilia.

Maumivu ya tumbo wakati wa hedhi, kitaalamu kama dysmenorrhea, huwasumbua wanawake wengi kila mwezi. Ingawa mara nyingi hutibika kwa dawa za dukani, njia za asili zinaweza kusaidia sana kupunguza makali ya maumivu hayo bila kuathiri mfumo wa mmeng'enyo wa chakula au figo. Makala hii inaangazia mbinu bora za asili unazoweza kuzitumia nyumbani ili kupata nafuu.

Soma Zaidi...
Maradhi ya macho, dalili zake na matibabu yake

Makala hii itakufundisha maradho makuu ya macho, matibabu yake na tiba zake

Soma Zaidi...
Dalilili za maumivu ya kifua

Maumivu ya kifua huja kwa aina nyingi, kuanzia kuchomwa na kisu hadi kuuma kidogo. Baadhi ya Maumivu ya kifua yanafafanuliwa kama kuponda kuungua. Katika baadhi ya matukio, maumivu husafiri juu ya shingo, hadi kwenye taya.

Soma Zaidi...