Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?
Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw
JE UNAZIJUWA DALILI ZA UKIMWI?
Yaliyomo
- Maana ya VVU na UKIMWI
- Historia fupi ya ukimwi
- Dalili za vvu
- Dalili za ukimwi
- Hatuwa za maambukizo ya vvu hadi kufikia ukimwi
- Njia za maambukizo ya vvu na ukimwi
- Njia za kujikinga na ukimwi
Ukiwa na maoni, mapendekezo ama maswali wasiliana nasi kupitia komenti hapo chini ana namba ya simu.
- Nini maana ya VVU?
VVU ni ufupisho wa maneno Virusi Vya Ukimwi. Hivi ni virusi vinavyo sababisha upungufu wa kinga mwilini. Ni katika aina ya virusi inayofahamika kitaalamu kama retrovisus. Virusi hivi vinaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwenda kwa mwingini kupitia muingiliano wa majimaji ya mwilini (body fluid). ni vurisi ambavyo kushambulia aina ya seli inayofahamika kama CD4.
Nini maana ya UKIMWI?
UKIMWI ni ufupisho wa maneno Upungufu Wa Kinga Mwilini. Upungufu huu hutokea baada ya mwili kushambuliwa na virusi aina ya VVU. Tunasema mtu ana upungufu wa kinga mwilini endapo seli zake za CD4 zitakuwa chini ya 200 kwenye kipimo. Kutoka kupata VVU hadi kuonyesha kupata upungufu wa kinga inaweza kuanzia miaka 5 hadi 5 baada ya maambukizo.
Historia fupi ya UKIMWI na asili yake.
Historia ya ukimwi imeanza zamani sana hata kabla ya neno IKIMWI kuanza kutumoka. Kabla hatujaona kwa ufupi hi historia hii ni vyema tukaanza kujuwa nini chanzo cha ukimwi? Kuna utata wa kutokukubaliana kauli juu ya chanzo cha UKIMWI. Wapo wanaodai kuwa ukimwiumetengenezwa kwenye maabara kisha kusambazwa, kuna wanaosea kuwa ni Mwenyezi Mungu ametowa adhabu ila wanasayansi wanaamini kuwa chanzo cha ukimwi ni Masokwe.
Kwa ufupi zipo nadharia zaidi ya 10 zinazojaribu kueleza nini chanzo cha UKIMWI. Kisayansi inathibitika kuwa ukimwi chanzo chake huwenda ikawa ni masokwe. Hoja hii pia inatiliwa nguvu na historia katika maeneo mbalimbali kama Kongo na maeneo mengine ya Afrika ya Magharibi.
Kwa ufupi ni kuwa tafiti zinaoyesha kuwa virusi vya VVU vilitika kwenye masokwewakati wa uwindaji, huwenda kuitia majeraha ama namna nyingine kulitokea mwingiliano wa majimaji ya mwili na ya sokwe. Virusi vikaanza kubadilika kutoka hatuwa moja hadi nyingine hadi kufikia leo. Kauli hii inatiliwa nguvu baada ya kupatikana kwa taarifa za kihistoria ambazo huwenda miaka ya 1950 watu wa maeneo ya UGANDA NA Kongo1920 walipata upungufu wa kinga Mwilini na walikuwa wanakufa kwa maradhi ambayo yana uhusiano na UKIMWI.
Kwa mara ya kwanza dunia ailianza kupata taharuki juu ya uwepo vivirusi hivi miaka ya 1980 ha hapo virusi hivi vikajulikana kwa jina la HTLV-III/LAV na nchini Uganda ugonjwauliosababishwa na virusi hivi ulikuwa ukifahamika kwa jina la slim. Mpaka kufikia mwaka 1986 international Committee on Taxonomy of Viruses wakaviita virusi hivi kama HIV na ugonjwa unaosababihwa na virusi hivi uitwe AIDs na hapo jina UKIMWI ndipo lilipoanzia.
Hadi kufikia miaka ya 1988 WHO walitangaza siku ya ukimwi duniani. Mapaka kufikia mwaka 1989 maambukizi kidunia yakafikia 400000 kwa makadirio ya moja wa mataifa. Hadi kufikia mwaka 1990 mwezi wa 10 dawa ya kwanza ya kupunguza makali ya virusi tunazozijuwa hivi leo kama ARV ilitangazwa nayo ilikuwa ni zidovidine (AZT).
Ni zipi dalili za mwanzo za HIV?
Hili ni swali la msingi sana na ni zuri pia. Kwa ufupi dalili za mwanzo za HIV huweza kujitokeza kuanzia wiki 2 toka kupata maambikizi, hadi kufikia wiki ya sita toka kupata maambukizi. Kuna wengine wanapita wiki hizi hata bila ya kuona dalili yeyote ile. Lakini pia dalili hizi huweza kuingiliana na maradhi mengine, hivyo haimaanishi kila mwenye dalili hizi atakuwa ni muathirika. Dalili hizo ni kama:-
- Kupata homa
- Maumivu ya kichwa
- Mafua
- Miwasho, ukurutu na upele
- Vidonda vya koo
- Kuvimba na kuuma kwa tezi za kwenye shingo na mapaja (mtoki)
- Kubanwa punzi
Dalili hizi huweza kuchukuwa muda mchache sana ndani ya wiki za mwanzo wiki ya 2 mpaka ya 6. huwenda pia zikachelewa ama zikawahi. Dalili hizi si zenye kudumu, yaani zitapotea baada ya muda na hazihitaji matibabu yeyote. Katika kipindi ili kiwango cha virusi kwenye damu ni kikubwa sana na huzaliana kwa haraka sana.
Baada ya dalili hizi kutokea bado virusi vya ukimwi haviweze kuonekana kwenye kipimo cha HIV. Itachukuwa kuanzia wiki 3 mapaka miezi mitatu kwa virusi kuweza kuonekana kwenye kipimo na mtu kuambiwa ni muathirika. Katika kipindi hiki mtu anaweza kumuambukiza mtu mwingine kwa uahisi.
Baada ya miezi mitatu ya mwanza dalili zote za HIV hazitaweza tena kuonekana na hapa mtua ataishi kawaida bila ya kuhisi chochote. Virusi vitaanza kupunguwa kwenye damu na kuhamia maeneo mengine ya mwili na kujifucha huko ili kujijengea makazi ya milele. Wakati huu vitaendelea kuchambulia seli za CD4 kidogo kidogo.
Seli za Cd4 ni nini?
Hizi ni seli ambazo kazi yake ni kupambana na vijidudu vya maradhi kama virusi, bakteria, fanfasi na protozoa. Seli hizi zinatafuta vijidudu hivi popote vilipo kwente mwili. Piti vikikutana nae vinatoa kemikali ambazi zitauwa kijidudu hiko. Kwa ufupi wa maneno seli za CD4 NI ASKARI MWILINI. Sasa virisi vya VVU vyenyewe vinatafuta sei hizi za CD4 popote zilipo na kuanza kuzishambulia na kuziuwa. Hii ni sawa na kusema VVU hushambulia askari wa mwili. Na ikitokea askari kapigwa basi mwili hauna ulizi dhidi ya maradhi.
Hatuwa za kufikia UKIMWI
Kikawaida seli za CD4 zipokuanzia 500 mpaka 1600 kwa mtu mwenye afya. Sasa kama tulivyoona kuwa VVU hushambulia seli hizi na kuzimaliza. Hivyo endapo zitafikia chnini ya 200 mtu huyu huambiwa ana upungufu wa kinga mwilini au UKIMWI. Na hadi kufikia hapa huwenda mtu huyu aliambukizwa VVU yapata miaka mitano hadi kumi iliyopita. Kufikia hapa ndipo mtu ataanza kuona dalili za UKIMWI.
Je ni zipi dalili za UKIMWI?
- Kupunguwa ukito bila ya sababu
- Homa za mara kwa mara
- Kuharisha na kutapika kwa mra kwa mara
- Kupata maradhi ya mara kwa mara
- Unaweza kupata TB, na saratani ambazo huhusiana na wenye IKIMWI
- Fangasi za mara kwa mara hasa sehemu za siri
- Kukonda sana
- Kupata upele, ukurutu na ngozi kukauka
- Uchovu mkali sana usio na sababu maalumu
Je ni njia zipi HIV huambukizwa
Kumekuwa na mawazo mengi na potifu kuhusu njia ambazo virusi vya VVU huambukizwa. Hapa tutaona baadhi tu ya njia ambazo VVU huambukizwa. Kisha tutaona njia ambazo watu hudhania huambukizwa ila ukweli ni kuwa haziambukizi njia ambazo VVU huambukizwa ni kama:-
- Kupitia kushiriki ngono zembe na mtu aliyeathirika
- Kushirikiana vitu vyenye ncha kali kama sindano
- Kutoka kwa mama muathirika kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito, kujifunguwa ama kunyonyesha
- Kuingiliana kwa majimaji ya mwili kama kupitia majeraha na vidonda na mtu aliyeathirika
- Kuongezewa damu ya mtu aliye athirika.
Nia hizi haziwezi kuambukiza VVU
- Kugusana
- Kula pamoja
- Kulala pamoja
- Kugusa mkojo wa muathirika
- Mate ya muathirika hayawezi kuambukiza
- Jasho la muathirika haliwezi kuambukiza
Je ipo dawa ya VVU na UKIMWI?
Kwa ufupi dawa ya kutibu na kumaliza VVU hakuna, ila matumaini yapo kuwa itapatikana. Mapka sasa kuna mgonjwa mmoja ambaye ainaaminika amepona kabisa UKIMWI. Ilamatibabu ambayo alipatiwa hayaweza kutumika kwa watu wengine kutokana na hatari yake. M hii inaleta matumaini kuwa tafiti zinahitajika zaidi na kuna matumaini pia ya kupatikana dawa kwa siku za mbeleni.
Kwa sasa tunayo matibabu ambayo atapatiwa muathirika ili kuzuia virusi visiendelee kuharibu kinga za mwili. Matibabu haya yanajulikana kama ART (antirteoviral therapy) ambapo mgonjwa atapatiwa dawa za ARV. Endapo mtu atatumia vyema itamsaidia kuzuia uharibifu wa kinga zake na pia itambunguza hatari ya kuambukiza wengine.
Je vipi kuhusu kinga ya UKIMWI?
Yes kinga ya ukimwi ipo nayo ni kondomu. Kama itatumika vyema inaweza kukinga kwa asilimia kubwa na kumuweka mtu salama. Ila tambuwa kuwa unaweza kutumia kondomu na ukaathirika kwani njia za maambukizi ni njingi. Kazi kuu ya kondomu ni kulinda maambukizi yanayopatikana kwa njia ya ngono. Zingatia haya:
- Unaweza kuathirika kama umenyowa na mwenzio akiwa amenyoa na kukawa na mikato midogo midogo kwenye ngozi na wakati wa ngono majeraha haya yakakutana, kwa bahati mbaya majimaji yakaingiliana na mmoja akawa muathirika mwingine anaweza kauthirika hata kama mnatumia kondomu.
- Kama kutakuwa na muingiliano wa majimaji kama upele, usaha ama majeraha maeneo mengine ya mwili na wakati wa ngono kukatokea muingiliano wa majimaji, na mmoja akiwa muathirika, hii inaweza kuathiri mwengine.
- Endapo kondom itapasuka wakati wa ngono, na majimaji yakaingiliana kupitia michubuko midogo na mmoja akawa muathirika hii inaweza kumuathiri mwingine.
Tukutane makala nyingie tutaona zaidi kwa nini unaweza kufanya ngono na muathirika na usiathirike.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Vyakula Vinavyosaidia Afya ya Uzazi kwa Mwanamke
​Afya ya uzazi kwa mwanamke inategemea sana usawa wa homoni, ubora wa mayai, na mazingira salama ya mfuko wa uzazi. Lishe bora ni nguzo kuu katika kuboresha maeneo haya. Makala haya yanachambua vyakula muhimu vinavyoweza kuongeza uwezo wa kushika mimba, kusawazisha homoni, na kulinda mfumo wa uzazi kwa ujumla, yakisindikizwa na ukweli wa kisayansi
Soma Zaidi...Dalili za Dengue.
Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg
Soma Zaidi...Tabia za kujidhuru (Self-harm): Nini cha kufanya?
Tabia ya kujidhuru kimakusudi ni ishara ya wazi ya maumivu makali ya ndani ya kihisia ambayo mtu anashindwa kuyastahimili. Makala haya yanachambua kwa nini hali hii hutokea, jinsi ya kuacha unyanyapaa, na hatua za vitendo unazoweza kuchukua ikiwa wewe mwenyewe au mtu unayemjali anapitia changamoto hii.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa Brucellosis
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Brucellosis ni maambukizi ya bakteria ambayo huenea kutoka kwa wanyama hadi kwa watu mara nyingi kupitia maziwa ambayo hayajasafishwa au kuchemshwa vizuri na bidhaa zingine za maziwa. Mara chache zaidi, ba
Soma Zaidi...Matumizi ya chumvi nyingi: Hatari kwa afya ya moyo.
Katika ulimwengu wa kisasa, mtindo wa maisha na vyakula vilivyosindikwa vimesababisha ongezeko kubwa la ulaji wa chumvi kupita kiasi. Makala hii inachunguza uhusiano wa moja kwa moja kati ya ulaji wa sodiamu na magonjwa ya moyo. Tutajadili jinsi chumvi inavyoathiri shinikizo la damu, utaratibu wa uharibifu wa mishipa ya damu, na hatua za kivitendo unazoweza kuchukua ili kupunguza matumizi yake kwa maisha bora na marefu.
Soma Zaidi...Dalili za Mafua kwa Watoto Wachanga
Mafua kwa watoto wachanga ni hali ya kawaida, lakini inaweza kuwa na changamoto kwa sababu watoto hawa bado hawana kinga imara. Post hii inatoa mwongozo wa kutambua dalili za mapema na hatua za kuchukua ili kumsaidia mtoto wako apate nafuu.
Soma Zaidi...