picha

Je unazijuwa dalili za Ukimwi na HIV?

Huwenda ukawa ni moja kati ya watu wanaotaka kujuwa juu ya dalili za ukimwi. Kama wewe ni katika watu hawa tambuwa kuwa kuna dalili za VVU (hiv) na dalili za ukimwi. Makala hii itakwenda kukuletea dalili kuu za mwanzo za VVU na HIV kuanzia wiki tatu za mw

JE UNAZIJUWA DALILI ZA UKIMWI?

Yaliyomo

  1. Maana ya VVU na UKIMWI
  2. Historia fupi ya ukimwi
  3. Dalili za vvu
  4. Dalili za ukimwi
  5. Hatuwa za maambukizo ya vvu hadi kufikia ukimwi
  6. Njia za maambukizo ya vvu na ukimwi
  7. Njia za kujikinga na ukimwi

 

Ukiwa na maoni, mapendekezo ama maswali wasiliana nasi kupitia komenti hapo chini ana namba ya simu.

 

  1. Nini maana ya VVU?

VVU ni ufupisho wa maneno Virusi Vya Ukimwi. Hivi ni virusi vinavyo sababisha upungufu wa kinga mwilini. Ni katika aina ya virusi inayofahamika kitaalamu kama retrovisus. Virusi hivi vinaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwingine kwenda kwa mwingini kupitia muingiliano wa majimaji ya mwilini (body fluid). ni vurisi ambavyo kushambulia aina ya seli inayofahamika kama CD4.

 

Nini maana ya UKIMWI?

UKIMWI ni ufupisho wa maneno Upungufu Wa Kinga Mwilini. Upungufu huu hutokea baada ya mwili kushambuliwa na virusi aina ya VVU. Tunasema mtu ana upungufu wa kinga mwilini endapo seli zake za CD4 zitakuwa chini ya 200 kwenye kipimo. Kutoka kupata VVU hadi kuonyesha kupata upungufu wa kinga inaweza kuanzia miaka 5 hadi 5 baada ya maambukizo.

 

Historia fupi ya UKIMWI na asili yake.

Historia ya ukimwi imeanza zamani sana hata kabla ya neno IKIMWI kuanza kutumoka. Kabla hatujaona kwa ufupi hi historia hii ni vyema tukaanza kujuwa nini chanzo cha ukimwi? Kuna utata wa kutokukubaliana kauli juu ya chanzo cha UKIMWI. Wapo wanaodai kuwa ukimwiumetengenezwa kwenye maabara kisha kusambazwa, kuna wanaosea kuwa ni Mwenyezi Mungu ametowa adhabu ila wanasayansi wanaamini kuwa chanzo cha ukimwi ni Masokwe.

 

Kwa ufupi zipo nadharia zaidi ya 10 zinazojaribu kueleza nini chanzo cha UKIMWI. Kisayansi inathibitika kuwa ukimwi chanzo chake huwenda ikawa ni masokwe. Hoja hii pia inatiliwa nguvu na historia katika maeneo mbalimbali kama Kongo na maeneo mengine ya Afrika ya Magharibi.

 

Kwa ufupi ni kuwa tafiti zinaoyesha kuwa virusi vya VVU vilitika kwenye masokwewakati wa uwindaji, huwenda kuitia majeraha ama namna nyingine kulitokea mwingiliano wa majimaji ya mwili na ya sokwe. Virusi vikaanza kubadilika kutoka hatuwa moja hadi nyingine hadi kufikia leo. Kauli hii inatiliwa nguvu baada ya kupatikana kwa taarifa za kihistoria ambazo huwenda miaka ya 1950 watu wa maeneo ya UGANDA NA Kongo1920 walipata upungufu wa kinga Mwilini na walikuwa wanakufa kwa maradhi ambayo yana uhusiano na UKIMWI.

 

Kwa mara ya kwanza dunia ailianza kupata taharuki juu ya uwepo vivirusi hivi miaka ya 1980 ha hapo virusi hivi vikajulikana kwa jina la HTLV-III/LAV na nchini Uganda ugonjwauliosababishwa na virusi hivi ulikuwa ukifahamika kwa jina la slim. Mpaka kufikia mwaka 1986 international Committee on Taxonomy of Viruses wakaviita virusi hivi kama HIV na ugonjwa unaosababihwa na virusi hivi uitwe AIDs na hapo jina UKIMWI ndipo lilipoanzia.

 

Hadi kufikia miaka ya 1988 WHO walitangaza siku ya ukimwi duniani. Mapaka kufikia mwaka 1989 maambukizi kidunia yakafikia 400000 kwa makadirio ya moja wa mataifa. Hadi kufikia mwaka 1990 mwezi wa 10 dawa ya kwanza ya kupunguza makali ya virusi tunazozijuwa hivi leo kama ARV ilitangazwa nayo ilikuwa ni zidovidine (AZT).

 

Ni zipi dalili za mwanzo za HIV?

Hili ni swali la msingi sana na ni zuri pia. Kwa ufupi dalili za mwanzo za HIV huweza kujitokeza kuanzia wiki 2 toka kupata maambikizi, hadi kufikia wiki ya sita toka kupata maambukizi. Kuna wengine wanapita wiki hizi hata bila ya kuona dalili yeyote ile. Lakini pia dalili hizi huweza kuingiliana na maradhi mengine, hivyo haimaanishi kila mwenye dalili hizi atakuwa ni muathirika. Dalili hizo ni kama:-

  1. Kupata homa
  2. Maumivu ya kichwa
  3. Mafua
  4. Miwasho, ukurutu na upele
  5. Vidonda vya koo
  6. Kuvimba na kuuma kwa tezi za kwenye shingo na mapaja (mtoki)
  7. Kubanwa punzi

 

Dalili hizi huweza kuchukuwa muda mchache sana ndani ya wiki za mwanzo wiki ya 2 mpaka ya 6. huwenda pia zikachelewa ama zikawahi. Dalili hizi si zenye kudumu, yaani zitapotea baada ya muda na hazihitaji matibabu yeyote. Katika kipindi ili kiwango cha virusi kwenye damu ni kikubwa sana na huzaliana kwa haraka sana.

 

Baada ya dalili hizi kutokea bado virusi vya ukimwi haviweze kuonekana kwenye kipimo cha HIV. Itachukuwa kuanzia wiki 3 mapaka miezi mitatu kwa virusi kuweza kuonekana kwenye kipimo na mtu kuambiwa ni muathirika. Katika kipindi hiki mtu anaweza kumuambukiza mtu mwingine kwa uahisi.

 

Baada ya miezi mitatu ya mwanza dalili zote za HIV hazitaweza tena kuonekana na hapa mtua ataishi kawaida bila ya kuhisi chochote. Virusi vitaanza kupunguwa kwenye damu na kuhamia maeneo mengine ya mwili na kujifucha huko ili kujijengea makazi ya milele. Wakati huu vitaendelea kuchambulia seli za CD4 kidogo kidogo.

 

Seli za Cd4 ni nini?

Hizi ni seli ambazo kazi yake ni kupambana na vijidudu vya maradhi kama virusi, bakteria, fanfasi na protozoa. Seli hizi zinatafuta vijidudu hivi popote vilipo kwente mwili. Piti vikikutana nae vinatoa kemikali ambazi zitauwa kijidudu hiko. Kwa ufupi wa maneno seli za CD4 NI ASKARI MWILINI. Sasa virisi vya VVU vyenyewe vinatafuta sei hizi za CD4 popote zilipo na kuanza kuzishambulia na kuziuwa. Hii ni sawa na kusema VVU hushambulia askari wa mwili. Na ikitokea askari kapigwa basi mwili hauna ulizi dhidi ya maradhi.

 

Hatuwa za kufikia UKIMWI

Kikawaida seli za CD4 zipokuanzia 500 mpaka 1600 kwa mtu mwenye afya. Sasa kama tulivyoona kuwa VVU hushambulia seli hizi na kuzimaliza. Hivyo endapo zitafikia chnini ya 200 mtu huyu huambiwa ana upungufu wa kinga mwilini au UKIMWI. Na hadi kufikia hapa huwenda mtu huyu aliambukizwa VVU yapata miaka mitano hadi kumi iliyopita. Kufikia hapa ndipo mtu ataanza kuona dalili za UKIMWI.

 

Je ni zipi dalili za UKIMWI?

  1. Kupunguwa ukito bila ya sababu
  2. Homa za mara kwa mara
  3. Kuharisha na kutapika kwa mra kwa mara
  4. Kupata maradhi ya mara kwa mara
  5. Unaweza kupata TB, na saratani ambazo huhusiana na wenye IKIMWI
  6. Fangasi za mara kwa mara hasa sehemu za siri
  7. Kukonda sana
  8. Kupata upele, ukurutu na ngozi kukauka
  9. Uchovu mkali sana usio na sababu maalumu

 

Je ni njia zipi HIV huambukizwa

Kumekuwa na mawazo mengi na potifu kuhusu njia ambazo virusi vya VVU huambukizwa. Hapa tutaona baadhi tu ya njia ambazo VVU huambukizwa. Kisha tutaona njia ambazo watu hudhania huambukizwa ila ukweli ni kuwa haziambukizi njia ambazo VVU huambukizwa ni kama:-

  1. Kupitia kushiriki ngono zembe na mtu aliyeathirika
  2. Kushirikiana vitu vyenye ncha kali kama sindano
  3. Kutoka kwa mama muathirika kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito, kujifunguwa ama kunyonyesha
  4. Kuingiliana kwa majimaji ya mwili kama kupitia majeraha na vidonda na mtu aliyeathirika
  5. Kuongezewa damu ya mtu aliye athirika.

 

Nia hizi haziwezi kuambukiza VVU

  1. Kugusana
  2. Kula pamoja
  3. Kulala pamoja
  4. Kugusa mkojo wa muathirika
  5. Mate ya muathirika hayawezi kuambukiza
  6. Jasho la muathirika haliwezi kuambukiza

 

Je ipo dawa ya VVU na UKIMWI?

Kwa ufupi dawa ya kutibu na kumaliza VVU hakuna, ila matumaini yapo kuwa itapatikana. Mapka sasa kuna mgonjwa mmoja ambaye ainaaminika amepona kabisa UKIMWI. Ilamatibabu ambayo alipatiwa hayaweza kutumika kwa watu wengine kutokana na hatari yake. M hii inaleta matumaini kuwa tafiti zinahitajika zaidi na kuna matumaini pia ya kupatikana dawa kwa siku za mbeleni.

 

Kwa sasa tunayo matibabu ambayo atapatiwa muathirika ili kuzuia virusi visiendelee kuharibu kinga za mwili. Matibabu haya yanajulikana kama ART (antirteoviral therapy) ambapo mgonjwa atapatiwa dawa za ARV. Endapo mtu atatumia vyema itamsaidia kuzuia uharibifu wa kinga zake na pia itambunguza hatari ya kuambukiza wengine.

 

Je vipi kuhusu kinga ya UKIMWI?

Yes kinga ya ukimwi ipo nayo ni kondomu. Kama itatumika vyema inaweza kukinga kwa asilimia kubwa na kumuweka mtu salama. Ila tambuwa kuwa unaweza kutumia kondomu na ukaathirika kwani njia za maambukizi ni njingi. Kazi kuu ya kondomu ni kulinda maambukizi yanayopatikana kwa njia ya ngono. Zingatia haya:

  1. Unaweza kuathirika kama umenyowa na mwenzio akiwa amenyoa na kukawa na mikato midogo midogo kwenye ngozi na wakati wa ngono majeraha haya yakakutana, kwa bahati mbaya majimaji yakaingiliana na mmoja akawa muathirika mwingine anaweza kauthirika hata kama mnatumia kondomu.
  2. Kama kutakuwa na muingiliano wa majimaji kama upele, usaha ama majeraha maeneo mengine ya mwili na wakati wa ngono kukatokea muingiliano wa majimaji, na mmoja akiwa muathirika, hii inaweza kuathiri mwengine.
  3. Endapo kondom itapasuka wakati wa ngono, na majimaji yakaingiliana kupitia michubuko midogo na mmoja akawa muathirika hii inaweza kumuathiri mwingine.

 

Tukutane makala nyingie tutaona zaidi kwa nini unaweza kufanya ngono na muathirika na usiathirike.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/05/18/Wednesday - 07:06:47 pm Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2785

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini

Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wale ambao tayari wameshakuwa na tatizo la asidi mwilini, ni njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza tatizo hili au Mgonjwa anapoendelea kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Sababu zinazoweza kumfanya figo kuharibika.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kufanya figo kuharibika.hili ni janga ambalo linawakumba Watu wengi siku hizi na kusababisha kupoteza maisha kwa wagonjwa wa figo hasa hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kulipia hela ya kusafishia figo.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kitomvuni, sababu zake na dalili zake

Hapa utajifunza sababu za kuwepo na maumovu ya tumbe kitomvuni.

Soma Zaidi...
Namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kuishi na vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Dalili za kifua kikuu kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.

Soma Zaidi...
Dalili, chanzo, sababu na vmambo hatari kuhusu kifua kikuu

Katika makala hii utajifunza kuhusu kifua kikuu, dalili zake, sababu zake, chanzo chake na mambo hatari kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.

Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.

Soma Zaidi...
Madhara ya fangasi.

Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi za ukeni kwa kawaida tunajua kubwa fangasi zikiingia kwenye uke usababisha madhara mbalimbali ambayo mengine yanaweza ya kudumu na mengine ya mda kama yametibiwa mapema.

Soma Zaidi...
Dalili za madhara ya ini

Ini Ni kiungo kikubwa Sana mwili na hutumika kuondoa sumu mwili ambayo hujulikana Kama detoxification

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa pepopunda kwa watoto

Pepopunda ni ugonjwa hatari wa kutishia maisha unaosababishwa na sumu inayojulikana Kama tetanospasmin inayotolewa kwenye majeraha yaliyoambukizwa. Bakteria ya pepopunda huingia kwenye mwili wa mtoto mchanga kupitia kisiki cha kitovu ambacho kimekatwa na

Soma Zaidi...