Malezi ya Mtoto Mchanga baada ya Talaka
Mtoto mchanga hataachanishwa na mama yake mpaka awe na umri wa miaka miwili - umri wa kuacha kunyonya. Matumizi ya mama na mtoto katika kipindi hiki cha kunyonya mtoto yatakuwa juu ya mume japo mkewe aliyemtaliki atakuwa kwa wazazi wake au penginepo nje ya nyumbani kwake. Lakini mume na mke walioachana, wakiridhiana wanaweza kumwachisha kunyonya kabla ya miaka miwili au wanaweza kumkodisha mwanamke mwingine amnyonyeshe. Hukumu hii ya malezi ya mtoto baada ya mume na mke kuachana inabainishwa vyema katika Qur-an:
Na wanawake waliozaa wawanyonyeshe watoto wao miaka miwili kamili; kwa anayetaka kukamilisha kunyonyesha; na ni juu ya baba (yake) chakula chao (hao watoto na mama) na nguo zao kwa sheria. Wala haikalflshwi nafsi yoyote ila kwa kadiri ya wasaa wake. Mama asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake, wala baba (asitiwe taabuni kwa ajili ya mtoto wake).
Na kama wote wawili wakitaka kumwachisha ziwa (kabla ya miaka miwili), kwa kuridhiana na kushauriana, basi sio kosa juu yao. Na kama mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha (wengine wasiokuwa mama zao) basi haitakuwa dhambi juu yenu kama mkitoa (kuwapa hao wanyonyeshaji) mlichowaahidi kwa sharia. Na mcheni Mwenyezi Mungu na jueni kwamba Mwenyezi Mungu anayaona yote mnayoyatenda. (2:233)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu mambo ambauo ni haramu kwa mtu asiye na udhu.
Soma Zaidi...Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno ยSwalaatย lina maana ya ยombi au ยdua.
Soma Zaidi...Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu.
Soma Zaidi...(b) WarumiJamii ya Warumi nayo ni miongoni mwa jamii zinazohesabika kuwa zilianza kustaarabika mapema katika historia ya ulimwengu.
Soma Zaidi...Nguzo za uislamu,umuhimu na msisitizowa zakat na sadaqat katika uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO.
Soma Zaidi...Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake?
Soma Zaidi...